FAFANUA VIPENGELE
MBALIMBALI AMBAVYO VINA UTATA KATIKA UFUNDISHAJI WA SARUFI YA KISWAHILI KISHA
UPENDEKEZE JINSI UTATA HUO UNAVYOWEZA KUONDOLEWA.
Matatizo ya kufundisha
sarufi
1.0:
Utangulizi
Lugha
ya Kiswahili imejikuta katika njia panda hasa kwa kurejelea vipengee mbalimbali
ambavyo vinatia utata katika uelewa wa lugha hii. Baadhi ya vikwazo hivi ni
fundishaji wa sarufi. Kwa kweli sarufi ndio mhimili katika lugha yoyote ile.
Hata hivyo ufundishaji wa sarufi ya Kiswahili una vikwazo chungunzima. Vikwazo
hivi ni pamoja na:-
1.1:Wanafunzi
kukabiliana na sarufi ya Kiswahili kwakutumia lugha yao ya mama.
Hali
kama hii huwafanya wanafunzi kufikiria na kukabiliana na Kiswahili kwakutumia
lugha zao za kwanza. Hili huwa tatizo kubwa sana kiasi kwamba sarufi za lugha
za mama haziingiliani na sarufi ya Kiswahili.
Kwa
mfano katika nafsi za Kiswahili tunapata viwakilishinafsi vifuatavyo:
|
NAFSI |
UMOJA |
WINGI |
|
1 |
NI |
TU |
|
2 |
U |
M |
|
3 |
A |
WA |
Zipo
baadhi ya lugha mama hasa za kinailoti ambazo huvitumia au kuhamisha viambishi nafsi vya lugha yao hadi
Kiswahilipasi kufahamu madhara wanayoyaleta kwenye sarufi ya Kiswahili.
Kwa
mfano katika lugha ya Waluo, utagundua kwamba wao hutumiwa kiwakilishinafsi A
kurejelea nafsi ya kwanza hali ya umoja ambapo katika Kiswahili huwa nafsi ya
tatu umoja.
Utawaskia
wakisema :
a. Abiro-Ninakuja
b. Adwaro-Ninataka
Katika
mtindo huo, wapo wale ambao huhamisha nafsi hii namna ilivyo hadi kwenye
Kiswahili. Utawaskia wakisema:
a.
Mimi
anaenda shuleni.
Badala ya :Mimi ninaenda shuleni.
b.
Mimi anaandika
polepole.Badala ya:Mimi
ninaandika polepole.
c.
Mimi anasoma
haraka. Badala ya:Mimi
ninasoma haraka.
Kwa
kufuata mifano ya hapo juu itaonekana wazi kuwa wanafunzi kutoka maeneo hayo
ambao huitumia lugha yao ya kwanza kama kioo wanaposoma sarufi basi wana kazi
ya ziada.
Hivyo
basi wanafunzi hawa hustahili kuiacha kando lugha yao ya mama wanapoikabili
sarufi ya Kiswahili la sivyo hali itawaendea mrama.
Waaidha
zipo lafundhi za lugha hizi za kwanza ambazo huathiri san sarufi ya Kiswahili
katika lugha ya Kikamba wengi wao hutamka konsonanti J kama Y. Utagundua kwamba
asilimia kubwa ya Wakamba wanapozungumza mahali palipo na J watatamka Y.
Kwa
mfano:
|
KISWAHILI |
KIKAMBA |
|
Jua |
Yua |
|
Juu |
Yuu |
|
Juni |
Yuni |
Waaidha
palipo na sauti G wao hupachika NG
Kwa
mfano:
|
KISWAHILI |
KIKAMBA |
|
Goli |
Ngoli |
|
Gareji
|
Ngaleji
|
|
Goti
|
Ngoti
|
Palipo na R wanaweka L.
|
KISWAHILI |
KIKAMBA |
|
Rudi |
Ludi |
|
Rarua |
Lalua |
|
Rinda |
Linda |
|
Mrembo |
Mlembo |
Mfano
mwanafunzi hataeleweka iwapo ataambiwa aisome sentensi kama hizi;
a. “Linda ana rinda refu lililoraruka
vibaya.”
b. “Mimi ni fundi wa kupaka rangi”
Utamsikia
mwanafunzi akitamka:
a. “Linda ana linda lebu lililolaluka
bimbaya.”
b. “Mimi ni bundi wa kubaka langi.”
Katika
hili kama hii sarufi hufanywa chapwa mno.
Katika
mfumo huo, jamii ya Waluhyia haijasazwa nje. Katika jamii hii utagundua kuwa
lafudhi yao wakati mwingine huwatia mashakani katika uchambuzi na usomi wa
Kiswahili.
