Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Namna Nadharia za Semantiki zinavyowasaidia Watunga Kamusi katika Kutimiza Malengo yao

  

 na

Hashim

 Juma

 Ikisiri 

Watunga kamusi huwa na malengo mbalimbali. Baadhi ya malengo hayo ni haja ya kueleza na 

kufafanua dhana mpya, kumsaidia mtumiaji kamusi kuwa na uelewa zaidi, haja ya kutaka 

kumsaidia mtumiaji kuwa na idadi kubwa ya msamiati inayorejelea dhana moja, kumsaidia 

mtumiaji wa kamusi kufahamu historia za maana za maneno, haja ya kutaka kuonesha matumizi 

ya maneno, na haja ya kutaka kutoa maana za maneno. Hata hivyo, malengo hayo ili yaweze 

kutimizwa kwa kiwango kikubwa yanategemea matumizi ya nadharia za maana. Lengo la makala 

haya ni kujadili jinsi nadharia za maana zinavyokidhi malengo ya watunga kamusi. Pia, katika 

kujadili hili makala haya yatakuwa na mpangilio ufuatao; kipengele cha utangulizi ambacho 

kimehusisha nadharia mbalimbali za maana, kipengele cha namna nadharia za maana 

zinavyowasaidia watunga kamusi katika kutimiza malengo yao na mwisho ni hitimisho.

1.0Utangulizi

Katika kipengele hiki nimeelezea nadharia mbalimbali za maana kwa kuwaangalia, waasisi wake 

na misingi ya nadharia hizo. Miongoni mwa nadharia za maana ni:

1.2 Nadharia ya Dhana/Taswira

Nadharia hii hudai kuwa, maana ya kiyambo ni dhana au taswira inayoibuliwa na kiyambo hicho 

akilini mwa mwanalugha pindi kiyambo hicho kinapotumika (Palmer, 1976: Lyons, 1987: 

Akmajian na wenzie, 2010). Hii ina maana kwamba, maneno ni alama ya mawazo yaliyomo akilini 

mwa watumiaji wa lugha inayohusika. Kimsingi, nadharia hii ina misingi ya kisaikolojia kwa 

kuhusisha suala la dhana inayoibuliwa katika ubongo ama akilini mwa mwanalugha. mfano,

maana ya neno mtoto ni ile picha au taswira inayojengeka kuhusishwa na kiyambo hicho katika 

ubongo wa mwanalugha.

1.3 Nadharia ya Uelekezi

Nadharia hii iliasisiwa na wanafalsafa waliodai kuwa njia nzuri ya kufafanua maana ya kitu ni 

kuonyesha kwa kidole kile kinachorejelewa (Resani, 2014). Katika nadharia hii uelekezi hutumika 

kama mbinu ya msingi inayotumiwa kuwaonesha watu vitu halisi katika mazingira wanamoishi. 

1.4 Nadharia ya Matumizi

Hii ni nadharia yenye mkondo wa kimawazo ya wanafalsafa. Mwanafalsafa anayehusishwa moja 

kwa moja na nadharia hii ni Lodwig Wittgenstein (1953) katika kitabu cheke cha Philosophical 

Investigation (Reimer, 2010: Akmajian na wenzie, 2010, Kahigi, 2019). Wittgenstein anaeleza 

kuwa, ni kosa kubwa kuweka mipaka ya maana kama ambavyo nadharia za maana kama dhana, 

mwitiko na kitaja zinavyofanya, kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kuweka mipaka ya thamani 

ya umbo lenyewe la kiisimu na hivyo kinachopaswa kuzingatiwa ni matumizi yake. Hivyo, haja 

ya kuuliza hili neno lina maana gani bali angalia neno hilo linatumikaje. Tobing (2010) anaeleza 

kuwa, maana za maneno hazitakuwa na uvulivuli kama zitakitwa katika muktadha wa matumizi. 

