Header Ads Widget

Responsive Advertisement

sifa pambanuzi za kifonetiki za sauti zote za Kiswahili. Sehemu ya tatu ni hitimisho la swali.






Hyman (1975) anafasili dhana ya Fonetiki kuwa ni taaluma ambayo huchunguza sauti ambazo hutumiwa na wanadamu wakati wanapowasiliana kwa kutumia lugha.

Pia Massamba na wenzake (2004) wanafasili Fonetiki ni tawi ambalo hujishughulisha na uchambuzi wa taratibu zote zinazohusiana na utoaji, utamkaji, usikikaji na ufasili wa sauti za lugha za binadamu kwa ujumla.

Vile vile Matinde (2012) anafasili kuwa neno “Fonetiki” limetokana na neno la Kigiriki “Phonetic” ambalo limeundwa na maneno mawili “Phone”  (sauti) na “tic” (uchunguzi). Hivyo, anafasili dhana ya Fonetiki kuwa ni taaluma ya isimu inayochunguza foni (sauti zote zinazotamkwa na binadamu ambazo hazihusishwi na lugha maalumu au mahususi).

Mgullu (1999:30) anafasili Sifa bainifu ni sifa ambazo hutumiwa kuzibainisha foni. Kila foni inaweza kupambanuliwa kwa kutumia sifa maalumu za foni fulani na jumla ya sifa hizo, ndizo ambazo huipambanua foni hiyo na pia huitofautisha na foni nyingine.

Pia Massamba na wenzake (2004:80) anafasili Sifa bainifu kuwa ni nduni zitumikazo kutofautisha kipashio kimoja na kipashio kingine cha aina yake.

Hivyo, Sifa bainifu ni nduni zitumikazo kubainisha foni moja kuwa au kutokuwa na sifa fulani tofauti na nyingine.

Katika lugha ya Kiswahili, sauti zimegawanyika katika makundi makuu mawili yaani sauti za konsonati na sauti za irabu. Mgullu (1999) anafasili Irabu ni sauti zinazotamkwa bila ya kuwa na kizuizi chochote katika mkondo hewa. Kwa mujibu wa Daniel Jones kama alivyonukuliwa na Mgullu (keshatajwa) anasema irabu msingi za Kiswahili ambazo hazihusishwi na lugha yoyote ni nane tu. Irabu hizo ni [a], [e], [i], [o], [u], [а], [ε], [Í»]. Vilevile kwa upande wa konsonanti, Mgullu (keshatajwa) anafasili kuwa ni sauti zinazotamkwa kwa kuwepo na kizuizi katika mkondo hewa. Katika lugha ya Kiswahili kuna jumla ya konsonanti ishirini na sita (G26) ambazo ni; [b], [d], [f], [g], ch [tʃ], dh [ð], gh [ɤ], [h], j [Ɉ], [k], kh [x], [l], [m], [n], ng’ [Å‹], ny [Ö€], [p], [r], [s], sh [ʃ], [t], th [Ó¨], [v], [w], y [j] na [z].

Zifuatazo ni sifa bainifu za kifonetiki za irabu za Kiswahili kama zilivyobainishwa na Mgullu (1999), ambapo amezingatia sifa kuu tatu yaani mahali pa kutamkia irabu, mwinuko wa ulimi na mkao wa mdomo.

Sifa ya mahali pa kutamkia irabu, kuna sehemu kuu tatu ambazo hutumika kutofautisha irabu. Sehemu hizo ni sehemu ya mbele ya ulimi, sehemu ya kati ya ulimi na sehemu ya nyuma ya ulimi. Sifa ya mwinuko wa ulimi, wanafonetiki wamegundua ya kuwa  mwinuko wa ulimi ni wa aina nne; mwinuko wa chini, mwinuko wa nusu – chini, mwinuko wa nusu – juu na mwinuko wa juu. Sifa ya mwisho ni mkao wa mdomo, ambapo wanafonetiki wameafikiana ya kuwa wakati wa kuzitamka irabu midomo huweza kukaa kwa namna kuu mbili yaani mkao wa mviringo na mkao wa mtandazo. Mathalani katika kielelezo kifuatacho kinadhihirisha sifa hizo;-























Hivyo, irabu msingi zinaweza kupambanuliwa kwa kutumia sifa bainifu tulizozijadili hapo juu kama ifuatavyo;-

     [i]                            [u]                                [e]                   [o]                     [a]

+ irabu                        + irabu                      + irabu                +irabu+ irabu

+ mbele                       + nyuma                   + mbele              + nyuma+ nyuma

+ juu   + juu                        + nusu juu          + nusu chini + chini

+ mtandazo                  + mviringo               + mtandazo          + mviringo    + mviringo



[ε]                         [Í»]                          [а]

+ irabu + irabu                     + irabu

+ mbele               + nyuma                   + mbele

+ nusu juu           + nusu chini             + chini

+ mtandazo          + mviringo                + mtandazo

Baada ya kubainisha sifa pambanuzi za irabu; zifuatazo ni sifa bainifu za kifonetiki za konsonanti zote za sauti za Kiswahili.

