Header Ads Widget

Responsive Advertisement

TAFSIRI NA UKALIMANI NI TAALUMA MUHIMU SANA ULIMWENGUNI.







DHANA  YA  TAFSIRI
Kwa mujibu wa Mwansoko na wenzake (2006) wanaeleza kuwa tafsiri ni zoezi la uhawilishaji wa mawazo katika maandishi kutoka lugha moja hadi nyingine. Woa wanatilia mkazo katika zoezi la uhawilishaji na kinachohawilishwa ni mawazo katika maandishi.
Pia Catford (1965) anaeleza kuwa, kutafsiri ni kuchukua mawazo yaliyo katika maandishi kutoka lugha mmoja yaani lugha chanzi na kuweka badala yake mawazo yanayolingana kutoka katika lugha nyingine yaani lugha lengwa. Hapa msisitizo upo katika matini zilizoandikwa na kuzingatia zaidi ujumbe au wazo lililopo katika matini chanzi lijitokeze vile vile katika matini lengwa. Mawazo haya hayawezi kuwa sawa kabisa na ya matini chanzi bali ni mawazo yanayolingana toka matini chanzi na matini lengwa, hii ni kutokana na sababu tofauti kama vile utamaduni, historia, kiisimu na mazingira.
Naye Newmark (1982) anaeleza kuwa tafsiri ni mchakato wa uhawilishaji wa maneno kutoka matini chanzi kwenda matini lengwa.
Pia Nida na Taber (1969) wanaeleza kuwa tafsiri hujumuisha kuzalisha upya ujumbe wa lugha chanzi kwa kutumia visawe vya asili vya lugha lengwa vinavyo karibiana zaidi na lugha chanzi kimaana na kimtindo. Wao wanatilia mkazo uzalishaji upya wa kwa kutumia visawe asili vinavyokaribiana na matini chanzi kimaana na kimtindo. Kutokana na maana hizi tunaweza kusema kuwa tafsiri hufanywa katika ujumbe uliopo katika maandishi, ni jaribio la kiuhawilishaji na wazo linalatafsiriwa huwa na visawe vinavyokaribiana na sio sawa kutokana na tofauti za kiisimu, kihistoria, kiutamaduni na mazingira.
Kwa  ujumla  tunaweza  kusema
Tafsiri  ni  taaluma  inayohusika na  uhaulishaji  wa   mawazo kutoka  lugha  chanzi  kwenda lugha  lengwa   kwa  maandishi bila  ya  kupoteza , kupotosha  na kubadili  maaana .mawazo yanayoshugulikiwa  katika taaluma  ya  tafsiri  sharti  yawe kwenye  maandishi  na  yalingane kati  ya  lugha  lugha  asilia  na lugha  lengwa.

AINA  ZA  TAFSIRI
Tafsiri  ya  neno   kwa  neno ,  Hii ni  tafsiri  amboyo  mofimu  na maneno  mengine  hufasiriwa yakawa  pwekepweke  kwa kuzingatia  maana  zake  za msingi  bila  kujali  muktadha. Mpangilio  wa  mofimu  na  lugha chanzi  hubaki  vilivile , maneno yanayofungamana  na  utamaduni  hufasiliwa  kisisisi .matini  ya tafsiri (matini  lengwa) huwandikwa  chini  ya  matini  ya lugha  chanzi
Mfano  (1) Kiswahili        : a – li – lala – hadi –asubuhi
                 Kiingereza        : she /past /sleep/  until / morning
             (ii) kiwahili           : a  -likwenda / nyumbani / kwke
                Kiingereza          : he / past / until /at /house /his.