Pia, Fodor (1980) anaeleza kuwa, nadharia hii haibagui umbo lolote la kiisimu lenye maana kwani 

kwenye Kiswahili kuna maneno kama vile ‘na’ ‘ya’ ‘wa’ ‘kwa’. Mfano neno na linapata maana 

kama litahusishwa na muktadha wa tungo mathalani, Baba na mama wanalima, neno na ambalo 

ni kiunganishi linapata maana kama, neno linalotumika kuunganisha maneno katika tungo. Hivyo, 

maneno kama hayo yanaweza kuelezwa vizuri kwa kutumia nadharia ya matumizi.

2.0 Jinsi Nadharia za Maana zinavyowasaidia Watunga Kamusi katika Kutimiza malengo 

yao

Kimsingi, watunga kamusi hutumia nadharia za semantiki kama sehemu ya kufanikisha malengo 

yao, makala haya yamezingatia malengo ya watunga kamusi hususani watunga kamusi ya lugha 

(wahidiya) na malengo hayo ni kama yafuatayo:

2.1Haja ya kutaka kuonesha matumizi ya Maneno mbalimbali

Watunga kamusi huwa la kusudio la kutaka kuonesha namna ambavyo neno fulani linavyoweza 

kutumika. Uoneshaji wa matumizi ya maneno katika kamusi humsaidia mtumiaji kufahamu 

mawanda ya neno husika kwani kila neno huwa na mipaka yake kimatumizi. Lengo hili huwa linatimizwa na watunga kamusi pindi wanapotumia nadharia ya matumizi ambayo msingi wake ni

‘maana ya neno ni matumizi yake katika lugha’. Tazama mifano ifuatayo kwa ufafanuzi zaidi. 

 Neno Maana

 i. Na neno linalotumika kuunganisha maneno katika 

 tungo: Baba~mama.

 ii. Mbuzi mnyama anayefanana na swala, anayefugwa kwa 

 ajili ya kutoa nyama au maziwa: Mama 

 amenunua mbuzi jike na dume

 

 Chanzo TUKI, 2014

Katika mfano wa (i-ii) hapo juu, kuna kategoria mbili za maneno ambazo ni tofauti, kuna 

kiunganishi na nomino. Mathalani neno na linapata maana kama litahusishwa katika muktadha wa 

tungo. Mfano: Baba~mama wanalima, matumizi ya na katika tungo (i) ni kuunganisha maneno 

yenye hadhi sawa katika tungo. Kadhalika, neno mbuzi limefasiliwa kama mnyama anayefanana 

na swala, anayefugwa kwa ajili ya kutoa nyama au maziwa. Maana ya mbuzi imetolewa kwenye 

kamusi kwa kuzingatia muktadha wa matumizi ya neno hilo. Lengo hili huwa linatimizwa na 

watunga kamusi kwa kutumia nadharia ya matumizi ambapo neno limepewa maana kutokana na 

jinsi linavyotumika.

2.2 Humsaidia Mtumiaji kuwa na idadi kubwa ya Msamiati inayorejelea dhana moja

Watunga kamusi wanapaswa kumsaidia mtumiaji wa kamusi kumuorodheshea msamiati 

mbalimbali inayorejelea dhana moja. Kimsingi, msamiati huo ni ule wenye mahusiano ya 

sinonimia mathalani pesa/hela/faranga. Mtumiaji anapokutana na maneno kwenye kamusi 

humsaidia kuwa na ukwasi wa msamiati na kumfanya aweze kuyatumia katika miktadha 

mbalimbali. Lengo hili huwa linatimizwa na watunga kamusi kwa kutumia nadharia ya matumizi 

ambapo mtumiaji atalazimika kutofautisha matumizi ya maneno hayo kulingana na muktadha. 

2.3 Haja ya kutaka kutoa maana za Meneno

Watunga kamusi hutoa maana za maneno ili ziweze kumsaidia mtumiaji wa kamusi. Maana za 

maneno ambazo zinapatikana kwenye kamusi hutokana na vyanzo mbalimbali vya data, mathalani 

kukusanya makongoo, kupitia kamusi tangulizi na kuwahoji watu (Mdee, 2006). Hivyo, katika 

vyanzo vya upatikanaji data, watu au jamii wana nafasi katika kutoa maana za maneno kwani 

watunga kamusi hulazimika kuwahoji watu au jamii ili waweze kupata maana za maneno. Lengo 

hili linaweza kutimizwa na watunga kamusi kupitia nadharia ya dhana/taswira ambapo wahojiwa 

wanakuwa na dhana fulani akilini mwao kuhusiana na maneno wanayoulizwa. Hivyo, maana ya 

maneno hayo watakayoulizwa yatatokana na dhana walizonazo katika akili zao. Tazama mifano 

ifuatayo kwa ufafanuzi zaidi.

