Header Ads Widget

Responsive Advertisement

FASIHI LINGANISHI; MISINGI YA ULINGANISHAJI WA KAZI ZA KIFASIHI YA KISWAHILI NA FASIHI YA KISWAHILI





1.0  Utangulizi,

Katiika kazi hii tutaangalia  mi singi  ya  ulinganishaji katika kazi za fasihi ambapo kazi za kifasihi ya Kiswahili na fashihi ya Kimagharibi zitatumika  kama mifano. Majibu ya swali hili yamegawwa katika sehemu tatu. Sehemu ya kwanza ni utangulizi ambayo inahusu fasili ya fasihi linganishi, sehemu ya pili ni kiini cha swali na mwisho ni hitimisho.

Wellek na Warren (1948), wamefasili dhana ya fasihi linganishi kuwa ni mbinu itumiwayo na wahakiki wengi wakazi ya fasihi hata wasayansi kwakujadili njia maalumu ya usomaji wa sanaa mbalimbali ulimwenguni. Ulinganishi unaweza kuwa wa fasihi ya kiafrika na Kizungu ama fasili ya kizungu dhidi ya Kihindi. Ulinganishi unahusu ulinganishaji wa kazi za mataifa mbalimbali na sio za kitaifa peke yake. 

Vilevile Henry Remark (1971) anafasili fasihi linganishi kama uwanja wa kifasihi unao husika na uchanganuzi na mahusiano ya kifasihi, nje ya mipaka ya nchi moja na fani nyinginezo.

Kwaujumla, fasihi linganishi ni ulinganishi wa kazi za kifasihi baina ya mwandishi mwenyewe, mwandishi na na mwandishi mwingine, jamii na jamii au taifa na taifa.

2.0   Misingi ya ulinganishaji.

Hiininguzonamiongozoimwongozayomlinganishajikulinganishakazimbalimbali za kifasihi, na humwezesha mlinganishaji kushughulikia kipengele kimoja baada ya kingine wakati wa shughuli ya ulinganishaji. Katika kazi hii tutamakinikia misingi mitano kama ifuatavyo;

2.1 Dhamira

Katika kipengele hiki mwandishi hujikita katika kuangalia kuingiliana na kutofautiana kati ya dhamirazakazimbilitofautizakifasihi. Kwa kutumia msingi huu katika kulinganisha fasiihi za Kiswahili na Kimagharibi, dhamira mbalimbali zinafana ingawa kazi hizozinztoka katika  Mabara tofauti yenye wakaaji wanaotofautiana. Mfano  suala la umasikini linavyo jadiliwa katika  riwaya ya usiku utakapo kwisha, ambapo tunaona marafiki wawili Gonza na Chioko ambao walikuwa ni masikini na walisaidina vivyo hivyo katika  Hekaya za Pinokio  swala hili la umasikini limejitokeza na  mafundi wawili masikini ambaoni Cillegia na  Geppetto, walikuwa wakisaidiana. Vilevile masuala ya udanganyifu   yanayojitokeza katika Hadithi za Esopo ambapo  Beberu alidanganywa na Mbweha akatumbukia kisimani ,swala hili la udanganyifu linajitokeza pia katika  tamthiliya ya Ngoswe Penzi kitovu cha uzembe ambapo Mazoea alidanganywa.  Katika kutofautiana kwa kazi hizi kidhamira ni kuwa fasihi za kimagharibi hazizungumzii maswala ya uganga na uchawi.

2.2  Historia

Ni taaluma inayohusu matukio ya mbalimbali ya kipindi kilichopita na wakati ujao.Historia inasaidia kulinganisha kazi za fasihi za mtunzi mmoja au wawili zilizoandikwa katika vipindi viwili tofauti na kuona mtagusano au muachano wa kazi hizo kihistoria. Kwa mfano: Katika ulinganishi wa kazi za zamani za Kezilahabi na kazi za hivi karibuni kama kuna kufanana au kutofautiana kwa kazi hizo. Kipengele cha kihistoria humsaidia mwanafasihi linganishi kujua kazi ya kipindi fulani cha kihistoria na kazi nyingine ya kipindi kingine ili kutambua kama kazi hiyo hiyo imejirudia au inautofauti. Mfano Tamthiliya ya Mfalme Edipode ya karne ya 5 na Utenzi wa Nyakiiru ya karne ya 19 kuna matukio ya kihistoria yamejirudia, kujirudia huko huhusisha wakati. Mlinganishi wa kazi za fasihi kwakutumia historia anaweza kubaini ujirudiaji wa kazi ya kifasihi katika vipindi tofauti vya kihistoria.

