Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Kwanini Profesa Aldin Mutembei anafaa kuwa ndiye nguli zaidi wa fasihi ya kiswahili kwa sasa

Prof, Aldin .k. Mutembei
Picha na mtandao.

Profesa Aldin .K. Mutembei alipata shahada ya Udaktari kutoka chuo kikuu cha Leiden  na baadaye mwaka 2015 kutunukiwa uprofesa katika chuo kikuu cha Dar es salaam: mkufunzi huyu wa fasihi na lugha Amewahi kuwa mkurugenzi wa taasisi ya taaluma za kiswahili, na sasa ni mkuu wa kigoda cha Mwalimu nyerere na mkurugenzi katika taasisi ya lugha na utamaduni ya conficuous.

Pamoja na kuandika na kushughulikia mambo mbali mbali ya kifasihi, Kuanzisha nadharia mpya ya uchambuzi wa fasihi iitwayo "Korasi katika fasihi ndiyo iliyompaisha zaidi, kwani imekuwa miongoni mwa nadharia mpya inayotumika kuhakiki kazi za kifasihi na yeye akitambulika duniani kama muasisi wa nadharia hiyo.
MAELEZO KUHUSU MKABALA WAKE


Mkabala Wa Ki-Korasi Katika Kuchambua Kazi Za Fasihi Ya KISWAHILI

"Kwa wachambuzi na wahakiki wa fasihi ya Kiswahili, mtazamo umekuwa ni wa kugawa makundi mawili: fani na maudhui. Hata hivyo, karibu wote wanakubaliana kuwa mgawanyo huu ni wa kinadharia zaidi na unafanyika kwa ajili ya uchambuzi na uhakiki;  kwani katika hali halisi maudhui huwezi kuyatenga kutoka katika fani (Senkoro 1982). Ingawa hivi ndivyo inavyojulikana, hakuna aliyeweza kupendekeza njia ya uchambuzi itakayoziweka pamoja dhana za maudhui na fani. Kwangu mimi, tatizo liko katika umapokeo, na kwa hiyo wachambuzi na wahakiki ambao bado wanashikilia dhana za fani na maudhui kwamba ndizo pekee zitumikazo katika uchambuzi wa fasihi wamegubikwa na mazoea ya kimapokeo ambayo mara nyingi hugomea mabadiliko. Dhana za fani na maudhui zimesimama kama sheria-mama katika uchambuzi na uhakiki wa fasihi. Kutokana na mtazamo huu wa ki-fani na ki-maudhui , wahakiki na wachambuzi wa fasihi kama vile tamthilia wameweka vigezo ambavyo havina budi vifuatwe iwapo mtu atataka kuichambua na kuihakiki kazi ya fasihi. Vigezo hivi sasa vimechukuliwa kama ni sheria katika uchambuzi na uhakiki wa tamthilia. Hata kuna waliothubutu kuweka "sheria" katika ubunifu wa kazi za fasihi Lakini uchambuzi, na hata uhakiki, kama ulivyo utunzi wa kifasihi, ni vigumu kuubana kwa sheria kama hizo. Suala la sheria katika usanii linaelekea kuwa jadi ya wanamapokeo (Abedi 1954; Mayoka 1984). Jambo hili limepingwa vikali katika usanii wa ushairi wa Kiswahili (Kezilahabi 1974; Mulokozi na Kahigi 1979). Likapingwa na E. Hussein kuhusu tamthilia aliposema: "Kuandika mchezo wa kuigiza ni kuumba sanaa. Na sanaa hukataa maelezo; kamwe haitaki sheria" (Hussein 1983: 195). Katika makala haya linapingwa katika uchambuzi wa fasihi ya Kiswahili. Nasisitiza kuwa fani na maudhui zisichukuliwe kuwa ndio dhana pekee zinapopaswa kuangaliwa wakati wa kuchambua fasihi. Dhana ya korasi ikieleweka vizuri, itaonekana kuwa ni kipengele kinachopaswa kuangaliwa kwa upekee wake na kikatumika katika uchambuzi wa kazi ya fasihi"
Licha ya kushughulikia kipengele hicho muhimu cha uhakiki, prof Mutembei mpaka sasa ameshughulikia maswala mengine ya fasihi ya kiswahili kama vile fasihi ya kiswahili na Ukimwi, fasihi ya kiswahili na teknolojia, fasihi linganishi na masuala mengine ikiwemo uandishi wa ushairi.
Pamoja na hayo Profesa Mutembei amekuwa akiipigia debe fasihi ya kiswahili na lugha ya kiswahili. Mwaka 2014, kituo cha habari za kiswahili katika mtandao wake wa kijamii kilimtaja kama Wole Soyinka wa Afrika mashariki. Aidha amekuwa mstari wa mbele katika mijadala inayohusu lugha ya kiswahili na fasihi ya kiswahili kiujumla.
Unaharakati wake kwa lugha ya kiswahili
Mutembei ni mmoja kati ya wataalamu wanaoamini itakuwa siku moja lugha ya kiswahili kuwa lugha ya bara zima la Afrika huku akishauri lugha zote za kiafrika kuchangia kukijenga kiswahili, Mara kadhaa amekuwa akilikazia hilo katika mjadala wa kiswahili kinawenyewe na Mohammed Khelef katika Dw.
Aldin Mutembei, picha na mtandao
Unaweza kusikiliza moja ya mijadala aliyoshiriki katika kituo cha Dw kiswahili kuhusu kiswahili kuwa lugha ya afrika katika kiswahili kina yenyewe. Hapa
Je Kwa hayo yote anastahili kuwa ndiye nguli wa fasihi ya kiswahili kwa miaka hii? Angalizo, katika kujibu swali hili lazima uzingatie kuwa mtaalamu huyu hajajikita sana katika kuandaa kazi za kifasihi Bali kuchambua, kueleza namna ya kuzichambua, kuziainisha, na kuzilinganisha kwa ajili ya msomaji.
Miongoni mwa machapisho yake pamoja na yale aliyoshiriki.
Social, cultural and sexual behavioral determinants of observed decline in HIV infection trends: lessons from the Kagera Region, Tanzania
J Lugalla, M Emmelin, A Mutembei, M Sima, G Kwesigabo, J Killewo, ...
Social science & medicine 59 (1), 185-198, 2004