Mfano (i), maana ya neno mpira itatokana na dhana ambayo ipo kichwani kwa mhojiwa, 

ambapo mhojiwa anaweza kusema kuwa mpira1

ni kitu cha mviringo kinachodunda na 

kinachotumiwa katika michezo mbalimbali. Mpira2

ni mti ambao hutoa utomvu mzito 

mweupe unaogandishwa na kutengenezwa vitu mbalimbali kama vile magurudumu. 

Chanzo (TUKI 2014).

Katika mfano (i) hapo juu, tunaona kuwa kuna maana mbili tofauti juu ya dhana mpira, ambapo 

maana hizo mbili zimetokana na dhana ambazo zimejengeka akilini mwa watumiaji lugha juu ya 

neno mpira. 

2.4 Haja ya kutaka Kuhifadhi historia za Maana za Maneno 

Watunga kamusi wanapaswa kuhifadhi maana za maneno ili watumiaji waweze kufahamu maana 

hizo. Mdee (2006) anaeleza kuwa, maana ya neno huweza kupangwa kufuatana na kigezo cha 

kihistoria. Maneno yenye uhusiano wa Kipolisemia maana zake hupangwa kwa kuzingatia kigezo 

cha kihistoria. Tazama mifano ufuatao kwa ufafanuzi zaidi.

1. mdomo

i.

-sehemu ya mwili wa binadamu inaopatikana kwenye kichwa 

ii.

-sehemu ya juu ya chupa iliyo wazi

2. mguu 

i.

-wa binadamu

ii.

-wa meza

Katika mfano (i-ii) hapo juu, maana za maneno zilizopangwa kwa kuzingatia kigezo cha kihistoria, 

ambapo maana ya kwanza ya maneno tajwa hapo juu, ndiyo maana ya msingi ambayo ilianza, 

kisha ndipo ikaja maana ya pili ambayo imekuja kutokana na mnyumbuliko wa maana ya kwanza. 

Hivyo maneno yenye uhusiano wa kipolisemia maana zake huwekwa kwa kufuata kigezo cha  maana kihistoria. Lengo hili linatimizwa na watunga kamusi pindi watumiapo nadharia ya 

matumizi ili neno kichwa na mguu liweze kueleweka lazima likitwe katika muktadha wa 

matumizi ili lipate maana. Mfano; mguu wa meza umevunjika. Kufanya hivyo tungo hiyo itakuwa 

haileti utata wa kimaana. 

2.5Lengo la kumsaidia mtumiaji kamusi kuwa na uelewa zaidi ya Maneno

Watunzi wa kamusi hawana budi ya kutafuta namna ambayo itamuwezesha mtumiaji wa kamusi 

aweze kuelewa zaidi maana za maneno. Kamusi zenye picha humsaidia mtumiaji kuelewa zaidi 

kutokana na matumizi ya picha kwenye kamusi. Baadhi ya maneno katika kamusi huitajika 

kupewa ufafanuzi kwa kutumia picha ili kumrahisishia msomaji aweze kuielewa zaidi juu ya dhana 

husika. Tazama mifano ifuatayo kwa ufafanuzi zaidi.

 Neno Maana

i. Mwewe Ndege mkubwa anayefanana na tai ambaye 

 hukamata vifaranga wa kuku.

ii. Mnandi Ndege mkubwa mwenye rangi nyeupe tumboni, 

 shingo ndefu na miguu mifupi kama ya bata na 

 hukaa baharini, mtoni au ziwani akiwinda samaki.