Ubainishaji wa sifa za konsonanti hutofautiana kutoka mtaalamu mmoja na mwingine. Mfano Jakobson na Halle miaka ya (1950), kama walivyonukuliwa na Mgullu (1999) walizipambanua konsonanti kwa kutumia sifa za kiakustika. Wao walikuwa na makundi matatu ya sifa ambayo ni sifa ya usonoranti, sifa ya uprotensi na sifa ya utoni. Baadaye Morris Halle alishirikiana na Noam Chomsky kuzipitia tena sifa za Jakobson na Halle na wakazigawa upya katika makundi makuu matano. Makundi hayo ni sifa za makundi makuu, sifa za chemba, namna ya kutamka, sifa chasili na sifa za kiarudhi. Lakini inaonekana kuwa sifa hizo zilizobainishwa na wanaisimu hao wakongwe, zilibuniwa ili kukidhi mahitaji ya kupambanua konsonanti zilizoonekana katika lugha ya Kihindi- Kizungu. Hivyo kama sifa fulani haisaidii kubainisha kitamkwa chochote katika lugha fulani, basi hiyo si sifa bainifu katika lugha hiyo na haina maana yoyote kuitumia.

Kwa mantiki hiyo, ingawa sifa bainifu tulizojadili hapo juu ni nyingi, lakini sifa zinazotakiwa kutumiwa wakati wa kuzibainisha konsonanti za lugha fulani mahususi, si lazima ziwe nyingi. Mathalani katika lugha ya Kiswahili, konsonanti zinaweza kubainishwa kwa kutumia sifa bainifu tano tu ambazo ni ukonsonanti, namna ya kutamka, mahali pa kutamkia, mkao wa glota na unazali. (Mgullu (1999).

Sifa ya ukonsonanti, konsonanti zote zinabainishwa kuwa na sifa hiyo yaani [+ konsonanti]

Sifa ya namna ya kutamka, inatusaidia kubainisha vitamkwa katika yale makundi makubwa kama vile; vipasuo (vizuiwa), vikwamizi, vizuiwa- kwamizi, vitambaza, vimadende, nazali na nusu- irabu (viyeyusho).

Vipasuo (vizuiwa), ni sauti ambazo zinapotamkwa hewa hutoka mapafuni, husukumwa nje na kuzuiwa kabisa kabla ya kuachiliwa kwa gafla na kutoa sauti ambayo hufanana na sauti za mlipuko. Vipasuo hivyo katika Kiswahili ni [p], [b], [t], [d], [k] na [g].

Vikwamizwa, ni sauti zinazotamkwa wakati ambapo, ala za kutamkia zinapokuwa zimekaribiana kiasi cha kutosha kuweza kusikika mkwaruzo unaotokea wakati hewa inapopita kati ya ala hizo. Vikwamizwa vilivyopo katika lugha ya Kiswahili ni [v],[f], [h], [z], [x], [s], [Ө], [ɤ], [ð] na [ʃ]

Vizuiwa- kwamizwi, ni konsonanti ambazo wakati wa kutamka hewa husukumwa nje kwa nguvu, huzuiwa halafu nafasi ndogo huachiwa ili hewa ipite ikiwa na mkwaruzo. Mfano konsonanti hizo ni [tʃ] na [Ɉ]

Vitambaza, ni konsonanti ambazo hutamkwa kwa hewa kusukumwa nje, kuzuiwa na kuruhusiwa kupita pembeni mwa kizuizibila kwaruzo mkubwa sana. Mfano wa kitambaza ni konsonanti [l].

Vimadende, hutamkwa huku ncha ya ulimi ikiwa imeugusa ufizi lakini kutokana na nguvu ya hewa inayopita katikati ya ncha hiyo na ufizi, ncha ya ulimi hupigapiga haraka haraka kwenye ufizi. Kwenye Kiswahili kuna kimadende kimoja ambacho ni [r].

Nazali, ni aina ya konsonanti ambazo hutamkwa kwa namna ya kukishusha chini kinywa kwa namna ambayo kiasi kikubwa cha hewa kutoka mapafuni huelekea kupitia kwenye chemba cha pua. Kiswahili kina nazali zipatazo nne ambazo ni [n], [m], [Å‹] na[Ö€].