Ø  Ubora  wa  tafsiri  neno  kwa  neno
Tafsiri  ya  aina  hii  humsaidia kumsaidia  kuelewa  jinsi  lugha inavyofanya  kazi  katika kuanisha  muundo
Ø  Udhaifu  wa  tafsiri  ya moja  kwa moja
Upungufu  wa  tafsiri  ya  neno kwa  neno  ni  kwamba  mara nyingi  haitoi   kwa  uangavu maana  inayokusudiwa  kwa sababu  nahau  na  misemo inayohusika  na  utamaduni hufasiliwa  kisisisi.
sababu  nahau  na  misemo inayohusika  na  utamaduni hufasiliwa  kisisisi.
Tafsiri  sisisi
Kwenye  aina  hii  ya  tafsiri maneno  hufasiliwa  yakiwa pwekepweke  kwa  kuzingatia maana  zake  za  msingi  katika lugha chanzi  bila  kujali  sana muktadha . lakini  kufuatana  na mfumo  wa  kisarufi ,hususani sintaksia  ya  lugha  lengwa

Mfano    kiingereza      :He  was taken  a  centrel  police  station

               kiswahili       : Alipelekwa kwenye  kituo  cha  kati  cha  police ( badala  ya  kituo        

                                      kikuu  cha police)

           kiingereza        :Dear  listener , lend  me  your  ears

             kiswahili          : Wasikilizaji wapendwa , niazimeni  masikio yenu (badala  ya naomba 

                                     mnisikilize.
Mfano   Kiingeza   : Two  heads are  better  than one
              Kiswahili   : Mbili  vichwa ni  bora  kuliko  moja .(badala yake  vichwa  viwili  ni  bora 
                                  kuliko  kichwa  kimoja
              Kizaramo   : Zege dimlemelwe  fisi ,mbwa  domgela muhe.
               Kiswahili   : Mfupa uliomshinda  fisi  mbwa  utampa pumu
Ø  Ubora  wa  tafsiri  sisisi  :
 Tafsiri  hii  husaidia  sana  mfasiri kuwa  hakuna  maaana  ya kudumu  ya  maneno , bali  maana halisi .Kutokana  na  matumizi yake  katika  muktadha  maalumu aidha  aina  hii  ya  tafsiri hutumika  sana  katika  tafsiri  ya vichekesho  kwani  huibua ukinzani  wa  ajabu  katika  tungo .(Mfano; My name is Dr Livingstone I come from Johanesberg
Ø  Upungufu  wa  tafsiri  sisisi  : Tafsiri  sisisi  agharabu  hutoa tafsiri  potofu  na  kwa  hiyo  huwa na  uwezekano  wa  kuleta     utata na  hasara  katika  mawasiliano

Tafsiri ya kisemantiki/maana/uwazi/(semantic trasilation)   hii ni aina ya tafsiri ambayo mfasiri huegemea zaidi kwenye kugha chanzi. Katika aina hii ya tafsiri, mfasiri hufasiri kila neno katika sentensi jinsi ilivyo ila kwa kufuata sarufi hususani vipengele vya kisemantiki na kistakisia ya lugha chanzi.Katika aina hii ya tafsiri masahihisho au ya neno au jambo lolote unalodhani limekosewa haliruhusiwi isipokuwa uweza kuweka haya marekebisho hayo au ufafanuzi katika tanbihi. (mujibu wa( Catford na Nida 1965)
Mfano  :  Kizaramo    :  kihanga cha  mkulu  kilava  nongo  ya ugimbi.
                 Kiswahili    : uso  wa mkubwa  umetoa  mtungi  wa pombe
                 Kizaramo     :ngwengwe hadisolo  jake
                  Kiswahili     : dume  la njani  huwa  na  mamlaka  zaidi katika  eneo  lake
Ø  Ubora  wa  tafsiri  :
Ubora  wa  tafsiri  ni  kuwa  na uwezo  mkubwa wa  kuendeleza lugha  legwa kwa  kuingiza  miundo  na  misemo  toka  lugha asilia .
Ø  Udhaifu  wa  tafsiri  :
 tafsiri  hii  haitilii  maanani  nahau , misemo  maalumu  inayohusiana na  utamaduni  na  lugha inayolengwa  katika  tafsiri . Mfano  (Assaina  married  Mtillah. –kiwahili :Assaina  alimuoa Mtillah)  badala Asha  kuolewa  na Moses  kwani  katika Kiswahili mwanamke  huwa  anaolewa  na mwanaume  ndiye  anaoa  hii huweza  kuleta  utata  katika lugha  ya  kiwahili  kwa mwanamke  ndiye  kuoa  na mwanaume  kuolewa.

