DHANA YA MOFOLOJIA, MOFOFONOLOJIA NA MICHAKATO YA KIMOFOFONOLOJIA
Na Mwl. Kagita I.S.A
Katika makala hii nitaanza kueleza maana ya fonolojia, mofolojia na mofofonolojia kwa kutalii wataalamu mbalimbali, kisha nitaeleza michakato ya kimofofonolojia nikijigeza katika mawazo ya wataalamu tofautitofauti.
Wataalamu mbalimbali wamefasili fonolojia na mofofonoloji kama ifuatavyo;
Kwa mujibu wa Mugulu (1999), akimrejelea Fudge (1973) anasema kwamba fonolojia ni kiwango kimojawapo cha lugha fulani kilicho na vipashio vidogo zaidi kuliko vipashio vingine vyote vya lugha. Vipashio vya kifonolojiani fonimu na alofoni zake.
Dosari ya fasili hii ni kwamba haijafafanua kiwango kipi cha lugha ambacho kinahusika na fonolojia kwani lugha inaviwango mbalimbali.
Massamba (2010) anasema kuwa fonolojia ni tawi la isimu linalojishughulisha na mfumo wa sauti (asilia) za lugha. Hii inamaana kwamba, kila lugha mahususi inamfumo wake wa sauti ambamo maneno hujengwa. Ki ukweli fonolojia hujihusisha na namna sauti zinavyotumika katika maneno ya lugha mahususi katika kuleta maana.
Massamba na wenzake (2004) wanafafanua kuwa, fonolojia ni tawi la isimu ambalo hujishughusha na uchunguzi, uchambuzi na uainishaji wa sauti pambanuzi ambazo hutumika katika mifumo mbalimbali ya sauti za lugha za binadamu.
John Habwe na Peter Karanja (2004) wanaeleza kuwa; fonolojia ni utanzu wa isimu unaochunguza jinsi sauti za lugha zinavyofanya kazi katika lugha mbalimbali. Fonolojia huchunguza jinsi sauti hizo zinavyotumika, zinavyounganishwa na kupangwa katika lugha yoyote mahususi ili kuunda tungo zenye maana.
Pia maana ya mofofonolojia imeelezwa kama ifuatavyo;
Massamba (2010) akimnukuu Martinet (1965) ambapo Martinet alinukuu kutoka kwa Trubetzkoy (1929) anaeleza kuwa; mofofonolojia kama ilivyotumiwa na Trubetzkoy ilimaanisha sehemu ya isimu ambayo ingeweza kutumia mofolojia kuelezea tofauti fulani za kifonolojia ambazo zisingeweza kuelezwa kwa kutumia data za kifonolojia peke yake.
Dhana ya michakato ya fonolojia na mofofonolojia imejadiliwa na wataalam mbalimbali kama ifuatavyo;
Tuki (2004) inaeleza kuwa mchakato ni mfululizo wa shughuli unaosababisha kitu fulani kufikiwa.
Hivyo katika uwanja huu wa fonolojia tunaweza kusema kuwa mchakato utakuwa unafanyika pale ambapo mofimu mbili zinapokutanishwa huweza kutokeza mabadiliko fulani katika mofimu mojawapo au kutotokea badiliko lolote. Mfano viungu hubadilikia kuwa vyungu,kietu hubadilika kuwa chetu hapa tunaona kuwa mabadiliko yametokea lakini miti hubakia kuwa miti, kiti hubakia kuwa kiti na hapa tunaona kuwa hakuna mabadiliko yoyote yaliyotokea.
Massamba (2011) anaeleza kuwa kuna aina mbili za michakato asilia yaani mchakato usilimisho na mchakato sio-usilimisho. Mchakato wa kiusimilisho anasema kuwa, usilimisho ni pale ambapo kitamkwa kimoja hufanywa kifanane na kitamkwa kilicho jirani yake kwa maana kwamba hupata baadhi ya sifa za kipande sauti chenziye kilicho jirani. Kwa mfano, konsonanti inaweza kupata baadhi ya sifa za irabu au irabu ikapata baadhi ya sifa za konsonanti, na konsonanti moja huweza kuathiri konsonanti nyenziye au irabu moja huweza kuathiri irabu nyenziye. Pia anaendelea kusema kuwa usilimisho unaweza kuhusisha michakato kadhaa kama vile,unazalishaji wa irabu, utamkiaji pamwe wa nazali, ukaakaishaji, ughunishaji kati irabu, uhafifishaji kati irabu, tangamano la irabu, ughunishaji konsonanti shadda, muungano.