 Chanzo: TUKI, 2014

Katika mfano (i-ii) hapo juu, neno mwewe na mnandi yamepewa ufafanuzi wake kwa kuwekewa 

picha ili zimsaidie mtumiaji wa kamusi aweze kuelewa zaidi juu ya dhana mwewe na mnandi. 

Watunga kamusi hutimiza lengo hili kwa kutumia nadharia ya uelekezi ambayo ina muelekeza 

mtu kwa kutumia picha ili aelewe zaidi kuhusu neno fulani. 

2.5 Haja ya kueleza na kufafanua dhana mpya

Kimsingi, dhana mpya zinazoingiwa kwenye kamusi huitaji ufafanuzi wa kimaana. Chuwa (1995) 

anaeleza kuwa, dhana mpya katika kamusi huitaji kufafanuliwa zaidi kwani dhana hizo zinakuwa 

ngeni kwa watumiaji wengine hivyo watunga kamusi hulazimika kutolea ufafanuzi maneno hayo. 

Pia, Wamitila (2010) anaeleza kuwa, yapo maneno ambayo ni mapya kwa watumiaji wengine

ambayo huitaji kupewa ufafanuzi. Tazama mfano (i-ii) kwa ufafanuzi. 

Neno Maana

i.

Ng’aure Paka wa Kike

ii.

Mafurudhati Hali ya kuwa nana tabia ya 

 usahaulifu na kupuuza mambo ya 

 Kimsingi anayotakiwa kufanya mtu.

 Chanzo Wamitila (2010).

Katika mfano (i-ii) hapo juu, ni dhana mpya kwa watumiaji wengine na zimeingizwa kwenye 

kamusi na kupewa ufafanuzi. Hivyo, lengo la kueleza na kufafanua dhana mpya huwa linatimizwa 

na watunga kamusi kwa kutumia nadharia ya dhana/taswira ambayo hulitazama neno. 

3.0 Hitimisho

Makala haya yameangazia Nadharia za Maana, Malengo ya watunga kamusi, na Namna ambayo 

nadharia za semantiki zinavyowasaidia watunga kamusi katika kutimiza malengo yao. Kuhusu 

nadharia za semantiki ambazo zinakidhi malengo ya watunga kamusi nadharia ya dhana/taswira, 

nadharia ya uelekezi na nadharia ya matumizi. Kadhalika, makala haya yamebaini kuwa, nadharia 

ya matumizi inayotumika kwa kiwango kikubwa na watunga kamusi pindi wapoingiza maana za 

maneno kwenye kamusi. Pia, makala haya yamebaini kwamba, kuna uwezekano wa kuwa na neno 

moja kutumia nadharia mbili katika kupata maana, mathalani, neno; mbuzi, kata, ota. Kimsingi,

maneno hayo yanaweza kutumia nadharia ya matumizi na nadharia ya dhana/taswira katika kupata 

maana zake.


MAREJELEO

Chuwa, A.R. (1995). Dhima ya Kamusi katika Kubainisha Kamusi ya Vihisishi. Vol 4 no 2: 

 Taasisi ya Taalima za Kiswahili.

Fodor, J. D (1980). Semantics. Theories of Meaning in Generative Gramma. London Harvard 

 University Press.

Kahigi, K. K. (2019). Misingi ya Semantiki na Pragmatiki ya Kiswahili. Dar es Salaam: KAUTTU.

Mdee, J. S. (2006). Nadharia na Historia ya Leksikografia. Dar es Salaam: TUKI.

Palmer, R. M. (1976). Semantics. Volume 2. London: Cambridge University Press.

Reimer, N. (2010). Introducing Semantics, New York, Cambridge University Press.

Resani, M (2014). Semantiki na Pragmatiki ya Kiswahili. Dar es Salaam: Karljamer Print 

 Technology.

Tobing, S. S (2010). Semantics Change and Meaning shift analysis of Film Making terms, Tasnifu 

 ya Strata 1 Digrii ya Isimu Chuo Kikuu cha Diponegoro.

TUKI, (2014). Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Dar es Salaam: Oxford University Press.

Wamitila, K. W. (2010). Kamusi Pevu ya Kiswahili. Nairobi: Vide Muwa. 

Post a Comment

0 Comments