Header Ads Widget

Responsive Advertisement

mjadala kuhusu jinsi Historia, Utamaduni, na Itikadi zinavyo pambanua mawanda ya ulinganishaji wa kazi za kifasihi





   MWANDISHI : SALOME CLOUDY
   UDSM IKS 2019


Katika mjadala huu umegawanywa katika sehemu tatu. Sehemu ya kwanza ni utangulizi ambayo inahusu fasili ya fasihi linganishi, sehemu ya pili ni kiini cna mwisho ni hitimisho.

Wellek na Warren (1948) wamefasili dhana ya fasihi linganishi kuwa ni mbinu itumiwayo na wahakiki wengi wakazi ya fasihi hata wasayansi kwakujadili njia maalumu ya usomaji wa sanaa mbalimbali ulimwenguni. Ulinganishi unaweza kuwa wa fasihi ya Kiafrika na Kizungu ama fasili ya kizungu dhidi ya Kihindi. Ulinganishi unahusu ulinganishaji wa kazi za mataifa mbalimbali na sio za kitaifa peke yake. 

Vilevile Henry Remark (1971) anafasili fasihi linganishi kama uwanja wa kifasihi unao husika na uchanganuzi na mahusiano ya kifasihi, nje ya mipaka ya nchi moja na fani nyinginezo. Mawazo ya mtaalamu huyu hayatofautiani sana na mawazo ya wataalamu walio tangulia ingawa mtaalamu huyu anaongeza swala la ulinganishi wa fani nyinginezo.

Kwa ujumla fasihi linganishi ni ulinganishi wa kazi za kifasihi baina ya mwandishi mwenyewe, mwandishi na mwandishi mwingine, jamii na jamii au taifa na taifa. Sehemu inayofuata ni jinsi historia, utamaduni na itikadi zinavyo saidia kupambanua mawanda na mipaka katika ulinganishi wa kazi za fasihi.

Kwanza ni historia, Historia inasaidia kulinganisha kazi za fasihi za mtunzi mmoja au wawili zilizoandikwa katika vipindi viwili tofauti na kuona mtagusano au mwachano wa kazi hizo kihistoria. Kwa mfano: Katika ulinganishi wa kazi za zamani za Kezilahabi na kazi za hivi karibuni kama kuna kufanana au kutofautiana kwa kazi hizo. Kipengele cha kihistoria humsaidia mwanafasihi linganishi kujua kazi ya kipindi fulani cha kihistoria na kazi nyingine ya kipindi kingine ili kutambua kama kazi hiyo hiyo imejirudia au inautofauti. Historia huweza kumsaidia mwanafasihi linganishi kuweza kupambanua yafuatayo,

 Kujirudia kwa Historia katika kazi za fasihi; Kwa mujibu wa Mlaga (2015), Kinacho onekana hapa ni dhana ya umviringo au uduara. Anaendelea kusema kuwa matukio ya kihistoria yana tabia ya kujirudia, kujirudia huko huhusisha wakati. Mlinganishi wa kazi za fasihi kwakutumia historia anaweza kubaini ujirudiaji wa kazi ya kifasihi katika vipindi tofauti vya kihistoria, Kwamfano tamthiliya ya Mfalme Edipode ya karne ya   5 BK  na Utenzi wa Nyakiru kibi ya karne 19.

 Mabadiliko ya kazi za kifasihi kihistoria.  Mlaga (keshatajwa) anasema mabadiliko huweza kutokea kwa namna mbalimbali kama vile kuhusu matukio ya zamani na athari za matukio husababisha kutokea kwa mabadiliko. Kutokana na historia mlinganishi huweza kubaini mabadiliko ya kazi mbalimbali kihistoria, hivyo kubaini tofauti ya kazi hizo. Kwa mfano tamthiliya ya Kinjekitile inayohusu vita vya majimaji  kabla ya uhuru na kazi za baada ya uhuru   kama vile Miradi bubu ya wazalendo. Kwakumakinikia historia mwanafasihi mlinganishi huweza kubaini mabadiliko katika kazi hizo.

