Header Ads Widget

Responsive Advertisement

AZAM MEDIA YAWALILIA WAFANYAKAZI WAKE WALIOFARIKI KATIKA AJALI




Katika taarifa waliyotuma katika mitandao yao ya kijamii waliandika yafuatayo

TANZIA

Uongozi wa Azam Media Limited umethibitisha vifo vya wafanyakazi wake watano wakiwa ni miongoni mwa watu saba waliofariki kwenye ajali ya gari iliyotokea kati ya Shelui na Igunga. Wawili wapo mahututi, mmoja hali yake si mbaya.

Ajali hiyo imetokea wakiwa njiani kuelekea Chato kwa ajili ya kwenda kuonesha shughuli ya TANAPA ambapo mgeni rasmi alitarajiwa kuwa Rais John Magufuli

Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi Ameen.

#WapumzikekwaAmani #AzamtvApp #AzamUTV #AzamTWO #UFMRadio

Post a Comment

0 Comments