Header Ads Widget

Responsive Advertisement

maana ya utafiti na aina za utafiti

 

 MAANA YA UTAFITI NA AINA KUU ZA UTAFITI

Utafiti ni nini?

Utafiti ni njia ya kupatautatuzi wa swala fulani katika jamii na mazingira ya binadamu kwa njia ya uchunguzi unaotumia nadharia za kitaaluma. Waaidha utafiti ni  njia maalum inayofuatwa ili kufikia ujuzi au taarifa muhimu inayokusudia kuchangia katika usomi wa kina na uchunguzi wenye mweleko wa kimaantiki.

Utafiti wowote ule hauwezi kufanyika wala haukamiliki pasi kuongozwa na nadharia kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Migao ya tafiti

Utafiti hugawika katika matapo mbalimbali kwa kutegemea madhumuni na maksudi ya utafiti.

Uainishaji huu ni kama ufuatavyo:-

§  Uainishaji wa Tafiti Kimakusudi

§  Uainishaji kwa kutumia mbinu za uchanganuzi

§  Uainishaji Kulingana na Aina za Utafiti.

 

 

 

 

1.      Utafiti wa kimaksudi

a.      Utafiti wa Kimsingi (Basic Research)

Hii ni aina ya utafiti ambao hutumiwa kujaliza ufahamu ambao jamii au mtafiti hana kuhusu swala fulani katika jamii.Utafiti huu hutumiwa katika kujaribu kujifunza mambo au vitu ambavyo kwa kawaida havikai kuwa wazi au havionyeshi umuhimu wake mara moja.

 

Utafiti huu huelekezwa na ari kisha ukachochewa na hamu ya kuongeza ujuzi na huusisha upataji wa ufahamu kuhusu jambo fulani. Lengo lake kuu ni kujibu maswali ya kwa nini? Nini? Na vipi? Kakika hali hiyo utafiti huu huongeza hali ya mtafiti na yeyote kufahamu maswala nyeti na muhimu. Aghalabu utafiti huu huwa hauna lengo la papo kwa hapo.

 

Utafiti kama huu  huangazia katika uzalishaji wa ujuzi wa kisayansi na kuukuza ujuzi huo kutoka sehemu pana ili kutoa masuluhisho katika sehemu zinazilingana sehemu hizo. Ifahamike kuwa utafiti huu  hujulisha na kuongeza ujuzi katika nyanda za elimu au usomi.\ Vile vile aina hii ya utafiti huzalisha ujuzi mpya ambao ujuzi huu hutumiwa katika uboreshaji na upanuzi wa nadharia zilizotangulia.Ifahamike kuwa utafiti aina hii ndio  unaofanywa na wasomi ili kujipatia shahada za uzamili, uzamifu n.k.

Mifano ya utafiti wa kimsingi

Wakati rununu zilipokuja au kugunduliwa, wanasayansi na watafiti mbalimbali walikuwa na hofu kuhusu matumizi ya kifaa hicho cha mawasiliano wakiendesha gari.wao walionelea kuwa kungekuwa na ongezeko la ajali barabarani. Hofu yao haikuwa kwamba eti madereva  wataendesha magari kwa  mkono mmoja huku wakiwasiliana kwa simu  bali  ni kwa sababu ya uzingativu  unaohitajika wakati wa kuongea kwa simu. Makisio yao haya yalitokana na nadharia za kimsingi kwa kwa kutozipa kipaumbele.

Mifano zaidi ya utafiti wa kimsingi.

*      Ugunduzi wa miale ya uyoka(X-rays) ambayo katika uchunguzi wa kasoro kwenye mifupa. Utambuzi wa kropromazini(chropromazine), dawa ambayo hutumiwa   katika matibabu ya sizofrenia(schizophrenia)

*      Utambuzi wa mawiano ya giza ambayo yalisaidia katika maendelezi na makuzi ya nadharia ya kimsingi ya kisayansi  kuhusu hali ya kuona ambayo ilesaidia kupata suluhu ya kutibu maginjwa ya macho yanayoambatana na upofu wa giza na kusoma mialeya uyoka.