The social and cultural contexts of HIV/AIDS transmission in the Kagera Region, Tanzania
JLP Lugalla, AIM Sandstrom, G Kwesigabo, CJ Comoro, JZJ Killewo, ...
Journal of Asian and African studies 34 (4), 377-402, 1999

HIV-1 infection prevalence and incidence trends in areas of contrasting levels of infection in the Kagera region, Tanzania, 1987-2000
G Kwesigabo, J Killewo, W Urassa, J Lugalla, M Emmelin, A Mutembei, ...
JAIDS Journal of Acquired Immune Deficiency Syndromes 40 (5), 585-591, 2005

Poetry and AIDS in Tanzania: changing metaphors and metonymies in Haya oral traditions
AK Mutembei
Research School of Asian, African and Amerindian Studies, Leiden University, 2001

Communicating about AIDS-Changes in Understanding and Coping with Help of Language in Urban Kagera, Tanzania1
AK Mutembei, MAC Emmelin, JLP Lugalla, LG Dahlgren
Journal of Asian and African Studies 37 (1), 1-16, 2002

The Availability and Acceptability of Intervention Strategies against AIDS/HIV Infection in the Kagera Region of Tanzania
JLP Lugalla, CJ Comoro, AK Mutembei

Ukimwi katika fasihi ya kiswahili: 1982-2006
AK Mutembei
Taasisi ya Taaluma za Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, 2009

African Languages as a Gateway to Sustainable Development, Democracy and Freedom: The Example of Swahili
AK Mutembei
ALTERNATION Interdisciplinary Journal for the Study of the Arts and …, 2014

KORASI katika Fasihi: Nadharia Mpya ya Uhakiki
AK Mutembei
TUKI, Dar es Salaam, 2012

UKIMWISHAJI wa Utanzu wa Fashihi: Mifano kutoka Methali za Tanzania
AK Mutembei
Kiswahili 70 (1), 2007