Wengi
wao badala ya sauti B hutia P, Sauti Z hutia S, D hutia T
Kwa
mfano:-
|
Matamshi
bora ya Kiswahili |
Matamshi
bandia ya Kiluhyia. |
|
|
1 |
Baba |
Papa |
|
2 |
Bora |
Pora |
|
3 |
Bata |
Pata |
|
4 |
Bure |
Pure |
|
5 |
Bei |
Pei |
|
6 |
Birika |
Pirika |
|
7 |
Bila |
Pila |
Sauti
Z na S
|
Matamshi
bora ya Kiswahili |
Matamshi
bandia ya Kiluhyia. |
|
|
1 |
Mzuri |
Msuri |
|
2 |
Mzee |
Msee |
|
3 |
Mzinga |
Msinga |
|
4 |
Muziki |
Musiki |
|
5 |
Mkizi |
Mkisi |
|
6 |
Zambarau |
Sambarau |
|
7 |
Mzigo |
Msiko |
Sauti
D na T
|
Matamshi
bora ya Kiswahili |
Matamshi
bandia ya Kiluhyia. |
|
|
1 |
Dada |
Tata |
|
2 |
Daktari |
Taktari |
|
3 |
Dadisi |
Tatisi |
|
4 |
Dereva |
Tereva |
|
5 |
Darasa |
Tarasa |
|
6 |
Domo |
Tomo |
|
7 |
Daka |
Taka |
Kwa
kuangaziwa athari za hapo juu ni dhihirisho tosha kuwa kufundisha sarufi katika
mazingira hayo huwa kugumu sana. Tatizo kubwa ni kupata kuwa mwalimu na
wanafunzi wote wana shida moja ingawa hawajagundua shida kama hiyo miongoni
mwao.
Hivyo
basi, ni muhimu kwa msomi au mwelekezi ambaye kwa njia moja au nyingine ana
tatizo kama hili basi ni muhimu kuzingatia sauti za Kiswahili pamoja na
konsonanti zote hukuakitilia maanani matamshi bora ambayo hayataathiriwa na
lugha zao za kwanza.
Kwa
hivyo athari kama hizi vile vile ni kuangaziwa kwa somo linalohusu konsonanti
na sauti katika Kiswahili ili kujenga msingi imara katika matamshi ambayo
huathiri sana sarufi ya Kiswahili.
Ikiwa
hili halitapata tiba mapema litakuwapo tatizo kubwa hasa wanafunzi waathiriwa
wanapoangazia somo kuhusu sentensi zenye utata vitatamshi.
1.2:Athari za
Kiingereza kwa Kiswahili kisarufi
Matatizo
katika sarufi ya Kiswahili huchangiwa vile vile sarufi katika somola
Kiingereza.
Hapo
hujitokeza sana kwa wasomi ambao wamemudi sana lugha ya Kiingereza hivyo basi
kuwa na dhana potofu kuwa sarufi ya Kiswahili ni sawa na Kiingereza pasipo
Kujua kuwa hizi ni lugha mbili tofauti na zilizo na miundo tofauti ya sentensi.
Kwa
mfano katika Kiingereza utagungua kuwa kivumishi(adjective) hutangulia nomino
kwenye sentensi. Kwa mfano:
Two
boys were punished(Neno two ni kivumishi kinachotoa sifa zaidi kuhusu neno
boys)
Iwapo
sentensi hii itahamishwa kimuundo hadi Kiswahili, itakuwa:
Wawili
wavulana waliadhibiwa(V+N+T). Hapa sentensi hii itakuwa imevunja kanuni za
sarufi ya Kiswahili ambapo huwa na mfumo huu N+V bali sio V+N. Hivyo sentensi
hii inafaa kuwa:
Wavulana
wawili waliadhibiwa.(N+V+T)
A
good meal was eaten.(Neno good ni kivumishi kinachotoa sifa kuhusu neno meal)
Sawasawa
na mfano tangulizi sentensi ii hii Vilevile itakuwa na utata wa kisarufi kwani
itasoma: Kizuri chakula kililiwa (V+N+T) badala ya Chakula kizuri
kimeliwa.(N+V+T)
Waaidha
utagundua kuwa katika nafsi za Kiingereza huwa nafsi ya pili(you) hujitokeza kabla ya nafsi ya kwanza hasa
unaporejelea swala fulani kwa mfano:
You and I were punished yesterday.
Bali katika Kiswahili hutangulia na nafsi ya kwanza ndipo ya pili ikafuata.Hivyo basi sentensi ii hii itasoma: Mimi na wewe tuliadhibiwa jana bali sio Wewe na mimi tuliadhibiwa jana.
Vile
vile katika ukanushi wa vitenzi katika Kiingereza wakati mwingine Ufupisho
hukubalika bali katika Kiswahili Ufupisho ukitumika mantiki na ufasaha lengwa
utakosekana.
Mfano:
If you force me to go to school, I won’t.
katika sentensi hii iwapo neno I wont litabakishwa jinsi lilivyo bado
litaeleweka. Iwapo sentensi ii hii italazimishwa kimuundo katika Kiswahili
kwakufupisha kitenzi katika hali yakutoa dhana ya Ufupisho sentensi hii itasoma
hivi:
Ukinilazimisha
kuenda shuleni,sita. Sasa hapa neno sita halijakamilika. Lina kikanushi(si) na
kiwakilishi wakati (ta) bila kitenzi. Kwa hivyo sentensi haitakuwa na maana.
Ingefaa iwe: Ukinilazimisha kuenda shuleni,sitaenda.
Kwa
hivyo si bora kutumia muundo wa sarufi ya Kiingereza katika kujifunza au
kufundisha sarufi ya Kiswahili.kwa hivyo ni muhimu kila mmoja kukita tu katika
miundo ya sarufi ya Kiswahili pasi kuchanganya na ile ya Kiingereza.
