1.0 UTANGULIZI
Katika kazi hii tutajikita katika uchunguzi wa
vipengele vya Kisayansi na Kisanaa katika utunzi wa kamusi. Ili kufikia lengo
la kazi hii,
sehemu kuu tatu zimezingatiwa ambazo ni fasili za dhana za msingi, kiini na
hitimisho.
1.1 FASILI ZA DHANA ZA MSINGI
Wiegand (1984) akinukuliwa na Mdee ( 2010), utunzi wa
kamusi ni sayansi ya kutunga kamusi. Anaendelea kusema kuwa, utungaji wa kamusi
hujumuisha uorodheshaji wa msamiati wa lugha inayotungiwa kamusi pamoja na
maelezo yenye kufafanua kila neno lililoorodheshwa kadri ya mahitaji ya mtumiaji aliyelengwa. Fasili hii
ikichunguzwa kwa makini inabainika kuwa, mtaalamu huyu amezingatia usayansi na
kupuuza vipengele vya sanaa ambavyo ama kwa hakika hutumika kukamilisha kamusi.
TUKI (2014) Sanaa ni ufundi wa kuwasilisha hisia na
mawazo ya binadamu katika maandishi, michoro, maigizo, nyimbo au uchongaji ni
zao linalotokana na ufundi
huo. Kwa ujumla Sanaa ni ubunifu alionao mtu katika kufanya au kutekeleza jambo
fulani.
TUKI (2014) Sayansi ni elimu inayotokana na uchunguzi,
majaribio, vipimo na kuthibitisha kwa muda uliopo. Hii ni kueleza kuwa sayansi
ni maarifa yanayotokana na uvumbuzi, tafiti, uchunguzi na uchambuzi wa jambo
fulani.
2.0 USAYANSI NA
USANAA WA KAMUSI
Ni kweli kwamba
kazi za utunzi wa kamusi ni ya kisayansi na kisanaa, ambapo
michakato hiyo ndiyo hukamilisha nyenzo hii muhimu ya lugha. Kwakuanza kuuabiri
usayansi ulipo katika kamusi ambapo hutokana na uzingativu wa kanuni na hatua
mbalimbali katika kukamilisha utengenezaji wa kamusi.
2.1.
USAYANSI WA KAMUSI
Kwa kuegemea
mawazo ya Mdee (2010, huu ndio usayansi uliopo katika utengenezaj wa kamusi.
2.1.1 Upangaji wa mradi wa kamusi,
Hii
ni hatua ya mwanzo ambapo mtunga kamusi, hupangilia michakato mizima ya utoaji
wa kamusi. Katika hatua hii mtunga kamusi huzingatia maamuzi ya aina ya kamusi
itakayotungwa, ukubwa wa kamusi hiyo, idadi ya wataalamu watakao husika katika
mradi ( wataalamu hawa huteuliwa kulingana na mahitaji ya kamusi), pamoja na
kupanga bajeti nzima ya mradi. Usayansi katika hatua hii hutokana na kumhitaji
mtunga kamusi kufanya tafiti pamoja na kupitia kamusi zilizo Keisha
kuchapishwa, na utumiaji wa elimu ya
hisabati katika kupangilia bajeti nzima ya mradi.
2.1.2 Uandikaji wa kamusi,
Katika
hatua hii huhusisha michakato mitatu ya kisayansi ambayo ni,
2.1.2.1 Ukusanyaji wa data.
Katika kipengele hiki humhitaji mtunga kamusi
kukusanya data kulingana na aina ya kamusi anayotaka kutengeneza kama vile
ukusanyaji wa leksimu kutoka katika jamii, au kutoka katika matini mbalimbali
zinazo husiana na ugha ambao mtunga kamusi ameamua kutungia kamusi yake.
Kwamfano kama mtunga kamusi anataka kutunga kamusi ya kichagga-kiswahili hana
budi kwenya kukusanya data kutoka katika jamii ya wachagga au matini mbalimbali
zilihusuzo jamii hiyo.
2.1.2.2 Uchambuzi wa data au
leksimu.
Kwa mujibu wa Mdee (2010), wataalam hutumia
taaluma yao katika kufanyia tafiti
leksimu zilizo kusanywa na kuteua zile zilizokidhi vigezo vya aina ya kamusi
inayoandikwa.
2.1.2.3 Uteuzi wa data,
Baada
ya uchambuzi wa kisayansi wa data zilizo kusanywa watunga kamusi huamua ni data
(leksimu) zipi zitumiwe kutokana na kukidhi haja ya mtunga kamusi, hii
nikutokana kuwa zipo leksimu nyingi sana katika lugha na mtunga kamusi huchukua
jukumu lakuteua leksimu zile tuu zilizo kidhi vigezo kutokana na aina ya kamusi
aliyokusudia, malengo ya kamusi, na walengwa wa kamusi. Baada ya uchambuzi
zileleksimu zilizo kidhi vigezo huingizwa katika kamusi kama taarifa kwa kuanza
na kidahizo, tahajia, matamshi, etimolojia, mofolojia, maana na mwisho mifano
na matumizi ya leksimu.
2.1.3 Uchapaji wa kamusi,
Hii
ni hatua ya kuchapisha kamusi ambapo kwa kawaida hutumia hadi asilimia 10 ya
muda wa utayarishaji wa kamusi kukamilika. Katika hatua hii kamusi hutolewa
katika maandishi makubwa ili kubaini makosa na kuingizwa katika nakala tepe na
baada ya urekebishaji hutolewa kama kazi kamili. Katika michakato hii huhusisha
vifaa vya kiteknolojia kama vile tarakilishi na machine za uchapaji.
