Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Afisa maendeleo ya jamii Majina ya WALIOITWA KWENYE USAILI afisa maendeleo ya jamii

 



SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Kumb. Na.JA.9/259/01/A/326

30/06/2023

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Wizara, Idara za 

Serikali, Wakala wa Serikali, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (MDA’s- & LGA’s)

anapenda kuwataarifu Waombaji Kazi wote walioomba kazi kwa nafasi ya Afisa Maendeleo 

ya Jamii II kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia tarehe 08-07-2023 hadi 18-07-2023

na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo.Wasailiwa

wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-

i. Usaili utafanyika kuanzia tarehe kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili muda na

sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kituo cha Usaili.

ii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa (Mask)

iii. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;

iv. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha

Mpiga kura,Kitambulisho cha kazi,Kitambulisho cha Uraia, Leseni ya Udereva, Hati ya 

kusafiria au barua kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji unakatoka.

v. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa,

kidato cha IV, VI, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana 

na sifa za Mwombaji.

vi. Wasailiwa watakaowasilisha Testimonials, Provisional Results, Statement of results,

hatiza matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA 

NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI.

vii. Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi.

viii. Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili.

ix. Kwa wasailiwa waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na

kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA)

x. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa

hawakukidhi vigezo. Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na 

kuzingatia mahitaji ya tangazo husika.

xi. Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao na

kunakili namba ya usaili kwa kuwa namba hizo hazitatolewa siku ya usaili

x. Vifaa vya kieletronic haviruhusiwi

Kupakua Majina Bofya >>HAPA>>

Post a Comment

0 Comments