Header Ads Widget

Responsive Advertisement

KENYA: Tume ya uchaguzi yaahirisha uchaguzi

Tume ya uchaguzi nchini Kenya IEBC imetangaza kuhairishwa kwa uchaguzi wa urais ambao ulitarajiwa kuandaliwa tarehe 28 mwezi huu katika kaunti nne magharibi mwa Kenya yaliyo kwenye ngome ya upinzani.

Kaunti hizo ni pamoja Migori, Siaya, Kisumu na Homa Bay.

Uchaguzi huo ulihairiswa kwa sababu za kiusalama maeneo hayo wakati wafuasi wa upinzani wakipinga kufanyika marudio ya uchaguzi

Katika taarifa yake Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alisema kuwa tume imechukua hatua hiyo ili kulinda maisha ya wafanyakazi wake.

Post a Comment

0 Comments