Pili, Utamaduni; Ni jinsi binadamu anavyo kabili maisha katika mazingira yake, ambapo hujumuisha ujuzi, imani, Sanaa, maadili, sheria mila na desturi. Katika kipengele hiki mlinganishaji wa kazi ya fasihi humakinikia kuangalia vielelezo vya kitamaduni katika kazi hizo na kuvilinganisha ambapo huweza kubaini  na kupambabua mambo yafuatayo;

Kuingiliana kwa vipengele vya kitamaduni;  Katika kumakinikia Utamaduni mlinganishaji huweza kubaini kuingiliana kwa baadhi ya vipengele vya kitamaduni katika kazi mbili za kifasihi za jamii tofauti. Kwa mfano: Mlinganishaji anapolinganisha tamthiliya ya Lina Ubani na tamthiliya na Kwenye Ukingo wa Thim atakuta kuna kufanana kwa kipingele cha Utamaduni kuhusu swala la ndoa, ambapo kwao kuoa kabila kingine ni kosa.

Kutofautiana kwa baadhi ya vipengele vya kitamaduni; Mlinganishaji wa kazi ya fasihi anapo jikita katika kulinganisha kazi za kifasihi kitamaduni anaweza kubaini kutofautiana kwa vipengele vya kitamaduni baina ya jamii na jamii. Kwa mfano:  Wimbo wa Lawino kilicho tafsiriwa na Paul Sozigwa.

Kipengele kingine ni itikadi.  McClosky (1964) anaeleza kuwa itikadi ni mfumo wa imani ambao unaeleza, kujumuisha na kufafanua masuala ya madaraka, haki za binadamu na kutathimini masuala ya kihistoria ili kufanya maamuzi sahihi kwa wakati uliopo na ujao. Itikadi katika jamii ndiyo inaeleza namna viongozi, haki za binadamu, masuala ya dini namna vinavyomuongoza binadamu katika maisha. Itikadi inamsaidia mlinganishi wa kazi za fasihi kujua imani ya mwandishi mmoja katika kazi zake au kazi za waandishi wawili tofauti. Katika kumakinikia itikadi katika ulinganishaji wa kazi za kifasihi mwandishi huweza kubaini,

Kufanana kiitikadi baina ya kazi tofauti za mwandishi mmoja; Katika ulinganishaji wa kazi za kifasihi kwa kjtumia kipengele hiki cha itikadi  mlinganishi huweza kubaini ufanano wa itikadi katika kazi za msanii mmoja kwa mfano Chuachua (2011) ameeleza  kuhusu  itikadi katika riwaya za Shaaban Robert kama vile Kusadikika na Kufikirika ambazo itikadi ya umoja na ushirikiano imejitokeza.

Kutofautiana kwa itikadi baina ya kazi ya mwandishi mmoja na mwingine;  Katika kuangalia kipengele cha kiitikadi katika kazi za kifasihi ulinganishaji huweza kupambanua tofauti baina ya kazi hizo  kwa mfano kutofautiana kwa itikadi baina ya kazi za Emanuel Mbogo na kazi za Penina Mlama kuhusu itikadi zao juu ya mwanamke.

Kwa ujumla katika kulinganisha mawanda ya kazi za fasihi mlinganishaji ataangalia itikadi, historia na utamaduni. Huku akijikita katika nadharia mbalimbali za fasihi kama vile katika historia mlinganishi atatumia nadharia ya U-historia, katika Utamaduni anaweza kutumia Ufeministi na katika itikadi anaweza kutumia nadharia ya Ubaada ukoloni.



                                     


               
MAREJELEO
Chuachua, R. (2011), ItikadikatikaRiwayazaShaaban Robert. TATAKI: Dar es salaam.
McClosky, F (1964), Consensus and Ideology in American Political Science Review 58 (June)
361-82.
Mlaga, W. (2005), UhistoriakatikaRiwayaya Kiswahili: Mifanokutokariwayaza ‘Ndotoya
Ndaria’‘Gamba la Nyoka’ na ‘MiradiBubuyaWazalendo’. University of
 Rwanda: Rwanda.
Remark, H.H. (1971), ComperativeLiterature: its definition and Function. Southern illios:
                               Carbondale.
Wellek, R. na Warren, A. (1948), Theory of Literature. Harcourt, Brace and Company:
 New York.





                  


Post a Comment

0 Comments