Tafsiri  ya  kimawasiliano ,
hii  ni  aina  ya  tafsiri  ambayo huzingatia  hadhira ya  matini  ya lugha  lengwa   kwa  kumjali  sana msomaji  wa  matini  hiyo . hii  ni tafsiri  huru  kwa  sababu  mfasiri anaweza  kuongeza  au kupunguza  maneno  ya  matini ya  lugha  asilia wakati  wa kufasili  ili  mradi  ujumbe uwafikie  kwa  namna inayotakiwa  na  bila  kupoteza wazo   la  matini  ya  lugha  asilia, mfasiri  ana  uhuru  wa  kutafuta maneno  au  mafungu  ya  maneno yanayolingana  na  nahau,misemo ,methali , utamaduni  na mazingira  ya  lugha  lengwa

Ø  Ubora  wa  tafsiri  mawasiliano
Ubora  wa  tafsiri  hii  ya kimawasiliano  ni  kwamba hufuata  kanuni  taratibu  na sheria  za  lugha  lengwa  na kuzingatia  mweelekeo  wake  wa kiutamadudi ,kiistoria ,kimazingira  na  kijamii  kwa hadhira  lengwa
Mfano
Kiingereza    : Veronika  married chris
Kiswahili       :chris  alimuoa veronica

Ø  Udhaifu  wa  tafsiri  mawasiliano
Kutokuwa  na  uwezo  wa kuendeleza  ,kuingiza  miundo  au misemo  kutoka  lugha  asilia kwenda  katika  lugha  lengwa. Hali   hii  inatokana  na  ukweli kuwa  tafsiri  hii  haizingatii miundo ,misemo , na  msamiati wa  lugha  asilia  wakati  wa kufasiri  bali  huzingatia  wazo  la jumla  la kiutamaduni  kwa  lugha lengwa
Udhaifu  mwingine  katika  tafsiri ya  kimawasiliano hujitokeza  pale mfasiri  anapoegea  sana  kwenye mawzo , historia ,utamaduni , mazingira  na  itikadi  ya  lugha lengwa . kwa  mfano  katika mwaka  2002  vyombo  vya  habari vilisikika  vikitangaza
Mfano kiingereza  : His  excellency president  saddam  Hussein (vyombo  vya  habari  vya
Iraq     mwaka  2002)
Kiswahili    :Gaidi  saddam Hussein  ( vyombo  vya  habari vya  marekani  mwaka 2002
Kutokuwa  na  uwezo  wa kuendeleza  ,kuingiza  miundo  au misemo  kutoka  lugha  asilia kwenda  katika  lugha  lengwa. Hali   hii  inatokana  na  ukweli kuwa  tafsiri  hii  haizingatii miundo ,misemo , na  msamiati wa  lugha  asilia  wakati  wa kufasiri  bali  huzingatia  wazo  la jumla  la kiutamaduni  kwa  lugha lengwa
Udhaifu  mwingine  katika  tafsiri ya  kimawasiliano hujitokeza  pale mfasiri  anapoegea  sana  kwenye mawzo , historia ,utamaduni , mazingira  na  itikadi  ya  lugha lengwa . kwa  mfano  katika mwaka  2002  vyombo  vya  habari vilisikika  vikitangaza
Mfano kiingereza  : His  excellency president  saddam  Hussein (vyombo  vya  habari  vya
Iraq     mwaka  2002)
Kiswahili    :Gaidi  saddam Hussein  ( vyombo  vya  habari vya  marekani  mwaka 2002)




                                                        MAREJEREO
Catford J.C. (1965) A Linguistic theory of Translation: OUP London.
Mwansoko, H.J.M. na wenzake (2006) Kitangulizi cha Tafsiri: Nadharia na Mbinu: TUKI
                         Dar es Salaam.
Newmark, P. (1988) A Textbook of Translaton. : Prentice Hall London.
Nida, A. E. na Charles, R. T. (1969)The Theory and Practice of Translation. The United
                       Bible Societies: Netherlands.
Wanjala S. F (2011) Misingi ya ukalimani na tafsiri; Serengeti Education publisher (T)
                      L.T.D. Mwanza