2.3 Itikadi,

katikakulinganishakaziza kifasihi, suala la itikadi huweza kufanana au kutofautiana kutoka kwa mwandishi mmoja hadi mwingine, mathalani katika kufanana kiitikadi kwa kazi za kifasihi na kimagharibi kuna itakadi za kimapinduzi ambapo wanaamini kwamba tabia njema ndio husababisha ujenzi wa jamii mpya. Mfano Shaban Robert huwatakawatuwawenamaadilihivyohivyoukimuangaliamwandishiwaHekayazaPinikioanawaonyawatoto dhidi ya tabia ya kusema uongo kwa kumtumia mhusika Pinoko ambaye pua yake alikuwa ndefu kila anapodanganya.

2.4 Utamaduni

Utamaduni ni jumla ya mtu au jamii inavyoishi na kujiwekea miongozo itakayo iongoza jamii hiyo,  mwanajamii analo jukumu la kuifuata misingi hiyo. Katika  ulinganishaji wa kazi za kifasihi ya Kiswahili na Kimagharibi, msingi huu humwongoza mlinganishaji katika kunga’amua ikiwa kazi  hizi kutokakatikajamiitofautizinafananakitamaduniama laa, Aidha katika ulinganishaji wa kazi hizi tunaona  kuingiliana kwa vipengele vya kiutamaduni wa jamii moja na jamii nyingine, mathalani katika jamii za Waswahili suala la kuoana kwa watu wenye nasaba moja ni kosa ambapo suala hili linaonekana pia kufanana na jamii ya watu wa magharibi hususani Ugiriki ambao nao ni kosa kuoana kwa watu wa nasaba moja. Mfano katika tamthiliya ya Mfalme Edipodena Tamthiliya ya kwenye Ukingo wa Thim. Vilevileutamaduniwakuchezangomakatika vikundi unaojitokeza muongonimwakazinyingizakiswahilikamaNgomayaMwanamalundi,katikafasihizaKimagharibini tofauti kwani wao hucheza muziki katika shoo na maonesho mbalimbali kama ijitokezavyokatikahadithizaEsopokatikakisacha Nyaninawacheza shoo.



2.5 Falsafa ;

Sodipo (1973) anafasili falsafa nimawazo, fikra na udadisi kuhusudhana na kanuni zinazotusaidiakuongeza uzoefu kuhusu maadili dini, siasa ,sheria , saikolojia,historianasayansiyajamii. Katika  ulinganishaji wa kazi za Kiswahili na zile za Kimagharibi kuna kuhitilafiana na kutaguzana katika kipengele hiki ambapo katika kufanana kifalsafa baina ya waandishi wa kazi hizo suala la falsaya ya Euprase Kezilahabi ya “ kifo sio mwisho wa kuwako” inajitokeza pia katika kazi ya hekaya za Pinokio ya  Mtaliano  Carlo Collodi. Aidha katika kutofautiana kifalsafa  baina ya kazi za Kiswahili na kimagharibi ni katika falsafa ya wema kuushinda ubaya inayopatikana katika kazi za Kiswahili zilizoandikwa na Shaaban Robert na falsafa ya Ubaya kwa ubaya inayopatikana katika kazi ya Wagiriki Pinkey na Aesopus  walioandika hadithi za Esopo katika kisa cha Nyoka na Nyigu.



3.0  Hitimisho

KwaUjumlakwabaadhi ya vipengele kazi za kifasihi za Kiswahili na zile za kimagharibi zinafanana  nakuitofautiana kwa uchache katiika baadhi ya vipengele.  





















MAREJELEO

Aesopus (1698). "Fabularum Aesopicarum Delectus". google.co.uk.



Collodi C, (1883) Le adventure di Pinocchio, Firenze. Italy

Sodipo (1973), Woman and African Society. France: Strasbourg

Remark, H. H. (1971), Comparative Literature: Its Definition and Function. Southern Ilions

Carbondale.

Wellek,   R . na Warren, A.  (1948), Theory of Literature. Horcourt, Brace and Company: New

York.



                                                      


Post a Comment

0 Comments