Sifa ya mahali pa kutamkia, hutusaidia kuonyesha mahali ambapo kila sauti hutamkiwa. Mfano kuna sehemu mbalimbali za kutamkia kama vile; midomo, ufizi, kaakaa laini, kaakaa gumu, glota, chemba cha pua na meno.

Sifa ya glota, inatusaidia kutofautisha kati ya zile sauti ambazo ni ghuna na zile ambazo si ghuna. Mathalani foni [p] na [b] zinafanana kwa sifa zingine zote, isipokuwa hutofautiana katika sifa ya mkao wa glota. Foni [p] ni sighuna [-ghuna] lakini foni [b] ni ghuna [+ghuna].

Sifa ya mwisho ni Unazali, ambapo hutusaidia kubainisha zile foni ambazo zina sifa ya unazali [+unazali] na zile foni zingine ambazo hazina sifa ya unazali yaani [-unazali]

Ufuatao ni ufafanuzi unaobainisha sifa za kifonetiki za sauti za konsonanti za Kiswahili.

Vizuiwa/ vipasuo

[p]                        [b] [d]                  [t]                     [k]                [g]

+ kons                 + kons + kons             + kons             + kons          + kons

+ kipasuo            + kipasuo + kipasuo        + kipasuo        + kipasuo     + kipasuo

+ a mdomo         + a mdomo + ufizi              + ufizi            + kk laini       + kk laini

- unazali- unazali - unazali           - unazali       - unazali         - unazali

- ghuna+ ghuna + ghuna             - ghuna         - ghuna           + ghuna

Vikwamizwa

[f]                           [v]  [Ó¨]                         [ð]                        [s]

+ kons + kons  + kons                      + kons                + kons

+ kikwamizwa        +  kikwamizwa + kikwamizwa           + kikwamizwa     + kikwamizwa

+ a mdomomeno    + a mdomomeno+ meno                      + meno                + ufizi

- unazali - unazali    - unazali                   - unazali - unazali

- ghuna  + ghuna                      - ghuna                    + ghuna - ghuna

[z]                            [x] [ɤ] [ʃ]                              [h]

+ kons + kons                  + kons + kons                      + kons

+ kikwamizwa+ kikwamizwa+ kikwamizwa + kikwamizwa      + kinusa

+ ufizi+ kk laini              + kk laini+ kk –a ufizi           + glota

- nazali - unazali  - nazali                     - nazali- nazali

+ ghuna                    - ghuna+ ghuna                    - ghuna - ghuna





Vizuiwa kwamizwaKitambaza                       Kimadende

   [tʃ][Ɉ]                             [l]                                   [r]

+ kons+ kons                      + kons                         + kons

+ kizukwa         + kizukwa                + kitambaza                    + kimadende

+ kk gumu+ kk gumu             + ufizi                              + ufizi

- unazali- unazali   - unazali                            - unazali

- ghuna+ ghuna                + ghuna                         + ghuna

Nusu irabu

[w]                                       [j]

+ nusu irabu                    + nusu irabu

+ midomo/ kk laini            + kk gumu

- Unazali                         - unazali

+ ghuna  + ghuna

Nazali

[m]                       [n]                            [Ö€]                             [Å‹]

+ kons               + kons  + kons                     + kons

+ nazali             + nazali  + nazali                   + nazali

+ midomo          + ufizi                       + kk gumu+ kk laini

+ unazali + unazali  + unazali  + unazali

+ ghuna  + ghuna+ ghuna + ghuna

Kwa ujumla fonetiki imetoa mchango mkubwa sana katika kuzitambua sauti na sifa zake kwa ujumla katika lugha nyingine na katika lugha ya Kiswahili. Ambapo katika lugha ya Kiswahili imetusaidia kubainisha utofauti uliopo katika kuzipambanua sifa za konsonanti na irabu na katika vipashio vya aina yake.























MAREJELEO

Hyman, L. M. (1975). Phonology: Theory and Analysis. New York: Holt, Rinehart & Winston.

Massamba, D. P. B. na wenzake .(2004). Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu: Sekondari na Vyuo

(SAMIKISA). Dar es salaam: TUKI.

Matinde, R. S. (2012). Dafina ya Lugha Isimu na Nadharia: Kwa Sekondari, Vyuo vya Kati na

 Vyuo Vikuu. Tanzania- Mwanza: Serengeti Educational Publishers Ltd.

Mgullu, R. S. (1999). Mtalaa wa Isimu. Uganda – Kampala: Longhorn Publishers (U) Ltd.



















Post a Comment

0 Comments