Pia,Habwe na Karanja (2004), wanaeleza kuwa usilimisho ni kule kufanana kwa fonimu kwa kiasi au kikamilifu kutokana na kuathiriana. Hapa sauti jirani katika neno huathiriana kiasi kwamba fonimu hupokea ama kupoteza sifa za kifonetiki kwa fonimu jirani, na matokeo yakiwa kuwa fonimu hizi hukabiliana sana katika kufanana. Pia wanaendelea kusema kuwa usilimisho unaweza kuhusisha kuimarika, kodhoofika, kuingizwa, kudondoshwa, au kuungana kwa fonimu katika neno.
Hivyo basi katika mchakato huu wa usilimishaji tunapata aina kuu mbili za usilimishaji kama zifuatazo;
Usimilisho wa nazali; ni aina ya usilimisho ambao nazali huathiriwa na konsonanti inayofuatana nayo hivyo nazali inasimilishwa yaani hutamkiwa mahali pale ambapo konsonanti inatamkiwa. Kwa mfano nazali zote hutumia msimbo “N”
Kwa hiyo, [ l ] [ d ] N-
[ r ] [ d ] N-
Hivyo basi, fonimu konsonanti / l / na / r / zinzpokzribiznz nz irabu haziathiriki lakini zinapotanguliwa na / n / hubadillika na kuwa / d / na zote hutamkiwa kwenye ufizi.
.Mfano
umbo la ndani
|
umbo la nje
|
/n+buzi/
|
[mbuzi]
|
/n+bwa/
|
[mbwa]
|
/n+bu/
|
[mbu]
|
/n+gongo/
|
[mgo go]
|
/n+gozi/
|
[ gozi]
|
/n+vua/
|
[ vua]
|
/n+vivu/
|
[ vivu]
|
Usilimisho wa Konsonanti ni aina ya usilimisho ambao konsonanti huathiriwa na nazali inayofuatana nayo hivyo konsonanti inasimilishwa yaani hutamkiwa mahali pale ambapo nazali inatamkiwa. kuna baadhi ya sauti ambazo huathiriwa na nazali “n” inapokuwa inaandamia yaani kuna sauti ambazo huathiriwa zinapokaribiana au karibiana moja kwa moja na nazali “n”. mara nyingi hutokea katika maumbo ya umoja na uwingi katika maumbo ya maneno
Mfano:-
Umbo la nje
|
umbo la ndani
|
Ulimi
|
u+limi
|
Ndimi
|
u+limi
|
Urefu
|
u+refu
|
Ndefu
|
n+defu
|
Kwa hiyo kama vile ulimi mrefu
|
Ndimi ndefu
|
Hapa tunaona kwamba sauti [ l ] na [ r ] zinapokaribiana na irabu na irabu haziathiriki lakini zinapokaribiana na nazali “n” hubadilika na kuwa “d”
Kanunixxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Pia kuna michakato isiyo ya kiusimilishokama ifuatayo;
Uyeyushaji
Uyeyushaji, wataalamu wengine huita irabu kuwa nusu irabu Mgullu (1999). Huu ni mchakato ambapo irabu irabu za juu /u/ na /i/ hubadlika na kuwa /w/ au / j/ katika mazingira ya kufuatiwa na irabu zisizofana nazo. Kwa kifupi ni kwamba /u/ inapofuatiwa na irabu yoyote isiyofanana nayo hubadilika kuwa [w] na /i/ ikifuatiwa na irabu yoyote isiyofanana nayo hubadilika na kuwa [j].
Hivyo uyeyushaji ni kanuni inayoelezea mabadiliko ya sauti (irabu) na kuwa kiyeyusho aidha [w] au [j] hii ni kwa irabu zote za juu zinapofuatana na sauti zingine zisizofanana nazo. Na sauti hizo hubadilika katika mazingira ya /u/ hubadilika kuwa [w] inapofuatana na irabu nyingine isiyofanana nayo na / i/ inabadilika na kuwa [ϳ] pia inapofuatana na irabu isiyofanana nayo.