*      Utafiti wa kisaikolojia kuhusu kufanya maamuzi ambayo yalikuwa nguzo katika nyanda za elimu, utabibu and uchumi.

*      Matokeo ya kisaikolojia kama inavyojitokeza katika mifumo mbalimbali ya kisheria: utathmini wa ushahidi, ushahidi wakati wa matokeo mbalimbali n.k

 

b.      Utafiti Tumikizi (Applied Research)

Utafiti tumikizi hutafiti kuhusu swala maalum na kutambua ikiwa nadharia fulani inatimiza matakwa yake au la.

Hivyo basi utafiti tumikizi hutumiwa data moja kwa moja ili kutoa suluhisho kuhusu tatizo lililopo wakati uo huo.

Katika  utafiti huu, lengo ni kusuluhishaswala  lililopo katika mazingira husika wakati uo huo. “Keth Stanvich mwanasayansi na mwandishi wa kitabu , To Think Straight About Psychology(2007, ukursa 106)

Kielimu utafiti huu hutumika kubaini ikiwa mbinu fulani zinazotumika zimefaulu au la. Kwa mfano ,matokeo duni  ya mtihani wa Kitaifa(KCPE) katika shuleza serikali nchini yameathiriwa vibaya sana na mfumo wa elimu bila malipo.

c.       Utafiti Kiutendaji (Action Research)

Ni  aina ya utafiti ambao kwamba hufanywa na wale ambao wana nia na lengo la kuchukua hatua katika kusuluhisha jambo fulani katika jamii. Jambo au tatizo hili huwa lile ambalo  limeibuka na  limeikumba jamii wakati maalum na utatuzi wake huhitajika papo kwa papo wala si wakati mwingine.

Mifano ya utafiti wa aina hii:

 

*      Muziki na athari zake kwa wanafunzi katika makuzi ya stadi za uandishi.

*      Sababu za ongezeko la visa vya kunyofolewa sehemu nyeti kwa wanaume katika kaunti ya Nyeri.

*      Sababu za kiwango cha juu cha wanafunzi  hasa wa kike kuachia masomo njiani katika jamii za kuhamahama.

*      Eneo fulani kuathirika na mafuriko ya maji ili kuweza kutafiti ili kupata suluhu la tatizo hilo.

*      Sababu za ongezeko la visa vya wajakazi kuwateka nyara na kutoroka na watoto.

*      Sababu za ongezeko la wanaume kuwaua kinyama wake au watoto wao katika jamii.

 

d.      Utafiti wa Kutathmini (Evaluation Research)

Utafiti wa aina hii hufanywa kwa lengo la kuthibitisha iwapo yaliyotarajiwa ndiyo yaliyotimia. Hivyo basi, utafiti huu huwa wa utaratibu fulani wa kukusanya data kisha kuichanganua data hiyo. Kwa mfano, utafiti wa aina hii unaweza kufanywa kuthibitisha kama mpango wa elimu ya bure umefaulu au la.

 

2.      Uainishaji kwa kutumia mbinu za uchanganuzi

a)      Utafiti wa kueleza (Descriptive Research)

Ni aina ya utafiti ambao unakusanya data ambayo data hiyo itauwezesha utafiti huo kufanya majaribio au kuyajibu maswali yanayohusu mada ya utafiti wakati ule. Huu ni utafiti ambao hueleza jinsi mambo yalivyo.

Utafiti wa aina hii haudhihirishi wazi ikiwa ni wa mfumo wa utafiti wa kimaelezo au wa kiidadi bali huzama katika aina zote mbili wakati wa kuichanganua data.

Hatua zake hufuatana hivi:

  • Kuunda malengo ya utafiti:

Pasi kuwepo na lengo ni muhalisana kufanya utafiti wowote. Hivyo basi mtafiti sharti awe na lengo la kumwongoza kama dira katika ufanyaji wa utafiti wake.