HIV/AIDS in Kiswahili and English Literary Works.
AK Mutembei
Matatu: Journal for African Culture & Society 46, 2015

AIDS Communication through Billboards and Murals in Tanzania
AK Mutembei
Asian Journal of African Studies, 75-94, 2014

Kukitandawazisha kiswahili kupitia simu za kiganjani: Tafakari kuhusu isimujamii
A Mutembei
Swahili Forum 18 (1), 198-210, 2011

Kiswahili Silaha Ya Afrika: Wanasiasa na Watawala
A Mutembei
Kiswahili 74 (1), 2011

Nadharia ya Fasihi Simulizi na Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia
AK Mutembei
Fasihi ya Kitaifa na Fasihi ya Kiswahili ni Dhana ileile?
AK Mutembei
Mulika Journal 26 (1), 2018
Nadharia ya fasihi simulizi na maendeleo katika sayansi na teknolojia
AK Mutembei
Mulika Journal 27 (1), 2018
Dhana ya Maadili katika Uandishi wa Shaaban Robert na Nafasi yake katika Muktadha wa sasa nchini Tanzania
AK Mutembei
FASIHI, LUGHA NA UTAMADUNI WA KISWAHILI NA KIAFRIKA.ISBN 978 9976 5316 1 9 …, 2018
Korasi na Uhusiano wake na Sanaa za Maonyesho: Uchambuzi wa Kidayakronia
AK Mutembei
Kioo cha Lugha 1 (1, 2), 2017
Dhima ya Lugha ya Mawasiliano katika Jamii: Kiswahili na Mkakati wa Usomaji kuelekea Umajumui wa Kiafrika
AK Mutembei
Kioo cha Lugha 14 (1), 2017
USAWIRI WA MAAMBUKIZI YA VVU KATIKA KISIKI KIKAVU
AK Mutembei
Kiswahili 75 (1), 2017
The Future of East African Orature in the Digital Age: Kiswahili Narratives in the Social Media
AK Mutembei
Studies in African Languages and Culture 51, 33-52, 2017
The Future of East African Kiswahili orature in the digital age: a case study of WhatsApp Narrative
AK Mutembei
Studies of the Department of African Languages and Cultures, 33-52, 2017
Slavery and Its Space in Kiswahili Literature
AK Mutembei
Asian Journal of African Studies, 3-31, 2016
Utandawazi wa Lugha za Kiafrika: Nafasi ya Kiswahili Sanifu katika Afrika inayobadilika
AK Mutembei
NADHARIA ZA TAFSIRI, UKALIMANI NA UUNDAJI WA ISTILAHI. ISBN 978 9976 9935 1 …, 2016
Epistolary role in East African Literary works on HIV/AIDS
AK Mutembei
Journal of the University of Namibia Language Centre 1 (1), 100-115, 2016
Language Dynamics in the Congo and the Strength of Kiswahili as a Unifying Force
AK Mutembei
Asian Journal of African Studies, 67-93, 2013
Swahili AIDS Plays
AK Mutembei
The Culture of AIDS in Africa: Hope and Healing Through Music and the Arts, 256, 2011
Mkabala Wa Ki-Korasi Katika Kuchambua Kazi Za Fasihi Ya Kiswahili: Mifano Kutoka Katika Tamthiliya
AK Mutembei
Kiswahili 73 (1), 2010
Decline in Prevalence and Incidence of HIV infection in Kagera: Analysis of Socio-Demographic and Behavioral Factors
G Kwesigabo, W Urassa, JZJ Killewo, JLP Lugalla, M Emmelin, ...
Social Change and Health in Tanzania, 148, 2005
Phonological aspects of foregrounding in Kiswahili poetry
AK Mutembei
University of Dar es Salaam, 1993
In honour of Professor Emmanuel Ngara and other African literary stylisticians.
L Acquah, A Adeniji, G Adeoti, P Adesanmi, S Adeyemi, JBA Afful, ...

Usisahau kuacha maoni yako hapa.


Post a Comment

0 Comments