Mfano wa /u/
umbo la ndani
|
umbo la nje
|
/mu+aminifu/
|
[mwe:mbamba]
|
/ku+enu/
|
[kwe:nu]
|
/mu+ anafunzi/
|
[mwa:nafunzi]
|
/mu+eupe/
|
[mwe:upe]
|
/mu+embe/
|
[mwe:mbe]
|
Hivyo tunaona wazi kabisa kuwa irabu ya juu nyuma /u/ imebadilika na kuwa kiyeyusho [w] katika mazingira ya kuatiwa na irabu isiyofanana nayo ambayo ni /a/ na /e/ kwa hapo juu lakini hata ikiwa ni /o/ huweza kubadilisha.
Mfano wa irabu /i/
/umbo la ndani/
|
[umbo la nje]
|
/mi+embe/
|
[mje:mbe]
|
/mi+endo/
|
[mje:ndo]
|
/mi+ezi/
|
[mje:zi]
|
/mi+anzo/
|
[mja:nzo]
|
/mi+eusi/
|
[mwe:usi]
|
/mi+oyo/
|
[mjo:jo]
|
Hivyo tunaona kuwa irabu ya juu mbele /i/ hubadilika na kuwa [j] inapofuatana na irabu nyingine isiyofanana nayo ambayo ni /e,a na o/.
Ukaakaishaji
Mgullu (1999) akimnukuu Les (1984), anadai kuwa ukaakaishaji wa fonimu hutokea ambapo fonimu zisizo za kaakagumu zinapobadilika na kuwa za kaakagumu. Katika Kiswahili sauti za kaakagumu zipo mbili tu yaani /ɟ/ na /ʧ/ ambazo ni vizuiwa kwamizwa. Anamalizia kwa kusema kuwa ukaakaishaji wa fonimu hutokea wakati ambapo fonimu zisizo vizuiwa kwamizi hubadilika na kuwa vizuiwa kwamizwa. Hii katika ukokotozi wake unakuwa kama ifuatavyo.
umbo la ndani
|
umbo la nje
|
umbo la nje
|
/ki+enu/
|
[kjenui]
|
[ enu]
|
/ki+eusi/
|
[kjeusi]
|
[ eusi]
|
/ki+ombo/
|
[kjombo]
|
[ ombo]
|
/ki+umba/
|
[kjumba]
|
[ umba]
|
/ambaki+o/
|
[ambakjo]
|
[ambao]
|
Hapa tunaona kwamba kipasuo cha kaakaalaini /k/ hubadili mahali pa matamshi na kuwa kizuiwa kwamizi /ʧ/ cha kaakaagumu katika mazingira ya kufuatiwa na sauti /ϳ/.
Tangamano la irabu.
Huu ni mchakato ambao irabu fulani hukubali kuandamana katika mazingira maalumu. Kwa mfano mofu [i] na [e] katika lugha ya Kiswahili huonekana kama alomofu au maumbo mbalimbali ya mofu moja ya kutendea na kutendesha, lakini utokeaji wake hutegemeana na mofu itakayojitokeza katika mzizi. Kama irabu ya mzizi ni /i/, /u/ au /a/ basi irabu ya kiambishi cha utendea lazima kiwe ni [i] , wakati irabu ya mzizi ikiwa ni /e/ au /o/ katika hali ya utendea kiambishi chake kitakuwa ni [e]. Mfano.
umbo la ndani
|
umbo la nje
|
/imb+a/
|
[Imb-i-a]
|
/andik+a/
|
[andik-i-a]
|
/dak+a/
|
[dak-i-a]
|
/chun+a/
|
[ un-i-a]
|
/og+a/
|
[og-e-a]
|
/ ez+a/
|
[ ez-e-a]
|
/kom+a/
|
[kom-e-a]
|
Hapa mofimu ya utendea ina alomofu mbili ambazo ni /i/ na /e/ ambapo alomofu /i/, inatokea pale ambapo irabu ya mzizi inakuwa na /i/,/u/ na /a/ wakati ambapo alomofu /e/ inatokea wakati irabu ya mzizi ikiwa ni /e/ na /o/.Kinachoonekana hapa ni kwamba irabu zinatangamana kwa kufuata mahali pa matamshi. Kwa mfano kama irabu ya mzizi ni ya juu basi irabu ya utendea pia itakuwa ni ya juu, na irabu ya mzizi ikiwa ni ya kati basi irabu ya utendea pia itakuwa ya kati,na irabu ya chini siku zote inaonekana kuwa ni ya juu.