  • Kuandaa vifaa vya kukusanya data:

o   Hizi ni nyenzo muhimu katika swala zima la utafiti. Ni sharti mtafiti aandae vifaa vya kukusanya data akiwa nyanjani.

o   Vifaa hivi vinaweza kuwa vya aina mbalimbali kulingana na sehemu ya kijiografia, tamaduni za walengwa, umri aidha hali ya anga.

Mifano ya vifaa vya ukusanyaji data.

o   Shajara

o   Kamera

o   Video

o   Vinasa-sauti

o   Simu  n.k

  • Kuchagua sampuli.

o   Mtafiti huichukua sehemu fulani kama kiwakilishi cha eneo zima ambalo analiangazia katika utafiti wake.

o   Katika utambuzi wa sampuli, mtafiti huhitajika kuwamakini sana kiasi kwamba kila pembe na viwango vya walengwa vinashirikishwa kikamilifu.

  • Kukusanya data.

o   Huu ndio uti wa mgongo katika utafiti. Ifikapo wakati huu, mtafiti hustahili kuwa makini huku akizingatia miongozo iliyoratibiwa pamoja na kuandamana sako kwa bako na nadharia lengwa.

o   Ifikapo tamati basi data hii inaweza kuhifadhiwa katika vyombo mbalimbali vikiwemo vya kisasa vya kielektroniki.

  • Kuchanganua data.

Katika sehemu hii, mtafiti huongozwa na kuelekezwa kwa kina na nadharia lengwa. Ni kutokana na uchanganuzi huu ambapo mapendekezo yanaweza kufanywa pamoja na kuona iwapo utafiti huo umeweza kuyajibu maswali tarajiwa.

 Kimsingi utafiti wa kueleza hujibu swali la “kwa nini?” maswali ambayo yanaweza kujibika ni kufanya utafiti kuhusu mada yafuatayo:-

Je, walimu wana msimamo na nafasi bora kuhusu matumizi ya vipakatalishi katika shule za msingi nchini Kenya?

Mifano zaidi:

*      Ni mbinu zipi za motisha zisizoonekana wala kushikika  ambazo zinatumika katika karne ya 21 kwenye sekta ya utalii nchini Kenya.
*      Je, ni athari zipizilizopo katika ulaji na matumizi ya chakula kwa wanafunzi wa chuo kikuu chaKenyatta njeya chuo hicho? 
*      Je, tofauti zipiku zilizopo katika vuguvugu la utetezi wa haki za raia na shirika rasmi laserikali lenye shughuli hizo?
*      Uratibu mpya wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na shirika la HELB una madharayapi kwa wasomina yeyote aliye na ari ya kutaka kujiongezea masomo?
*      Je,kuanzishwa kwa kituo cha runinga katika chuo kikuu cha Kenyatta kuna athari zipi kwa wanafunzi?
Ubora wa Utafiti wa kueleza 
*      Ufanisi wa kuchambua mada zisizo kukaguliwa na masuala.
*      Kunao ufanisi mkubwa wa kuchambua na kuchanganua masuala yasiyokadirika.
*      Kunao uwezekano mkubwa wa  kuchunguzanna kutafiti  jambo katika mazingira yake halisi bila kuyabadili.
*      Upo uwezekano na nafasi kubwa ya kuunganisha  mbinu bora katika ukusanyaji wa data.
Matatizo ya  Utafiti wa kueleza 
*      Ni vigumu  kutafiti wala kuthibitishwa suala la utafiti lisilokadirika kitakwimu.
*      Wingi wa utafiti wa kueleza aghalabu si rahisi kuurudia kutokana na mbinu au maumbile ya utafiti huo.
b)     Utafiti Linganishi (Casual – Comparative Research)
Huu ni utafiti ambao hutumiwa katikaulinganishaji wa vigeu ukiwa na nia au lengo la kutaka kuonyesha sababu za jambo au hali  kuwa jinsi ilivyo.
Katika funya hayo, utafiti huu huvilinganisha vigeu pasi kuyaingilia matokeo yake.
Kwa hivyo ni utafiti ambao hujaribu kulinganisha chanzo na matokeo ya haliau jambo.
Sifa zake
*      Hujaribu  kubaini chanzo na madhara ya uhusiano kati ya vigeu tofauti.
*      Inahusisha  ulinganishi wa vigeu.
*      Sampuli haziwezi kuchukuliwa au kuteuliwa bila kufuata utaratibu na kuhusishwa kwa makundi mawiliau zaidi.
*      Haiwezi kuendesha au kuelekeza vigeu ambavyo vinajitegemea.
*      Ina gharama ya chini.
*      Inachukua muda mrefu sana.
Mifano zaidi.
*      Jinsi gani mahudhurio katika shule ya malezi yanaweza  kuathiri ukomavu wa mtoto kijamii mwishoni mwa shule ya msingi?
*      Jinsi gani kuwa na mzazi wa kike anayefanya kazi ya kuajiririwa inavyoathiri mahudhurio ya mtoto shuleni?
*      Ni kwa nini wafafunzi wa chuo kikuu cha Kenyatta wa mfumo wa ODEL hawafanyi vizuri sana katika kozi ya AKS 100 ikiliganiswa na wenzao wa daima chuoni katika kozi iyo hiyo?

