Afunguka A – Z jinsi Tukio Lilivyokuwa,Walipopelekwa na Jinsi Walivyoteswa na Kutupwa Mtaroni..!

Anaeongea kwa sasa ni msanii Roma na anatoa shukrani kwa wote bila kujali itikadi zao, anasema kilichowapata watu wafanye kama case study.
Roma anasema hawana uhakika wa usalama wao hata kidogo, amesema nature ya tukio, studio zilizopo Tongwe records yuko tangu 2007 na ni eneo salama sana. Amesema wana majirani wanaowapa amani sana ikiwemo ujirani na Tibaigana, Waitara na mstaafu mmoja wa Magereza.
Amesema hofu hiyo isiishie kwao kwani inaweza ikarudi kwa yeyote muda wowote, mtu yeyote inaweza kumkuta. Amedai wao ni wachanga mno na hawawezi kupambana na yeyote. Anasema Bin Laden hayuko sawa na anastuka sana mpaka kuwastua watu wote.
Amedai kuna watu wanaamini hakuna kilichotokea kwa kudhani ni kiki na wengine wanasema wanatumika kisiasa labda kuchafua serikali.
ROMA: Tunatafuta ruzuku yetu kupitia mziki, tumelia sana kwa haya maneno tena mengine kutoka kwa watu wa karibu sana ikiwemo wanamuziki, si kweli. Tunaishi familia za kawaida na hatuwezi kurisk maisha yetu kwa ajili ya hela au sababu nyingine yeyote.
Kilichotokea ni kweli, nadhani mnaona mwili wangu(anaonyesha), linatuumiza sana mtu kusema tumepewa dola 5,000. Tumeumia, tumepigwa kiukweli na tumeripoti kwenye vyombo vya dola.
0 Comments