Udondoshaji, kanuni hii inahusu kuachwa kwa sauti fulani katika matamshi wakati mofimu mbili zinapokaribiana yaani katika mazingira hayo hayo ya sauti ambayo ilikuwepo hapo awali hutoweka.hapa kuangalia umbo la ndani la neno na umbo la nje.
Kwa mfano irabu /u/ ikifuatiwa na konsonanti halisi basi irabu hiyo hudondoshwa, kama inavyooneshwa hapa chini.
umbo la ndani umbo la nje
Muguu mguu
Mutu mtu
Mujapani mjapani
Musichana msichana
Kanuni; /u/ Ø k[halisi]
Mara nyingi irabu “u” katika mofimu “mu” ikabilianapo na na mofimu fulani hasa konsonati halisi katika mpaka wa mofimu, irabu “u” hudondoshwa lakini inapokabiliana na irabu inayofanana nayo hubaki kama ilivyo.
Mfano; Muumba- muumba
Muumini- muumini
Muuguzi-muuguzi
Muungwana- muungwana
Pia udondoshaji hutokea pale ambapo irabu mbili zinapofuatana katika mpaka wa mofimu, kwa mfano
Umbo la ndani Umbo la nje
Zietu zetu
Hautaki hutaki
Chaake chake
Kanuni; /I/1 Ø /I/2
Yaani irabu ya kwanza inadondoshwa katika mazingira ya irabu hiyo kufuatiwa na irabu ya pili.
Muungano wa irabu, kanuni hii hutokea pale ambapo irabu ya mofimu moja inapokabiliana na irabu ya mofimu nyingine katika mpaka wa mofimu irabu hizo huungana na kuzaa irabu moja, na irabu hizo sharti moja iwe ya chini na nyingine ya juu.
Mfano;
Umbo la ndani
|
Umbo la nje
|
Wa + enya
|
wenye
|
Wa + ingi
|
wengi
|
Ma + ino
|
meno
|
Wa + izi
|
wezi
|
Wa + enzi
|
wenzi
|
Ma+ino
|
Meno
|
Wa+izi
|
wezi
|
Kanuni; /a+i/=e mpakani mwa mofimu.
Lakini kanuni hii haifanyi kazi wakati wote kwani kuna mazingira mengine ambayo haifuati hasa katika mofimu mnyambuliko
Mfano:-
Wa + igizi +a +ji - waigizaji
|
Wa+ingereza - waingereza
|
Wa +oko+a+ji - waokoaji
|
Wa+ite - waite
|
Mwisho, taaluma ya mofolojia na fonolojia licha ya kuwa na uhusiano mkubwa kupitia athari zilizojadiliwa hapo awali, taaluma hizi zina usigano mkubwa hii ni kwa sababu fonolojia inajishughulisha na uchambuzi na ufafanuzi wa sauti za lugha mahususi lakini fonolojia inahusika na uchambuzi wa maumbo ya sauti (maneno) bila kujali kuwa ni ya lugha mahususi au laa!.
MAREJEO
Habwe, J na Peter K. (2004) Misingi ya sarufi ya Kiswahili. Phoenix Publishers: Nairobi.
Massamba,D.P.B. (2011) Maendeleo Katika Nadharia ya Fonolojia. Taasisi ya Taaluma za
Kiswahili (TUKI): Dar es Salaam.
Mgullu, R.S. (1999) Mtalaa wa isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili. Longhorn Publishers Ltd: Nairobi
TUKI, (2004) Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Oxford University Press: Nairobi.
TANBIHI; Ikumbukwe kuwa makosa ya kiuandishi yatakayojitokeza katika makala hii hayana uhusiano wowote na vyanzo rejewa hapo juu.