c)      Utafiti Wiani (Correlation Research)

Kwa ujumla, utafiti wiani  ni  utafiti ambao unavigeu viwiliau zaidi kutoka katikasampuli moja. Hivyo basi mtafiti huwa kwake anajaribu kutafiti iwapoupo uhusiano mabadiliko katika vigeu hivyo.Kuwepoau kutokuwepo kwa uhusiano ndiyo dira ya utafiti waaina hii.

Kukosekana kwa uwiano katika vigeu husika kutalazimisha utafiti huo kutamatika. Lau uhusiano utakuwepo baina ya vigeu hivyo basi utafiti huu utazidi kupiga hatua ili kutambua aina ya uhusiano ule na chanzo chake.

 Kuna aina tatu za uwiano:
v  uwiano chanya:
Katikaaina hii ya uwiano ni kuwa kuongezeka kwa kigeu kimoja husababisha ongezeko kwenye kigeu kingine. Hii inaashiria kuwa kupungua kwa kigeu kimoja vile vile hulazimisha kigeu kingine kupungua.
Kwamfano:- kiwango cha pesa ailizo nazo mtu huenda zikauiana na idadi ya magari anayomiliki. 
Ama kiwango cha pesa za matumizi alizo nazo mwanafunzi wa chuo kikuu cha Kenyatta huenda kikauiana na aina ya chakula anachoagiza kwenye ukumbi wa maakuli.

v  Uwiano hasi:

Katika uwiano huu, ni kuwa ongezeko la kigeu kimoja husababisha kupungua kwa kigeu kingine.Kwa mfano uboreshaji wa sekta ya elimu nchini unaweza kupunguza visa vya uhalifu katika jamii.Ikumbukwe kuwa sio eti  ukosefu wa elimu katika nchi husababishi  uhalifu katika taifa husuka. Inaweza kuwa ukosefu wa elimu na uhalifu vyotevimesababishwa na hali ya umaskini katika nchi.

 

 

v  Ukosefu wa uwiano:

Katika hali hii, hakuna uwiano wowote katika vigeu vinavyoangaziwa. Kwa mfano, kati ya mabilionea, amani huenda ikakosa kithibitika na pesa. Hiiina maana kuwa ongezeko la pesa haliwezi kusababisha amani katika maisha ya mabilionea.

3 Uainishaji Kulingana na Aina za Utafiti.

v  Utafiti wa Kukagua (Survey Research)

Hii ni aina ya utafiti ambapo mtafiti hukusanya data kutoka kwa makundi husika na ili kutambua haliyake kwa wakati ule kwamujibi wa kigeu kimoja au zaidi.

Utafiti huu huhitaji mtafiti akusanye ujumbe wa kutosha kutoka kwa sampuli.

 

Ujumbe huu unaweza kukusanywa kwa njia ya maswali au hojaji ya moja kwa moja. Hojaji hizi zinaweza kufanywa kwa watu ana kwa ana wakiwa nyumbani,shuleni au hata kazini.Wakati mwingine hata maswali huweza kutumwa kwa njia pepe au kwa kutumia mbinu yoyote ile watu wakayajibu ya kuyatuma yalikotoka kwa kutumia njiaiyohiyo.