Wakati
mwingine utakuta kuwa mwalimu amesombwa na kasumba ya Kiingereza wakati wa
Kiswahili kiasi kwamba anatumia lugha zote wakati mmoja katika
kufundisha.unapomsikiliza mwalimu kama huyu utashindwa kuelewa iwapo anafunza
Kiingereza au Kiswahili kwenye kipindi kimoja.
Inastahili
masomo hayo yapewe heshima sawa na kukubalika na utawala ima uwe wa shule,
taassisi au chuo chochote. Wanafunzi waweze kupewa siku zaidi ya moja kwajuma
kuwasiliana kwa Kiswahili na pia ingekuwa bora walimu wa masomo mengine kutumia
siotu Kiingereza wanapofundisha masomo yao bali vile vile watumie Kiswahili ili
kiweze kukwea na kumea mizizi.
1.3:Kiswahili
kuchukuliwa kama lugha duni.
LICHA ya
hadhi na umaarufu wa Kiswahili ndani na nje ya nchi, bado lugha hii inakumbana
na matatizo makubwa ya dhana na matumizi sahihi. Kuna baadhi ya watu
wanaonasibisha Kiswahili na dini ya Kiislamu na hili limekuwa ni tatizo kubwa
miongoni mwa watumiaji wake. Hapa utagundua kuwa ile kasumba iwapo itamwingia
msomi kwa misingi hiyo basi hawezi kuwa na umakinifu wa kuizingatia ifaavyo. Na
pasipo mtu kuwa na msukumo katika kile afanyacho basi hawezi kutia bidii na
juhudi hata kidogo.
Hii hata
hudhihirika wazi wakati unapotembelea mwuza-magazeti kisha uagizie gazeti la
Kiswahili mfanoTaifa Leo, mwuza-magazeti yuyo huyo ndiye atakayekuwa wa kwanza
kuanza kushuku kuwango chako cha elimu na uelewa wako wa mambo. Sababu ni kuwa
umenunua gazeti la Kiswahili. Kwa hivyo iwapo jamii kwa jumla haitabadili
mafikiro haya basi mwalimu atazidi kuwa na ugumu katika kuifunza sarufi katika
lugha ya Kiswahili kwa kuwa wanafunzi wameathirika na msimamo wa jamii.
Pia kunao upinzani mkubwa kutoka katika lugha
ambazo zimekwisha kujitanua kimatumizi kote duniani kama vile Kiingereza,
Kifaransa, Kihispania, Kijerumani, Kichina, Kireno na Kiarabu. Watumizi au watu
wenye asili ya lugha hizo wanakipiga vita Kiswahili wakihofia kuwa wasipofanya
hivyo kitazimeza lugha zao katika siku za usoni.
Hali kama hii huathiri sana
mwalimu wa Kiswahili. Kwa mfano iwapo mwalimu atajikuta katika shule ya
Kimataifa ambapo lugha ya lazima ni Kiingereza bali Kiswahili kiwe mwongoni mwa
masomo ya kuteua, basi wanafunzi wengi wataangukia lugha nyingine kama
kifaransa, kijerumani, au Kiarabu ma
kuachilia mbali Kiswahili.
Kudharauliwa kwa lugha ya
Kiswahili na kupigiwa chapuo kwa lugha nyinginezo za kigeni kwamba ndizo pekee
zinazofaa kutumiwa katika shughuli mbalimbali za kiuchumi kwa kuwa zina hadhi
ni changamoto kubwa.
Papo hapo utagundua kuwa hata
teknolojia inaweka nguvu sana katika masomo ya kisayansi huku lugha hasa
Kiswahili zikiteketea kwani kila mtu kwa sasa anaimba wimbo wa kunawiri
kisayansi pasipokujua kuwa huyo mwanasayansi huenda akahitajika kutekeleza
wajibu wake katika maeneo yanayotumia Kiswahili tu! Hali hii vile vile ya jamii
kuzipa kipaumbele taaluma nyingine hasa za uhandisi huku maswali ya kukuza
lugha kama Kiswahili yakitupiliwa mbali
1.4:Kutoweka
kwa Kiswahili katika matumizi.
.kuwa na mazoezi katika kila
ufanyacho huwa nyenzo muhimu na Mihimili katika udhibiti wa kila ufanyacho. Katika
mtazamo huo itakubalika kuwa wasomi wengi hawana mazoea katika kuendeleza kile
wanachokisoma nje ya darasa. Utagundua kuwa kila wanachokisoma hubakia langoni
pa darasa hadi wakati mwingine wa kipindi.
Hata iwapo mwalimu ataangazia
mada ambayo wasomi wanahitaji kuifanyia mazoezi ya maongezi hawajatilii maanani
kabisa. Wapo wasomi wngine ambao hata wakipewa kaziya ziada, kuifanya ni
mtihani au ngoma. Kwa hivyo ifahamike
kuwa msomi yeyote ni wa kujituma na huku kujituma kuna mambo mengi ya kujitolea
mhanga. Itakumbukwa kuwa apatacho msomi kutoka kwamwekekezi wake ni asilimia
ndigo sana bali mzigo mkubwa unatoka kwake msomi mwenyewe.