2.1.4
Uhariri na upitiaji wa kamusi,
Hii ni hatua nyingine inayo dhihirisha usayansi katika
utengenezaji wa kamusi ambapo hii ndio hatu ya mwisho katika mchakato wa
utengenezaji wa kamusi, na umuhitaji mtunga kamusi kuipiti kamusi yake, na
kuihariri ili kubaini makosa na mapungufu mbalimbali yanayo jidhihirisha katika
kamusi hiyo.
2.2
USANAA WA KAMUSI
Baada ya kuangalia vipengele hivyo vya kisayansi sasa
tutalii usanaa uliopo katika kazi ya utungaji wa kamusi.
2.2.1 Matumizi ya vielelezo,
picha na
michoro. Katika utungaji wa kamusi mtunga kamusi hulazimika kubuni picha,
michoro na vielelezo ili kurahisisha uelewekaji wa vidahizo. Mtunga kamusi
hutumia ufundi wake kubuni picha na vielelezo hivi na kuhakikisha vitaashriria
dhana aliyo kusudia kwa msomaji wa kamusi. Mfano TUKI(2014) mtungaji katumia michoro katika kufafanua dhana
mbalimbali kuanzia ukurasa wa kwanza hadi mwisho wa kamusi.
2.2.2 Mpangilio wa vidahizo katika kamusi;
Kwa
mujibu wa Mdee (2010) maneno
yanayoorodheshwa katika kamusi huweza kupangwa kwa
kuzingatia mpangilio wa alfabeti au mpangilio wa leksimu ambapo katika mpangilio
huo huelezea maneno
yenye kuanza na herufi ya alfabeti ya aina moja ambazo hupangwa pamoja. Kwa
mfano katika kamusi ya Kiswahili
sanifu (imeshatajwa)
imepangilia vidahizo kialfabeti.
Katika mpango wa leksimu huelezea maneno yenye
uhusiano wa kimaana. Mpango huu wa kuorodhesha maneno kwa kufuata utaratibu wa
maana ulitumiwa na Peter Marck Robert 1852 alipotunga Thesaurusi. Hivyo mchakato huu unaonesha usanaa kwakuwa watunzi
wa kamusi ndio wenye jukumu lakuamua namna ya kupangilia maneno katika kamusi
yake.
2.2.3
Umbo la kamusi;
Katika utungaji wa kamusi mtunga kamusi huamua umbo la
kamusi yake kulingana na vidahizo alivyo amua kuviingiza katika kamusi yake.
Ikiwa mtunga kamusi atateua vidahizo vingi basi kamusi hiyo huwa kubwa sana na
ikiwa ataingiza vidahizo vichache bass kamusi hiyo huwa ndogo au ya wastani
mfano wa kamusi ya wastani/ndogo ni kamusi
ya Biolojia, Fizikia, na Kemia (2004). Hivyo umbo la kamusi hutokana na
mapenzi na ufundi wa mtunga kamusi.
2.2.4
Matumizi ya rangi katika kamusi.
Mtungaji wa
kamusi huweza kuamua kutumia rangi mbalimbali katika kamusi yake, kama vile
kutumia rangi katika kuandika vidahizo katika kamusi au kutumia mkolezo katika
kuonesha dhana za msingi katika kamusi yake. Mtunga kamusi hutumia sanaa hii ya
rangi kwa lengo lakuifanya kamusi yake kuwa na mvuto au kuainisha dhana za
msingi. Mfano katika kamusi ya Kiswahili- Kingereza(2014),
ametumia rangi ya bluu katika kuandika vidahizo.
2.2.5 Matumizi ya vifupisho katika kamusi;
Utungaji wa kamusi hutumia vifupisho katika
baadhi ya maneno. Kwa mfano: TUKI
(2004) kunavifupisho vya
aina kuu mbili katika kamusi, vifupisho vya kawaida , yani vile vilivyo vya
jumla na vifupisho mahususi, vifupisho vya jumla nikama adj, (adjective) n,
Nomino, K.m kwamfano . Matumizi haya ya vifupisho huamuliwa kutumiwa na mtunga
kamusi katika kuwakilisha dhana mbalimbali katika kamusi
Mfano katika
kamusi TUKI (201:99) imetumia vifupisho kama ifuatavyo ,
elewek.a kt be well known, bee understood...
Pia, elem.a kt <ele> 1 be a burden to. Hata
hivyo wakati wa kutumia sanaa hii ya vifupisho nilazima mtunga kamusi atoe
ufafanuzi wa vifupisho alivyo vitumia katika kamusi yake.
3.0 HITIMISHO
Kwaujumla,
Katika utungaji wa kamusi matumizi ya vipengele vya kisayansi na kisanaa
kwa pamoja ndivyo huweza kuikamilisha kamusi na kuifanya kamusi kuwa bora na
yenye mvuto.
MAREJELEO
Mdaee
J.S(2010), Nadharia na Historia ya
Leksikografia, TUKI: Dar es salaam.
TUKI (2004) Kamusi
Sanifu ya Biolojia, Fizikia, na Kemia. Taasisi ya Uchunguzi wa
Kiswahili: Chuo Kikuu cha Dar es
salaam.
TUKI (2014), Kamusi
ya Kiswahili-Kingereza, Taasisi ya Taaluma za Kiswahili: Chuo Kikuu cha Dar
es salaam.
TUKI(2014), Kamusi
ya kiswahili Sanifu.Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dar
es salaam.

0 Comments