Aina mbili za utafiti wa kukagua

§  Maswali(Questionnaires)

Utafiti huu wa kukagua kwa kutumia maswali unaweza kutendeka kwa njia ya mtandao ingawa matatizo huwenda yakawa kuwa kuyapata majibu ya moja kwa moja ni ngumu sana.

Hii ni kwa sababu watu walengwa huyajibu maswali kulingana na vile wana wakati wao wa kutosha. Hii hupelekea matokeo kutoridhisha.

Aina nyingine ya maswali ni ile ambapo sampuli huchukuliwa na kupewa maswali yaliyoratibiwa ili wayajibu papo kwa papo huku wakielekezwana mtafiti.

Mfano mzuri unaweza kuwa utafiti kuhusu taka na athari zake.katika utafiti huu, mtafiti anaweza kuyatoa maswali katika kila nyumba yakajibiwa na kutumwa kwake ama akayangoja yajibiwe papo kwa papo.

§  Hojaji (interview)

Katika hojaji ni kuwa ni kuwa mtafiti hushikiana moja kwa moja na sampuli teule katika kujaliza matakwa yake. Hojaji huchukua muda mrefu kutimilika. Maswali yote huelekezwa na mtafiti. Ingawa mtafiti hastahili kukuelekeza kwenye majibu anayoyatakakuhusu hojaji teule.

 

v  Utafiti wa kihistoria (Historical research.)

Huu utafiti unahusu usomi unaohitajika katika kukusanya ujumbe/taarifa kutoka wakati uliopita. Mtafiti hutafuta data ambayo tayari ipo. Umuhimu wa utafiti huu ni kufikia uamuzi wa chanzo, athari au mfuatano wa mambo yaliyotukia hapo awali na kuona jinsi hayo mambo yameathiri ya sasa na pengine yataathiri yajayo. Mifano ya tafiti za aina hii ni kama:

  • Historia ya jamii ya watu fulani
  • Historia ya mashirika au taasisi za elimu
  • Historia ya vyama vya kisiasa
  • Historia ya kanisa
  • Historia ya tamaduni fulani katika jamii.

 

Utafiti huu ni njia muhimu katika kutafiti, kutambua na kufahamu yale yote yaliyotokea awali na kutambua athari za matukio hayo katika jamii.

Utafiti huu wa kihistoria ni kuwa unampa mtafiti wazo kuhusu swala fulani na namna wazo hilo lilivyokuwa hapo awali.

Udhaifu wa utafiti huu ni kuwa ipo mipaka katika data itumiwayo kulingana na lengo linalotarajiwa.

 

v  Utafiti wa Uchunzaji (Observation Research)

Kwenye utafiti wa aina hii, jambo linachunguzwa kwa kuliangalia tu. Utafiti huu hutoa taarifa ambayo haina hisia za kibinafsi kwa sababu mtafiti huchunuguzana kuangalia hali katika mazingira yake halisi au ya kawaida.

Kwa mfano, mtafiti akitaka kuchunguza nidhamu ya wanafunzi katika shule fulani, atahitaji tu kutembelea ile shule na kukaa mahali – fiche na achunguze au aangalie tabia na mienendo yao bila wao kujua. Katika mazingira ya aina hii, ataweza kupata hali halisi ya wale wanafunzi na kuandika ripoti isiyo na ubinafsi wowote.

 

 

 

Mbinu za uchunguzaji.

1.      Uchunguzaji uliodhibitiwa

2.      Uchunguzaji halisia

3.      Uchunguzaji shirikishi

 

*      Uchunguzaji uliodhibitiwa

Huu ni uchunguzaji ambapo huelekezwa ambao aghalabu hufanywa kisaikolojia katika maabara

Mtafiti huamua mahali ambapo utafiti utafanyikia, wakati gani,na kwa kutumia sampuli zipi na katika hali gani. Hapo mtafiti hutumiwa mbinu iliyojaribiwa na kutambulika wazi.