Isije ikwa haliya kusema ati “Bora nimewasiliana si lazima kanuni”La
hasha! Ndio maana vazi si vazi tu bali huwa vazi linapovaliwa sehemu ifaayo tu!
Katika hali hiyo utagundua kuwa wasomi wetu hawajakuwa na hamu na tama ya
kutaka kusoma mara kwa mara. Wamekuwa wavivu sana hasa kwa kutaka kutabaradi
bila kufanya cha mno kuhusu mustakabaliwao.
Sarufi kama somo lolote huhitaji kutengewa
muda wa ziada na binafsi.hii ni kwa mwanafunzi husoma vyema hasa
anapojigundulia mambo mbalimbali. Msomi
Kama huyu hupata balaa na beluwa hasa anapokuwa na nia ya kukwea ngazi
kielimu kufikia uzamili au uzamifu. Hapo ni kuwa mwandani wa kusoma kwa kupanua
na kujifunza ujuzi mpya.
Hali hii imewafanya baadhi ya wasomi kutopata
hata wasaa wa kufunua Kamusi ya Kiswahili. Wapo wasiojua kuwa kila neno katika
Kamusi huelezwa ni aina gani ya neno(Nomino, kitenzi, kivumishi n.k).Hivyo basi
bila kuwa mpenzi wa Kamusi basi kutakuwa na ugumu sana katika kubaini na
kuichanganua maneno yanayotumiwa katika kukisoma Kiswahili.
Kwa
hivyo wasomi watengewe muda wa kutosha wakusoma huku wakielekezwa ifaavyo. Ni
bora wanafunzi wawe na aghalabu kipindi kimoja kwa wiki cha maktaba ambapo watapata fursa ya
kujisomea huku wengine wakielezwa. Kuhusu matumizi ya kamusini bora iwapo
wasomi watazoeshwa mapema namna ya kuitumia Kamusi wakiwa katika madarasa ya
awali.
1.5: Athari za
vitandazi na mitandao ya kijamii.
Ieleweke
kuwa Kiswahili kimeingia mtandaoni hivi karibuni baada ya lugha nyingine nyingi
kunawiri kwenye mtandao. Hata vile vile kimeingiakama kwenye ukumbi wa Google
transalate ikumbukwe kuwa huo ni ukumbi tu wa kutafsiri tena tafsiri sisisi
ambapo hazikupi maana ya neno namna linavyostahili kuwa.
Tukiwa
bado kwenye mtandao, kuwa vitandazi kama face book, tweeter, whatsup, histogram
n.k
Vitandazi
hivi vimeteka jamii bakunja kwamatumizi ya mikato ya maneno. Vifupisho hivi
huathiri sarufi moja kwa moja.Waaidha utapata kuwavitandazi hivi vimezidisha
uzembe katika usomi na kufanya mazoezi ya uandishi kwa kukosa kujuamaendelezo
sahihi ya neno.
Hapo
hapo kwenye mtandao utagundua kuwa nguvu za msongarika(peer pressure)
zimewatanda wasomi kiasi kwamba wanahimizana kutozingatia wakifanyacho wakiwa
nje ya darasa. Hii hi kwa kuwa wamebadili lengo lao la mawasiliano na kuwa
ukumbi wa kujadilitu maswali mengine ya kijamii pasi Kujua kuwa jamii
haikamiliki pasi usarufi wa lugha na mawazo. Kwa hivyo hili huwapelekea wasomi
wengi kutumia lugha chapwa isiyojua kuwa zipo kanuni zinazifaa kufuatwa ima
katika uandishi au uzungumzi.
1.6:
Kiswahili kukosa udugu au ujirani na masomo mengine shuleni.
Katika
shule zote, Taasisi hata vyuo vyote nchini Kiswahili ndiyo lugha ya pekee
ambayo ni yatima katika kuifundisha. Mfano
tu ni kuwa katika shule za msingi wanafunzi huyasoma masomo
haya:Sayansi,Hisabati, Kiingereza,Somo la Jamii Kiswahili, Stadi-ishi(life
skills) Tarakilishi n.k.Ni ukweli mtupu kuwa masomo hayo mengine isipokuwa
Kiswahili huingiliana.
Walimu wa masomo hayo yote wanapoingia darasani kwa
njia moja au nyingine hufundisha sarufiya Kiingereza.Hii ni kwa kuwa masomo
hayo yote hufunzwa katika Kiingereza na mtihani vile vile kuandaliwa katika
lugha ya Kiingereza.kwa hivyo kwanjia moja au nyingine lugha hizi hukipiga
msasa Kiingereza huku Kiswahili kikibaki yatima kwani hubakitu pekee katika
lughayake pekee. Atokapo mwalimu darasani hadi atakaporudi ndipo lugha hiyo
labda isikike kinywani mwa mwalimu.
Kuongeza
msumari moto kwenye kidonda ni kuwa katika shule nyingi nchini wanafunzi hupewa
siku moja tu ya kuwasiliana katika Kiswahili huku Kiingereza kikibaki na siku
nyingine zote. Hii inakinyima Kiswahili fursa ya kunawiri. Kwanza heri siku
moja. Zipo shule nyingine ambazo kuwasiliana kwa Kiswahili nje ya somo la
Kiswahili ni hatia kubwa ambapo adhabu
yake haitamaniki.
Ikiwa
hata sheria za shule hazimruhusu mwalimu wa Kiswahili kuwasiliana na wasomiwake
kwa Kiswahili atikwa kuhofia kupigwa kalamu basi huko ni kudidimiza ari ya
kukua kwa lugha hii.
1.7: Uzalizaji na
utumiaji wa msamiati bila mpangilio
Ikumbukwe
kuwa kukua kwa msamiati ni kukua kwa lugha yoyote ile. Hata hivyo hili
haliangaziwi na baadhi ya watumizi wa lugha hii.wengi wao wamekuwa na kasumba
ya kuibuaibua msamiati bila kuelewa mbinu zifaazo kuzingatiwa. Ukasuku kama huu
hauleti Ladha kabisa kiasi kwamba wasomi huchanganyikiwa kabisa.
Vile
vile ni muhimu kugundua kuwa ukasuku katika uumizi wa lugha ya Kiswahili una
athari zake. Ikumbukwe kuwa kabla ya kulitumia neno ni muhimu kulifanyia neno
hilo utafiti ndipo ulifahamu fika asili
na matumizi yake barabara.
Kwa
hivyo ni muhimu kufanya utafiti ufaao kwa kila neno ukutanalo nalo kabla ya
kuanza kulitumia.
1.8: Athari za vyombo
vya habari
Sarufi ni utaratibu maalumu wa
lugha husika. Utaratibu huu ni kanuni, sheria au kaida nyingine zinazotawala
mfumo mzima wa lugha ili iweze kukubalika na kueleweka katika matumizi ya lugha
hiyo kwa wanajamii. Hivyo tunapoongea sarufi ya lugha moja kwa moja tunalenga
utaratibu maalumu wa lugha Fulani. Kama zilivyo lugha nyingine, Kiswahili kina
utaratibu wake pia, yaani sarufi ya Kiswahili, ambayo inafanya lugha hii kuwa
katika utaarabu wake.
Katika matumizi ya lugha, wadau
wengi wa habari hasa waandishi, wa habari, watangazajia, na wahariri wa habari,
wamekuwa wakifanya makosa ya kisarufi ya mara kwa mara katika habari
wanazoandika na kuzichapisha kama zilivyo. Habari za magazetini, kwenye
mitandao, runinga, hata zile zinazosikika redioni, hujaaa makosa mengi ya
kisarufi. Makosa hayo ni kama kuchanganya au kuhazima sarufi ya lugha za kigeni
kama kiingereza na kuitumia katika Kiswahili; mathali, mtangazaji katika
kujitambulisha anaweza kusema "yangu
majina" badala ya jina langu; "yangu
matumaini" badala ya matumaini yangu. "Yangu Majina"
ni sarufi ya kiingereza sio ya Kiswahili, alafu katika Kiswahili hatuna dhana
ya;majina' kwa mtu mmoja, bali tuna jina.
Katika utaratibu sahihi wa
Kiswahili, jina/nomino hutangulia kivumishi na kivumishi hufuata kwani
kivumishi hufanya kazi ya kutoa sifa kwa jina, ila kwa kiingerza utaratibu ni
tofauti kwani kivumishi huweza kutangulia nomimo; mfano: my name (jina langu),
beautiful lady ( binti mrembo), strong
man (mtu shupavu) n.k. Katika
mifano hii, tungo za Kiswahili kwenye mabano ndio muundo sahihi kisarufi wa
Kiswahili lakini kiingereza ni tofauti kwani katika kiingerza kivumishi
hutangulia nomino katika mazungumzo au maandishi.
Vilevile kutofuata kanuni za lugha ya
Kiswahili imekuwa ni jambo la kawaida kwa wanahabari. Imekuwepo kasumba kwa
baadhi ya watangazaji na waandishi wa habari hapa nchini kusema au kuandika
neno "jumbe" wakiwa na dhana ya wingi wa;ujumbe'.
Hakika katika taaluma ya sarufi ya Kiswahili hatuna wingi "jumbe" kwa
maana ya ujumbe.
Katika
vyombo hivi Vilevile tumekuwa na hali ya kubuni maneno ambayo hayana ithibati
ya matumizi na kuyatumia katika lugha pamoja na matumizi yasiyo sahihi ya
maneno katika lugha.
Kosa hili limeshika kasi sana
katika maisha ya sasa ya vijana na uga mzima wa habari. Katika mitandao ya
kijamii, redio, runinga na magazetini yamekuwepo matumizi ya maneno ya kubuni
na yamezoeleka ni ya kawaida kumbe sio. Pamoja na hayo yapo matumizi ya maneno
ambayo sio sahihi kwa maana yake halisi. Mfano kuna maneno kama "tiririka au funguka" ;
hutumika kumaanisha mtu kujieleza au kutoa ya moyoni( kwa matumizi ya sasa);
matumizi ya maneno hayo sio sahihi katika mantiki yake ya msingi maneno haya
kwa Kiswahili. Pia kuna "ngoma" kwa maana ya wimbo/muziki n.k.
Wanahabari wawa hawa vile vile
wamekuwa na kosa la kuchanganya lugha mbili au zaidi(Kiswahili na KiingerezaLugha ya Kiswahili imekumbwa na
wimbi hili zito la baadhi ya watu wengi kuchanganya lugha ya Kiswahili na lugha
za kigeni.
Katika uga wa habari jambo hili
siku hizi ni la kawaida. Ipo misemo, maneno ya kiingereza na lugha nyingine,
ambayo hutumika kama maneno ya Kiswahili. Magazeti mengi na makala huandika
habari kwa kuchanganya maneno ya lugha mbili tofauti. Mfano, "wikiendi/wikendi (mwisho wa
wiki); wachezaji walikuwa kambini wakifanya training ya viungo; habari
zilizotufikia katika newsroom (chumba cha habari), reporter wetu (mtoa habari
wetu); time imekata(muda umeisha) n.k". Kwa mfano kule Tanzania katika gazeti
la mwana sporti namba 1217 la tarehe 3 hadi 6, mwaka 2012, ukurasa wa 18, kuna
kichwa cha habari kimeandikwa hivi,;First Eleven ya waliofunga mabao mengi'. Hivyo basi kuchanganya lugha sio
taratibu sahihi katika kuhimarisha lugha. Ikumbukwe
kuwa kazi ii hiiya uanahabari huzagaa haraka sana na ikiwa ina athari hasi basi
sarufi ya Kiswahili hupata pigo kubwa.
Lugha ya Kiswahili ni lugha
yenye sifa zote na inayokidhi mawasiliano miongoni mwa watumiaji wake kama
zilivyo lugha nyinginezao hapa ulimwenguni, hivyo inapaswa iheshimike na
ithaminiwe sawa kama lugha nyingine. Na kufanya hivyo, upendo katika lugha hii
utakuwepo na kuitangaza lugha hii kimataifa. Sanjali na hili, ni jukumu letu
sisi sote wapenzi wazalendo kuifuatilia
na kuisoma lugha hii kwa undani ili tuweze kuwa wamaizi kwa undani wake na
kupunguza makosa madogo madogo madogo yanayosababisha lugha hii kutoendelea.
Tasnia ya habari, ni sehemu muhimu katika
kuleta mchango na maendeleo makubwa katika jamii, na hivyo basi kupitia dhamana
hii, vilevile wanahabari wanayo nafasi kubwa kuithamini, kuipenda, kuisoma na
kuiendeleza lugha ya Kiswahili katika kutoa taarifa na babari katika jamii husika.
Hii itaenda sambamba endapo wanahabari watafunguka macho na kuona umuhimu wa
kusoma Kiswahili kama taaluma ya kumwezesha mtu kupata cheti kama mwanatabari.
Makosa ya kisarufi, kuchanganya lugha, na mengineneyo hayataonekana katika
matini mbalimbali za habari huku wahariri wakitakiwa kuwa ni wenye ujuzi wa
lugha hii.
Wakati mwingine utamsikia
mwanahabari mtangazaji akisema kuwa: “Majangili
wawili waliivamia benki moja katika mji wa
……………………………………….” Iwapo magangili watawageuza watu kuwawanyamapori kisha
wawavamie basi hapo ni hatari kabisa, Majangili kwakawaida hawani wawindaji
haramu wa wanyamapori, sasa itakuwa je sasa hawa majangili wamegeuza benki zetu
kuwa hifadhi za wanyamapori? Wapo wengine ambao husema “ Gari waimokuwa wakisafiria lilipata ajali na kuwaua watu watatu papo
hapo”. Huku ni kuitia kitanzi sarufi ya
Kiswahili moja kwa moja.
Hapa ni kuwa mtangazaji huyu
hafahamu chochote kuhusu ngli ya mahali (PAKUMU) wala matumizi yake ni usiku wa
giza. Angefaa kusema “Gari walilokuwa
wakisafiria lilipata ajali na kusababisha vifo vya watu watatu”.Ukasuku huu
haufai katu na ndio unadidimiza juhudi za kuikuza sarufi ya Kiswahili.
Kupitia juhudi hizi, hakika,
watumizi wa Kiswahili wote tukishirikiana tunaweza kuiendeleza lugha yetu murua
ya Kiswahili na kuitangaza kimataifa
1.9: Ngeli za Kiswahili na athari zake.
Ngeli zimewachanganya wengi
sana. Hasa kwa kukosa kufahamu namna ya kuvitumia viambishingeli kwenye mafungu
tenzi hasa wakati nomino mbalimbali zinapotumika.
Kwa mfano ukitazama ngeli ya A-WA
maelezo yake huwa ni ngeli inayorejelea ya
majina ya viumbe wenye uhai k.v watu, wanyama, ndege,samaki, wadudu, miungu,
malaika n.k Majina mengi katika ngeli ya A-WA huanza kwa sauti M- kwa umoja na
sauti WA- kwa wingi.
Katika ufafanuzi huu wa nomino
wakati mwingine utangundua kuwa ufafanuzi huu una dosari kiwango fulani wakati
msomi anapoanza kuangaziwa nomino zizo hizo lakini katika hali ya ukubwa. Mfano
jitu,janadume,gombe n.k. kwa vile wanafunzi huenda wasitambue wenyewe kuwa
nomino katika ngeli hii huihama hasa zinapukuzwa, huwa vigumu sana kumenyana
nazo kisafufi.Mfano mzuri ni mazoea ya kutumia neno JIBWA kwa wengi wetu
kurejelea Mnyama huyu katika hali yake ya Kawaida. Kasumba kama hii huwa hatari
sana kiasi kwamba kumrekebisha huyu msomi ni mtihani.
Inastahili maelekezo kuzihusu
ngeli yawekwe wazi kwa kutalii hali zozote ambazo huenda zikabashiriwa kuwa
zinaweza kuleta utata katika kuzichanganua.
Katika usanjari huo zipo
sentensi ambazo zinaweza kulazimishiwa katika wingi ingawa mantiki yakakosekana.
Baadhi ya sentensi hizi ni zile ambazo zinarejelea nomino za pekee hasa majina
ya watu.
Mfano wa sentensi kama hizi ni:
a.
Maria aliliruka shimo
b.
Daktari Jactone Onyango aliwasili darasani mapema.
c.
Bwana Omukabe ni mwanafunzi wa shahada ya uzamili katika chuo kikuu
cha Kenyatta.
Katika mifano hii ya hapa juu
ni kuwa iwapo katika sarufi wasomi watalazimishiwa kuzibadili katika wingi huku
wakirejelea sifa za ngeli ya A-WA , huenda umaantiki ukakosekana kabisa.
Zipo nomino nyingine ambazo
haziwezi kujikuta katika ngeli zozote labda paibuke ngeli nyingine ya A-WA.
Nomino hizini zile ambazo hurejelea majina ya vitu vya kufikirika na majina
halisi ya watu. Mfano wa nomino hizi ni:-
a.
Mungu
b.
Yesu
c.
Mtume Muhammed
d.
Omukabe
e.
Onyango n,k
Itabidi utafiti wakina ufanywe
ili kuziorodhesha nomino hizi ifaavyo. Wapo wanaonadi kuwa zipo katika ngeli ya
A-WA huku wengine wakilonga kuwa ngeli yake ni A-A.Wakati wa kuichanganua swala
hili huleta utata sana miongoni mwa wasomi.
Katika hali iyo hiyo ipo nomino
ambayo hadi sasa hapajaibuka maelezo yafaayo kuihusu. Nomino yenyewe ni MAITI.
Wapo wanaosema kuwa hii ni nomino katika ngeli ya A-WA huku wengine wakisema
kuwa ngeli yake ni I-ZI.
Kwa hivyo ni bora sana iwapo
wahusika watatoa mwelekeo ufaao kuhusu swala hili la ngeli ili kila mmoja aweze
kunufaika.
Waaidha katika karne hii,
teknolojia imeshika kasi sana kiasi kwamba, msamiati unazalika kucha kutwa. Kwa
hivyo ni bora zaidi iwapo washika dau wote kushika kasi katika swala
lauainishaji wa msamiati huu ili ngeli zake zieleweke barabara.
Kwa kutokosa namna ya
kuziainisha nomino hizi katika ngeli, wengi wamejikita wakizilazimishia katika
ngeli ya I-ZI.
Ili kuondoa utata huu.
Ambaokwamba umekithiri na kuisonga Sarufi ya Kiswahili, ni muhimu sana kwa wahusika
kuweka mikakati kabambe ambayo itaondoa utata huu. Iwapo hili litafanywa basi
jamii haitakuwana ugumu wowote katika usomi wa sarufi ya Kiswahili. Sera
borazaKiswahili ziwekwe na kuheshimika iwe shuleni au popote ambapo usomi wa
Kiswahili upo.
Jamii vile vile inafaa iondoke
katika fikra potovu za kupitwa na wakati ati Kiswahili nilugha ya watu duni
wasioelimika. Hili litasaidia sana kuikuza lugha hii katika vizazivya sasa na
vijavyo.
1.10: Ufinyu wa Vitabu vya utafiti wa sarufi ya
Kiswahili
Kwa hakika hili ni swala zito
mno ambalo linakandamiza sarufi ya Kiswahili katika viwango vyote ingawa
viwango vya juu ndivyo vinavyoathirika pakubwa. Ukiingia katika maktaba yawe ya
umma au ya Taasisi yoyote ile ni muhali kuvikuta Vitabu vya Kiswahili. Kutia
msumari moto kwenye kidonda ni pale ambapo mwanafunzi wa kozi ya uzalimi au
uzamifu katika vyuo vyetu vikuu anapopewa mwongozo wa kozi utagundua kuwa
kupatika na kwa kitabu cha Marejeleo cha Kiswahili ni usiku wa giza.
Wingi wa Vitabu hivi ni vya
Kiingereza. Katika hali hii mwanafunzi anastahili awe na ustadi wa lugha hizi
mbili ili aweze kutafsiri anachokitalii katika Kiingereza huku akikitasiri
katika Kiswahili. Kitendawili hapa ni kuwa, wakati msomi huyu anapofanya hivi
basi moja kwa moja anachangia katika maendelezi ya sarufi ya Kiingereza huku ya
Kiswahili ikizidi kuporomoka.
Kwa hivyo ni bora iwapo Vitabu
vya Marejeleo viwe vile vimeandikwa katika lugha ya Kiswahili tu basi sio
Kiingereza. Cha kushangaza ni kuwa wafanyao kozi za juu katika Kiingereza
hawavitumii Vitabu vya Kiswahili kama vyombovya Marejeleo.
MAREJELEO
1)
Massamba, D.P.B. (2011). Maendeleo Katika Nadharia ya
Fonolojia. Taasisi ya Taaluma za
Kiswahili chuo Kikuu cha Dar es salaam. Dar es salaam: TUKI.
2)
Massamba, D.P.B. (2004). Fonolojia ya Kiswahili Sanifu
(FOKISA), Sekondari na Vyuo.
Dar es salaam. TUKI
3)
Matinde, R.S. (2012) Dafina ya lugha, Isimu na Nadharia Sekondari
Vyuo vya kati na vyuo Vikuu. Mwanza: Serengeti Educational Publisher (T) Ltd.
4)
Chomvisky, NN.& Halle,M.(1968)The sound pattern of English New
York: Harper & Row
5)
Massamba, D.P.B(2012)Misingi ya Fonolojia. Dar es Salaam: TATAKI.
6)
Massamba, D.P.B(2011) Maendeleo katika Nadharia ya Fonojia .Dar es
Salaam:TATAKI
7)
Massamba, D.P.B(2004)Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha.Dar es
Salaam: TUKI.
8)
Jensen, J.T.(2004) Principles of Generative Phonology:An
Introduction . Amsterdam: John Benjamins Publishing House.
9)
Kenstowicz, M(2006) “Generative Phonology”. Katika Brown, K na
wenziwe, (wah)
10) Encyclopedia of
Language and Linguistics(2nd ed.) uk. 3276-3286.Elsevier Ltd
11) Kiparsky, P. (1968) ‘How
abstract is Phonology?’Bloomington, India: Indiana University Linguistics Club.
12) Lass, R.(1984)
Phonology: An Introduction to basic concepts.. Cambridge University Press.
13) Chiduo,
E.( 2002),”Syno nymy: A Defining Method in the Standard Swahili Dictionary: Its
Strength and Weakness”, Kiswahili juzuu 65: 43-58.
14) Bicrwisch.,
M (1970). Semantics.Katika j.Lyons( Mh.) New Horizons in Linguistics.Penguis book.
166-184.
15) Kahigi,
K. (1995). Lugha Katika Vitabu vya Watoto. Kioo cha Lugha (mfululizo mpya)
juzuu 1:21-35.
16) Lakoff,
G. (1987) Women, Fire and Dangerous Things, What categories Reveal About the
mind. Chicago; University of Chicago Press.
17) Lyons,
J. (1977). Semantics.Cambridge .Cambredge University press.
18) Mkude,
D. (1995).Towards a Semantic Typology of the Swahili Language. Institute for
the study of Languages and Cultures of Asia and Africa (ILCAA).
19) Goddarf
C. (1998) Semantic Analysis: A practical Introduction.Oxford: Oxford University
Press.
20) Lakoff,
G. (1987) na M.Johnson, (1980) Metaphors We Live By. Chicago; University of
Chicago Press.
21) Khamis,
S A (1991), “Supperstration and Polysemy in Swahili; A Tentative Study in
Lexical Semantics”, Kiswahili . juzuu 58: 25-33.
22) Barwani
Sheikh, Sauda. 1995. Masomo ya bidii: a Swahili intensive course. Hamburg:
Helmut Buske.
23) Bearth,
Thomas. 1995. Wortstellung, Topik und Fokus. Katika Swahili-Handbuch, wahariri
G. Miehe na W. J. G. Möhlig, k. 173-205. Cologne: Rüdiger Koppe.
24) Dryer,
Matthew S. 1986. Primary objects, secondary objects and antidative. Language
62:808- 845.
25) Sacleux,
Charles. 1939. Dictionnaire swahili-français. (Travaux et mémoires de
l'Institut de 'l'Ethnologie, 36-37.) Paris: Musée de l'Homme.
26) Taasisi
ya Uchunguzi wa Kiswahili. 1990. Kämusi sanifu ya isimu na lugha. Dar es
Salaam: Educational Publishers and Distributors kwa niaba ya TUKI
27) Habwe, J. na Karanja, P. (2007) Misingi ya
Sarufi ya Kiswahili, phoenix
publishers LTD, Nairobi.
28) Holm, P. and Karlgrey, K. (1995) The Theory of
meaning and Different perspective on information System, Stockholm University, Marburg.
29) Lyons, J. (1981) Language;
Meaning and Context, Fontana Paperbacks.
30) Matinde, R. S. (2012) Dafina ya
Lugha Isimu na Nadharia, kwa Sekondari, Vyuo vya Kati na Vyuo Vikuu Serengeti Education publishers (T) LTD, Mwanza.
31) Mdee, S. J. na wenzake (2011) Kamusi ya
Karne ya 21: Kamusi ya Kiswahili yenye Uketo zaidi Katika Karne Hii, Longhorn publishers LTD, Nairobi.
32) Sengo, T. S. Y.M (2009) Fasihi za
Kinchi, The Regestered Trustees of Al
Amin Education and Research Academy, Dar es Salaam.
33) Wamitila, K. W, (2003) Kamusi:
Istilahi na Nadharia, Kenya Focus
Publications LTD, Nairobi
0 Comments