Mihimili yake

1.      Uchunguzi huu ni rahisi kuigwa na kutumiwa  na wengine kwa kutumia utaratibu uliotengwa.

2.      Data iliyopatikana katika uchunguzi wa aina hii huwa rahisi sana kuichanganua kwa kuwa huwa ya kiidadi (kihesabu)

3.      Huwa ni rahisi kufanyika kwa muda  mfupi.

Udhaifu wake

Uchunguzi huu unaweza kukosa uhalali kwa kuwa mtafiti huwa na dhana kuwa amesimamiwa anapofanya utafiti hivyo basi huenda akatafiti visivyo kwa kuwa katika hofu.

*      Uchunguzaji halisia

Huu ni utafiti ambapo sampuli huchunguzwa ikiwa katika mazingira yake ya asili. Katika hali kama hii mtafiti huhakikisha kuwa kuwepo kwake hakutaathiri ukusanyaji wa data kutokakwenye sampuli lengwa. 

 

Mihimili yake.

·         Kwa kuwa utafiti huu huchunguza tabia katika mazingira yake ya kiasili basi matokeo yake huweza kutoa taswira kamili ya kile kinacholengwa baada ya uchanganuzi wa data iliyokusanywa.

·         Huweza kuibua ujuzi mpya kwa kuwa humpa mtafiti nafasi ya kutafiti hoja kwa ukamilifu.

Udhaifu wake

·         Utafiti huu hufanywa kwa kuangaziwa sampuli ndogo sana hivyo basi huenda hili likaathiri matarajio ya utafiti huo.

·         Ni muhali kwa mtafiti mwengine kurudia utafiti huo kwa kufuata mbinu zilizotumika na mtafiti aliyetangulia.

·         Mtafiti vile vile anahitaji kupata mafunzo ya kutosha ili kuweza kutambua hali ambayo huenda ikahitaji mbinu ya kisaikolojia katika utafiti.

·         Ni muhali ni kubadili vigeu kwa vyovyote vile.  

*      Uchunguzaji shirikishi

Katika aina hii ya uchunguzi, mtafiti huungana au hujumuika na kikundi ambacho anahitaji kukifanyia utafiti. Hivyo  basi mtafiti anachukua nafasi sawana jamii lengwa ambayo angeitafiti kwa kushiriki kikamilifu sawa kama wao.

Katika aina hii mtafiti vile vile anaweza kujibanza mahali kisha akaanza kuchunguza kwa umbali pasi kujulikana wazi na walengwa kwa kila hatua.

Udhaifu wake

a.       Kuna uwezo wa kukosekana kwa usiri wakati wa kutosha kwa mtafiti katika aina hii ya utafiti.

b.      Iwapo mtafiti atajiingiza sana katika kikundi anachokitafiti, upo uwezekano wa kupotea kwa Malengo au kuwepo kwa upendeleo.

 

Marejeleo

*      Ethridge, D.E. (2004) “Research Methodology in Applied Economics” John Wiley & Sons, p.24

*      Fox, W. & Bayat, M.S. (2007) “A Guide to Managing Research” Juta Publications, p.45

*      Quinn,P.M.(1990).Qualitative Evaluation and Research Methods.

*      Nsubuga, EHK (2000)Fundamentals of Educational Research.

*      Mugenda, O. na Mugenda A.M., (1999).  Research Methods Nairobi: ACTS Press.

*      Prewit, K. (1974).  Research Methods.  IDS, University of Nairobi.

*      Lokeshi (1984).  Methodology of Educational Research.

*      Kasomo Daniel, 2006.  Research Methods in Humanities and Education.  Egerton University Press

*      Nyandemo, S.M. (2007) Research Methodology, Methods and Approaches, Richmonds Designers and Printers.

*      Gatara, T.H. (2010) Introduction to Research Methodology.  The Olive Marketing and Publishing Company.

*      Mishra, R.C. (2005) Encyclopedia of Educational Research, A.P.H. Publishing Corporation, New Delhi.

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments