ATHARI ZA VISWAHILI KWA KISWAHILI SANIFU.
Utangulizi:
v
Kiswahili
sanifu:
Kiswahili sanifu ni mtindo wa kusema na hasa wa kuandika lugha ya Kiswahili kwa mujibu wa dhima fulani ambazo
zinachukuliwa kuwa ni muhimu katika jamii.
Waaidha
Kiswahili sanifu ni Kiswahili ambacho mara nyingi kimefanyiwa marekebisho
fulani ambayo yanakiwezesha kukubalika na kutumiwa kwa upana zaidi.
Kiisimu,
Kiswahili sanifu kimesukwa na kufanywa kijipambanue kutokana na ‘Viswahili’
vingine kutokana na sifa kadhaa za kimuundo.
Pamoja
na kuainisha na kufafanua taratibu za ufasaha wake, ni lazima pia kuonyesha
namna zitakazokiwezesha Kiswahili sanifu kijirekebishe kwa kadiri utamaduni wa
jumuia unavyobadilika. Usukaji huu ni pamoja na kuweka taratibu ambazo
zitatawala jinsi ya kukiandika.
Waaidha unaweza kusema kuwa Kiswahili sanifu ni lugha isiyokuwa na
makosa ya kisarufi kwa kuwa huzingatia kanuni zote za lugha ya Kiswahili kama
mofolojia, fonolojia, fonetiki na nyingine nyingi.
v Viswahili:
Hivi ni
vijilugha vilivyo na ujirani na lugha ya Kiswahili sanifu ingawa havijafanikiwa
kujitosheleza kimofolojia, kifonolojia, kifonetiki na kileksia.
Kwa yakini
viswahili vivi hivi vimekuwa na athari sufufu kwa Kiswahili sanifu. Athari zizi
hizi zinajitokeza katika makumbo mbalimbali kama yafuatayo:-
§ Lahaja
§ Sheng
§ athari za lugha
ya kwanza(mama)
§ Rejesta
mbalimbali.
A) Lahaja
Lahaja ni vilugha
vidogovidogo vya lugha moja ambavyo hubainishwa na jamii au jiografia. Lahaja za lugha
moja zinatofautiana katika matamshi, miundo ya sarufi na msamiati.
Dhana hii ya
lahaja imechanganuliwa na wanaisimu mbalimbali. Massamba (2002) anasema kuwa lahaja ni lugha mbalimbali
za pwani zilizokuwa na uhusianao wa karibu sana. Lugha hizo ni kama vile
ci-mbalazi, ki-amu, ki-mvita, ki-jomvu, ki-mtang’ata, ki-makunduchi,
ki-tumbatu, ki-mgao na ki-unguja. Wakati wengine wanaziita lahaja mfano, Polome
(1967), Bryan (1959) pamoja na Temu (1980).
Msanjila (2009:124) anasema lahaja ni lugha
mojawapo kati ya lugha ambazo kimsingi kuhesabiwa kuwa lugha moja isipokuwa
zinatofautiana katika baadhi ya vipengele fulani fulani kama vile lafudhi,
fonolojia, msamiati usiokuwa wa msingi au muundo kutokana na eneo lugha hiyo
inazungumzwa.
Lahaja za Kiswahili hutofautishwa kulingana na maeneo
yake kama Kiunguja (kisiwani Zanzibar) ambacho kimekuwa msingi wa Kiswahili Sanifu Kimvita (eneo la "Mvita" au Mombasa mjini, Kenya) , ambacho zamani kilikuwa lahaja kubwa ya pili pamoja na Kiunguja, Kiamu (kisiwani Lamu, Kenya) na kadhalika.
Mifano mingine ya
lahaja za Kiswahili ni pamoja na:
·
Kimrima: eneo la Pangani, Vanga, Dar es Salaam, Rufiji na Mafia kisiwani (Tanzania)
·
Kimgao: eneo la Kilwa (Tanzania)
·
Kingwana: Kiswahili cha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
·
Shikomoro: Kiswahili cha Komoro
·
Shimaore: Shikomor cha Mayotte (Mahore)
·
Shindzuani: Shikomor cha Anjouan (Komoro)
·
Shingadzija: Shikomor cha Komoro Kuu
·
Kimwani: kaskazini mwa Msumbiji na visiwa vya Kerimba
·
Chimwiini: eneo la Barawa, kusini mwa Somalia
Kwa kuzingatia lahaja
hizi utagundua kuwa lahaja hizi kwa njia moja au nyingine zinakilemaza Kiswahili
Sanifu. Hali hii hujitokeza kwa wale watumizi wa lugha hii kwa wingi pasi
kujali kuwa si rasmi wala sanifu kutumia. Kile ambacho wazungumzi hawa
hawagundui ni kuwa ni lahaja moja tu ambayo iliinuliwa hadhi na kukubalika kama
Kiswahili Sanifu ingawa ao hao bado katika usingizi wa pono huku wakizipigia
debe lahaja zao.
Hebu tutazame
mifano ya maumbo ya maneno katika lahaja mbalimbali ambayo huboronga Kiswahili
Sanifu.
ü Lahaja ya Kimtang’ata : Hii ni lahaja
inayozungumzwa maeneo ya Tanga. Mfano ya misamiati yake ni ;
|
Msamiati katika lahaja ya Kimtang’ata |
Kiswahili Sanifu |
|
||
|
a |
Tombo |
Ziwa |
||
|
b |
Kifugutu |
Kisu(ki)butu |
|
|
|
c |
Mbeko |
Akiba ya nafaka |
|
|
|
d |
Uwanda |
Tambarare |
|
|
Lahaja ya Kitumbatu: Hii ni lahaja
inayozungumziwa katuka kisiwa cha Tumbatu kaskazini mwa Unguja. Mfano wa
misamiati ya lahaja hii ni;
|
Msamiati katika lahaja ya Kitumbatu |
Kiswahili Sanifu |
|
Ulanda |
Kisu kikali |
|
Kifuto |
Kisu kibutu |
|
Angulia |
Piga bao(ramli) |
|
chuchu |
ziwa |
|
Yula |
Yule |
Lahaja
ya Kihadimu; hii
nilahaja inayozungumzwa kisiwani Unguja. Mifano ya msamiati wa lahaja hii ni:-
|
Msamiati katika lahaja ya Kihadimu |
Kiswahili Sanifu |
|
Kule |
Mbali |
|
Rikacha |
Pikicha |
|
vacha |
pacha |
Lahaja
ya Kimvita; hii nilahaja
inayozungumzwa “Mvita” au Mombasa mjini. Mifano ya msamiati wa lahaja hii ni:-
|
Msamiati katika lahaja ya Kimvita |
Kiswahili Sanifu |
|
|
|
a |
Mthezo |
Mchezo |
|
|
b |
Mthuzi |
Mchuzi |
|
|
c |
Thungu |
Chungu |
|
|
d |
Thai |
Chai |
|
Mbali na lahaja ambazo zimeangaziwa hapajuu
ambazo ni za kijiografia zile za kijamii vile vile zina uwezo mkubwa wa
kuboronga Kiswahili Sanifu.Mifano mwafaka ni kama ifuatayo:-
·
katika
kigezo cha kijinsia wanawake hutumia neno shosti na wanaume
hutumia neno msela, wote wakiwa na maana ya rafiki katika
Kiswahili sanifu
·
Pia
kuna kigezo cha kiumri ambapo tunapata msamiati wa lahaja za kijamii kama
vile; demu kwa vijana na binti kwa
wazee ambapo wote wakiwa na maana ya msichana katika Kiswahili sanifu.
Kwa hivyo itafahamika kuwa lahaja huwa na
athari kubwa sana kwa Kiswahili sanifu kwa kuwa wale wanaoizungumza lahaja
teule huku wakaiona kuwa inafaa kabisa basi hutatiza Kiswahili sanifu huku
wenyewe wakijitatiza kwa kukosa kuelewana kikamilifu na wale waliozamia
Kiswahili Sanifu.
Ø Ikumbukwe kuwa lahaja hutotautiana kimatamshi
hali ambayo huathiri Kiswahili sanifu. Mfano wahaya kutoka mkoa wa Kagera
katika matamshi yao hawana kitamkwa ng’ kwa hiyo wanapotamka
maneno kama vile ng’ombe wao hutamka ngombe, neno ng’ang’ania hutamka
ngangania, neno ung’amuzi wao hulitamka kama ungamuzi. Vile vile watu kutoka
mkoa wa Mara ambao ni wakurya hutumia kitamkwa r badala
ya l kwa mfano neno kula wao hulitamka kura, neno
kulala hulitamka kurara, kulalamika wao hulitamka kuraramika.
Ø Pia wazungumzaji kutoka mikoa ya kusini mfano
kutoka mkoa wa Mtwara na Lindi ambao ni Wamakonde wao hutumia kitamkwa n badala
ya m kwa mfano mtoto hutamka kama ntoto, msichana
hutamka kama nsichana, mchana hutamka nchana. Vile vile wazungumzaji kutoka
mkoa wa mbeya ambao ni wanyakyusa wao hutamka f badala
ya v kwa mfano neno viatu vyangu hutamka kama fiatu
fyangu, uvivu hutamka ufifu, viazi hutamka fiasi. Wazungumzaji wa kutoka mikoa
ya kaskazini mfano wapare kutoka mkoa wa moshi hutumia kitakmwa th badala
ya s kwa mfano badala ya kusema sisi sote ni wasichana wao
hutamka thithi thote ni wathichana. Kwa hiyo tofauti hizo za kimatamshi
zinatokana na athari za lahaja za mikoa waliyotoka.
Ø Miundo
ya sentensi vile
vile huathirika. kwa mfano wazungumzaji wa mkoa wa Tabora hutumia wingi mahala
pa nomino ya umoja wakiashiria heshima. Kwa mfano husema baba wanakuja badala
ya kusema baba anakuja, mmefika salama? Badala ya kusema umefika salama?. Kwa
hiyo mtu wa heshima kwao hutumia nomino ya wingi na hii yote ni kutokana na
kuathiriwa na lahaja za mikoa watokayo.
Ø Lahaja nyingine hizi vile vile huathiri mkazo katika maneno hali ambayo
hutatiza mawasiliano.Mkazo ile ni hali ya neno au silabi katika neno kusikika
kuwa na nguvu zaidi kuliko silabi au maneno mengine. Kwa hiyo ulahajia huweza
kuelezea utofauti wa mkazo uliopo katika baadhi ya wazungumzaji wa lugha moja.
Kwa mfano kabila la Wasukuma kutoka mkoa wa Mwanza huweka msisitizo katika
mazungumzo, kwa mfano “baba anakujaa”, pia wanaongeza vitamkwa
ambavyo si vya msingi katika maneno yanayojitosheleaza. kwa mfano neno amekuja
wao huongezea kitamkwa ga, = amekujaga, neno ameenda + ga,
= ameendaga, hakuna + ga.=hakunaga.
B)
Sheng
Yapo madai kuwa
Sheng iliibuka katika mitaa ya Mashariki ya Nairobi mnamo miaka ya sabini
(Osinde1986; Shitemi 2001). Kufuatia kupatikana kwa uhuru 1963, idadi ya wakazi
wa Nairobi ilipanda kwa haraka sana kutokana na kumiminika kwa watu kutoka
mashambani wakitafuta ajira katika mitaa ya viwanda humo jijini. Wananchi hao
maskini waliishia kuishi katika mitaa ya makazi duni ya viwandani Mashariki ya
Nairobi ambayo ni kitovu cha maendeleo ya viwanda.
Ijapokuwa
wafanyakazi hawa pamoja na jamii zao walilazimika kutumia Kiswahili kwa
mawasiliano baina yao, wengi walikichukia Kiswahili kwa vile kilikuwa
kimedunishwa sana na sera ya ukoloni kama lugha ya mashambani, lugha ya vibarua
au “maboi” wa kuwatumikia Wazungu. Hata hivyo, watoto wa wafanyikazi hao
hawakupendelea kuendelea kukitumia Kiswahili kama wazazi wao kwa sababu kadhaa.
Kinyume na wazazi wao, watoto walilazimika kuishi katika hali ya jamii ya
utatu-lugha: 'lugha za kinyumbani’, Kiswahili na Kiingereza. Pia, walitambua
kuwa ingawa walilazimika kutumia lugha nyingi, ni Kiingereza pekee ambacho
kilipewa hadhi kama lugha ya utawala, mamlaka, heshima na uwezo mkubwa wa
kiuchumi.
Ili kuepuka matatizo
ya kimawasiliano na kama njia ya kusuluhisha utata wa hali hiyo iliyowakabili,
vijana hao waligundua msimbo wa mawasiliano kati yao ambao, ingawa ulifuata
sarufi ya Kiswahili, uliazima msamiati kutokana na lugha za kiasili na kuunda
baadhi ya maneno yake. Msimbo huo ndio uliotokea kuwa Sheng hapo baadaye.
Sheng ama lugha simo ni lugha inayotumiwa na watu wa kundi
maalum kwa ajili ya kutaka waelewane wao kwa wao na pengine kuwatenga watu
wengine. Katika mukhtadha huo ni sawa kusema kuwa ni lugha isiyokuwa na mfumo
wa rasmi wa sarufi kwani watu hubuni majina wanavyofikiria.
Majina yanaweza kubuniwa kutoka kwa vipande vya
lugha tofauti, kubadilisha maneo kwa mfano kutoka nyuma ukirudi mwanzo na
kadhalika. Kwa mfano neno bata unaweza kuwasikia vijana wakenya wakisema taba
na kuoga wanasema kugao.
Kutokana na maelezo hayo inaonyesha namna lugha hiyo
inayotajwa kuwa ya kihuni na baadhi ya wasomi wa Kiswahili inatofautiana
kutokana na mtu anachosema na mahali anaposemea. Hata hivyo kwa wataalamu wa isimu jamii ( social linguists) watakupiga
mawe ukikashifu matumizi ya sheng. Wengine hata wamefanyia utafiti kipengee
hicho.
Ingawa kuna mvutano mkubwa kuhusu matumizi ya
sheng ama lugha simo, ni muhimu kutaja kuwa kuna baadhi ya maneno yaliyoanza
kama sheng na yakaswahilishwa. Kwa mfano
nchini Kenya, Matatu ni magari ya uchukuzi wa umma ama matwana kwa Kiswahili
sanifu. Vivyo hivyo, Tanzania chombo hicho kinaitwa daladala ambalo si jina la
Kiswahili sanifu lakini limetiwa katika matumizi.
Hata hivyo kuna hasara kubwa ya kutumia baadhi
ya majina ya sheng ambayo yanapotosha maana halisi ya maneno hayo ya Kiswahili.
Kwa mfano nchini Rwanda mtu akiwa hajakamilika
kwa namna moja au nyingine watu wanamuita kasorobo. Kwa hakika kasorobo ni neno
la Kiswahili kumaanisha kuna upungufu wa robo ya kitu kujalizia mahali fulani
kama vile dakika kumi na tano za saa na kadhalika.
Hivyo inapotumika katika mazungumzo
inawakanganya waswahili. Si hayo tu, Burundi ndio kuna mambo, eti muasi kwa
lugha simo ya huko ni msichana mrembo.Kwa Kiswahili sanifu muasi ni mwanamgambo
ama mtu msumbufu tu asiyeambilika wala kusemezeka.
Kenya na Tanzania ni nchi ambazo zinajulikana pia kuibuka na
misimo mbalimbali na inayopotosha maana halisi ya maneno ya Kiswahili. Nchini
Tanzania wengine huita msichana mrembo Mkwaju. Tunavyojua katika Kiswahili mkwaju ni namna moja ya
kiboko cha kumchapa mtu. Je sasa twabadilisha jina la mrembo kuwa kiboko? Mambo
mawili kando kabisa. Tanzania mtu atakwambia anasikia ubao kumaanisha kuwa
anaona njaa. Inavyoeleweka ni kuwa ubao ni sehemu ya mti ama mbao katika
Kiswahili sanifu. Na huko Tanzania mtu anapokwambia patachimbika ana maana ya
kuwa pameharibika jambo. Utata unaojitokeza hapa ni kuwa patachimbika ni
kitenzi cha Kiswahili kumaanisha hali ya pengine kufanya shimo mahali ama
kutoboa kitu ilhali kuharibika ni kusambatarika kwa hali ama kitu fulani. Hizo
ni dhana mbili tofauti kabisa kama mbingu na ardhi.
Nchini Kenya pia mambo ya sheng yanapigiwa upatu
sana hususan na vijana. Hata hivyo ni muhimu kutaja kuwa matumizi ya maneno
fulani huvuruga Kiswahili Kabisa. Kwa mfano katika lugha simo Kuro ni kahaba
lakini ukweli ni kuwa katika Kiswahili kuro ni mnyama wa porini wa jamii ya paa
anyefanana na kulungu. Yaani hapa kosa la kwanza ni kumlinganisha binadamu na
mnyama. Pili neno mbuyu Kenya lina maana ya baba lakini katika Kiswahili ni mti
unaozaa mibuyu na ikiwekwa semi na iwe "kuzunguka mbuyu" basi
inamaanisha kutoa hongo.
Kadhalika neno demu ambalo linatumika Tanzania, Kenya na Jamhuri ya demokrasia ya
Congo lina maana ya msichana lakini
katika Kiswahili sanifu ni kitambaa kinachofunika mwanamke maziwa anapolima ama
tambara hivi. Je unapomwita msichana demu hujui kwa Kiswahili unamlinganisha
msichana huyo na tambara labda? Je huo ni uungwana? Kenya watu wanasema masa ni mama katika lugha simo lakini
katika Kiswahili sanifu masa ni matendo
mabaya yanayofanywa na mtu.
Athari
nyingine ya lugha simo ni kuwa inaweza kuwafanya watu waache kuyatumia maneno
mengine ya Kiswahili wakidhania ni Sheng. Baadhi ya maneno hayo ni kama vile manzi ambalo ni neno la Kiswahili
sanifu kumaanisha msichana ila wengi hulitumia kama sheng. Ashara kumaanisha idadi kumi ni sawa kwa Kiswahili lakini Kenya
watu wandhania hiyo ni sheng. Mifano zaidi ya msamiati wa Sheng:-
|
Sheng |
Kiswahili
sanifu |
|
|||
|
a |
Mnati, ras |
Rasta
|
|||
|
b |
Babi, barbie |
Mtu
asiyeweza kuzungumza sheng |
|
||
|
c |
Bonga (bong-gah) |
Zungumza/ongea/sema |
|
||
|
d |
Dungia (doong-gi-ah), gawia, chapia, vutia |
Pigia
mtu simu |
|
||
|
e |
Ocha, moshatha |
Sehemu
za mashambani |
|
||
|
f |
Njeve |
baridi |
|
||
|
g |
Ngodha |
chupi |
|
||
|
h |
Fegi, mozo, ngale, fuaka |
Sigara |
|
||
|
i |
Kanjo |
Askari
wa mabaraza ya miji. |
|
||
|
j |
Mboch. |
mjakazi |
|
||
|
k |
Keja, hao, mbanyu, base, diggs |
Nyumba/nyumbani |
|
||
|
l |
Magondi |
Hofu/uwoga |
|
||
|
m |
Karau/kerea |
polisi |
|
||
C)
Athari za sajili kwa Kiswahili
sanifu
Sajili ni mukhtadha/rejista mbalimbali au mitindo
maalum ya lugha katika mazingira/hali mbalimbali. Itakubalika kuwa zipo rejista
ambazo zinaathiri moja kwa moja Kiswahili
sanifu. Hivyo ni kuwa iwapo rejista hizi zitatumiwa kwa kiasi kwamba
zinakuwa katika hali ya Kawaida ya mawasiliano basi Kiswahili Sanifu kitazidi
kupata pigo.
Baadhi ya sajili ambazo hukandamiza Kiswahilisanifu
nikama zifuatazo.
ü Sajili ya Biashara
Lugha ya biashara
huzungumzwa na wauzaji na wanunuzi katika sehemu za kibiashara. Inapaswa
ikumbukwe kwamba lugha hii inaweza kubadilika kidogo kulingana na mazingira.
Kwa mfano, katika mikutano ya kibiashara, lugha rasmi hutumiwa ilihali katika
soko, lugha ya mitaani inaweza kutumika.
Sifa za Lugha ya
Biashara
1. Hutumia
msamiati wa kibiashara kama vile:
Fedha
Faida
Hasara
Bei
Bidhaa
2. Hutumia
misimu ili kuwavutia wanunuzi
3. Ni
lugha yenye malumbano hasa watu wanapojadiliana kuhusu bei
4. Ni
lugha legevu - haizingatii kanuni za lugha.
5. Huchanganya
ndimi kwa kuingiza maneno ya lugha za kigeni
6. Ni
yenye heshima na unyenyekevu kwa wanunuaji
7. Msamiati
katika lugha ya Kibiashara
Mfano
wa Sajili ya Biashara
|
MtuX: |
Tatu kwa mia! Tatu kwa mia! Leo ni
bei ya hasara! |
|
MtuY: |
Unauza hii briefcase kwa pesa ngapi? |
|
MtuX: |
Hiyo ni seventy bob mtu wangu |
|
MtuY: |
Huwezi kunipunguzia. Niuzie hamsini
hivi. |
|
MtuX: |
Haiwezekani mtu wangu. NItapata hasara
nikiuza hivyo. Ongeza mkwaja, mama. |
|
MtuY: |
Basi hamsini na
tano. |
|
MtuX: |
Tafadhali ongeza
kitu kidogo. Unataka nikule hasara leo? Fikisha sitini na tano. |
|
MtuY: |
Basi sitanunua hii.
Sina pesa hizo zote. Unajua uchumi ni mbaya siku hizi. |
|
MtuX: |
Tafadhali mtu
wangu. Huu mkoba ni mzuri sana. Umetoka Germany. Angalia. Unaweka pesa hapa,
kitambulisho hapa halafu unafunga hivi. Hauwezi kupoteza chochote ukiwa na
mkoba huu. Angalia wewe mwenyewe. Hakuna mahali pengine utaweza kununua mkoba
huu kwa bei ghali kama hii. |
|
MtuY: |
Nimekwambia sina
hizo pesa. Nitanunua baadaye ukipunguza bei. |
|
MtuX: |
Lete sixty bob.
Lakini utakuwa umeniumiza. Nakufanyia hivyo kwa kuwa wewe ni customer poa. |
|
MtuY: |
Sawa basi
nitanunua. Shika sixty bob. |
|
MtuX: |
Asante Customer.
Mungu akubariki. (akimfungia) Hey! Tatu kwa mia. Bei ya hasara! Tatu kwa mia! |
ü Sajili ya Bungeni
Hii ni lugha
inayozungumzwa wakati wa kikao cha bunge. Sajili hii ni tofauti na na sajili ya
siasa, ambayo huhusisha wanasiasa wakipiga kampeni.
Sifa za Lugha ya
Bungeni
1. Ni
lugha yenye ushawishi – wabunge hutumia vishawishi ili kuwahimiza wenzao waunge
ama kupinga msalaba
2. Ni
lugha ya mjadala yenye waungao na wapingao.
3. Ni
lugha yenye heshima na nidhamu. Maneno ya heshima kama mheshimiwa, tafadhali na
samahani hutumika sana.
4. Hutumia
maneno maalum yanayopatikana katika mazingira ya bunge kama vile kikao,
mswaada, kuunga mkono, kujadili, kupitisha, n.k.
5. Lugha
ya bungeni ni rasmi na sanifu.
6. Hulenga
maswala mbalimbali ya kisiasa na maendeleo katika taifa.
7. Huwa
na maelezo kamilifu
8. Ni
lugha yenye maswali na majibu miongoni mwa wabunge.
ü
Mfano wa sajili ya Bungeni
|
Spika: |
Waheshimiwa, muda
unayoyoma. Nawaomba mfanye mazungumzo yenu sauti ya chini tumsikize huyu.
Endelea mheshimiwa. |
|
Mbunge 1: |
Asante Bwana spika.
Hii siyo mara ya kwanza ya kuuwasilisha mswaada huu hapa. Kila mbunge
anayethamini raia wa taifa hili ni lazima auunge mkono mswada huu. Katika
kikao kilichotangulia, mliupinga mkidai kwamba hauna heshima kwa rais. Leo
tumefanya ukarabati wote mliotaka. Hamna budi kuuunga mkono. Bwana spika…. |
|
Spika: |
Muda wako umekwisha
tafadhali keti. Wabunge wataamua hatima ya mswada huu ikiwa utapitishwa kama
sheria. Lakini kumbukeni uamuzi wa mwisho ni wa rais |
ü Sajili ya Kidini
Katika sajili ya
kidini tunaangazia lugha inayozungumzwa na waumini/washiriki wa imani fulani
wakati wa ibada, sala, katika nyumba takatifu au mahali popote pale ambapo
wanazungumzia mambo yanayorejelea imani au Mwenyezi Mungu.
Sifa za Lugha ya
Kidini
1. Hutumia
msamiati wa kidini kama vile
Bibilia
maombi
mbinguni
jehanamu
Madhabahu
Paradiso
Mbinguni
Mwenyezi Mungu
Mwokozi
2. Ni
lugha inayonukuu sana hasa wazungumzaji wanaporejelea Kitabu kitakatifu
3. Lugha
yenye heshima, upole na unyenyekevu
4. Lugha
sanifu
5. Ni
lugha iliyojaa ahadi nyingi kwa wanaoandamana na mafunzo ya kidini na vitisho
kwa wanaoenda kinyume na mafundisho
6. Huwa
imejaa matumaini
7. Ni
lugha yenye kutoa maneno ya sifa, kumtukuza na kumshukuru Mwenyezi Mungu
Mfano
wa Sajili ya Kidini
|
Boriti: |
Bwana asifiwe Bi... |
|
Bi Rangile: |
Amina, mchungaji.
Watoto wanaendeleaje? |
|
Boriti: |
Karita hana neno.
Mwenyezi Mungu ametunyeshea rehema na neema zake. Je, wajukuu wako wa hali
gani? |
|
Bi Rangile: |
Wanaendelea vizuri
isipokuwa hawataendelea na masomo. Sijui nilimfanyia Mungu dhambi gani. |
|
Boriti: |
Nasikitika sana
kusikia hivyo. Mungu atawalinda mayatima hao. Yeye ndiye baba wa mayatima.
Mungu ni mwenye huruma. |
|
Bi Rangile: |
Sijui hayo,
mchungaji. Hata sijui maana ya kuishi hapa duniani. Kila siku ni matatizo. |
|
Boriti: |
Usife moyo. Mungu
anasema katika kitabu cha Yohana 14:18, "Sitawaacha nyinyi kama
mayatima..." Kwa hivyo, ukiwa na imani, Mungu atakuonekania. |
|
Bi Rangile: |
Basi niombee
mchungaji ili Saumu na Neema wapate karo ya kurudi shuleni. |
|
Boriti: |
Funga macho tusali.
Ewe Rabuka uliyejaa neema na baraka tele. Tunakushukuru na kulitukuza Jina
lako takatifu kwa baraka zako za ajabu. Tunajua kwamba wewe ndiye Mungu
uliyewatoa wana wa Israeli kutoka Misri. Sisi wenye dhambi tunakuja mbele
yako tukiomba ukafanya miujiza katika nyumba hii ya Bi Rangile...... |
|
Wote: |
Amina. |
Sajili ya Kisayansi
Sifa za Lugha katika
sajili hii
1. Hutumia
msamiati wa kipekee unaoambatana na taaluma inayorejelewa.
2. Huwa
na maelezo kwa ukamilifu.
3. Huwa
na mpangilio maalum na maendelezo ya hoja na ujumbe.
4. Huchanganya
ndimi na kutumia maneno ya kisayansi au lugha mbalimbali.
5. Hutumia
lugha sanifu.
6. Ni
lugha yenye udadisi mwingi (wakati wa kufanya utafiti)
Kwa sababu zisizoweza
kuepukika, kikundi chetu hakitamaliza utafiti ulioratibiwa kukamilishwa
mwishoni mwa mwezi ujao. Hii ni kwa sababu ya changamoto kadhaa ambazo
tumekutana nazo. Kwanza, viluwiluwi, ambao ndio tunaotafiti wamekuwa haba sana
wakati huu wa ukame. Pili, kutokana na kufungwa kwa maabara ya kisayansi katika
taasisi hii, ni muhali kufanya majaribio yoyote ya kazi yetu. Tatu, kumekuwa na
pingamizi kubwa kutoka kwa baadhi ya wanakijiji kwamba kukusanya viluwiluwi
kunawatia hofu. Aidha, tume yetu imepungukiwa na fedha baada ya serikali kusitisha
kudhamini utafiti huu.
Baada ya kujadiliana
kwa vikao tatu mfululizo, tume yetu inapendekeza haya: Muda wa kufanya utafiti
uongezewe kwa kipindi cha miezi sita; serikali kupitia kwa taasisi hii ifadhili
wachunguzi. Wananchi wahamasishwe kuhusu umuhimu wa kuwafanyia viwavi utafiti
na maabara ya utafiti ikaraatiwe haraka iwezekanayo.
Sajili ya Mahakamani
Hii ni lugha
inayozungumzwa na wanasheria, mahakimu, mawakili, washitakiwa na mashahidi
katika mahakama.
Sifa za Lugha ya
Mahakamani
1. Hutumia
msamiati wa kipekee unaorejelea sheria kama vile
katiba
sheria
mashtaka
Hakimu
Ushahidi
Wakili
Jela
Mshitakiwa
Kiongozi wa mashtakiwa
2. Huwa
na maelezo marefu na ya kina ili kutafuta ushahidi wowote uliopo
3. Ni
lugha yenye kunukuu sana hasa vipengele katika vitabu vya sheria kama vile
katiba
4. Ni
lugha rasmi na sanifu
5. Ni
lugha iliyojaa maswali na majibizano
6. Ni
lugha yenye heshima
Mfano
wa Sajili ya Mahakamani
|
Kiongozi: |
Musa Kasorogani,
mwanaye Bi Safina na Mzee Mpotevu Kasorogani; umeshtakiwa kwa kosa la jaribio
la mauaji mnamo tarehe 23/08 mwaka huu. Unaweza kukubali mashitaka, kukana au
kunyamaza. Je, unakubali mashitaka. |
|
Musa: |
Naomba kukanusha
mashtaka hayo, bwana mkubwa. |
|
Kiongozi: |
Je, kuna shahidi
yeyote katika kesi hii? |
|
Katili: |
Hapa mkubwa. Siku
hiyo ya tarehe 23/08, Musa alipatikana akiwa akijinyonga usiku wa maneno.
Kijiji chote kilikusanyika hapo kwenye boma ya Kasorogani. Nilipoleta polisi,
wakamkamata na kumpeleka hospitalini atibiwe kwanza. Ndiposa ameletwa hapa siku
ya leo. |
|
Kiongozi: |
Je, mshitakiwa una
tetesi lolote. Ama pia unaweza kuleta wakili wako azungumze kwa niaba yako. |
|
Kisaka: |
Bwana mkubwa, mimi
ndiye wakili na shahidi wa Musa. Musa hakuua mtu. Alikuwa akijinyonga
kutokana na mkasa uliomfika tarehe hiyo ya Agosti 23 baada ya bibi harusi
wake kubadilika. Mimi na mamake, Bi Safina Kasorogani tulijaribu kumtuliza
jioni hiyo. Asubuhi nilipoamka siku iliyofuatia, nikapata habari kwamba
alikuwa amepelekwa hospitalini. Je, alipojaribu kujiua, alimwua mtu yeyote? |
|
Kiongozi: |
Kulingana na katiba
ya nchi hii, kifungu cha 12.ab, kuua ni kutoa uhai wa binadamu yeyote.
Haijalishi ikiwa ni yeye mwenyewe au ikiwa ni rafiki yake. Hivyo basi jaribio
la kujiua ni hatia kulingana na kanuni za nchi hii. Una jingine la kuulizia? |
|
Kisaka: |
Je, sheria yetu
inaruhusu mtu kuadhibiwa kwa kosa ambalo hakufanya? |
|
Kiongozi: |
La hasha. |
|
Kisaka: |
Basi tutakuwa
tumekiuka kanuni za nchi yetu iwapo tutamhukumu Musa kwa kujiua ilhali
hakujiua bado. Tunawezaje kutambua kama angekufa? |
|
Katili: |
Inafaa ahukumiwe
kinyonga au kifungo cha maisha gerezani. Hata alivunja simu yangu... |
|
Kiongozi: |
Order! Lazima kutii
mpangilio wa mahakama. Katili hauruhusiwi kuongea bila ruhusa ya hakimu au
kiongozi wa mashitaka. Polisi, mpelekeni nje. |
ü Sajili ya Michezoni
Lugha ya michezoni
hutumiwa wakati wa mashindano ya michezo kama vile kandanda, ukimbiaji n.k Hii
inaweza kuwa lugha ya watangazaji/wasimulizi wa mchezo, watazamaji, mashabiki
au wachezaji.
Sifa za Lugha ya
Michezoni
1. Hutumia
msamiati wa kipekee unaohusu michezo kama vile mpira, goli, mchezaji
2. Huchanganya
ndimi na kuingiza maneno ya lugha nyingine kama vile Kiingereza. mfano
'goal!!!'
3. Ni
lugha ambayo hutumia vihisishi na mshangao kwa wingi
4. Sentensi
nyingi katika lugha hii huachwa bila kukamilika hasa hali inapobadilika
uwanjani
5. Husimuliwa
kwa haraka haraka ili kuambatana na kasi ya mchezo
6. Ni
lugha yenye sifa na na chuku kwa mfano msimulizi anaposimulia sifa za mchezaji
fulani
7. Hutumia
misimu kama vile 'wametoka sare'
8. Hutumia
kwa ya kulinganisha ili kuelezea matokeo ya mechi k.m 'walitoka mbili kwa
nunge'
9. Ni
lugha yenye kukariri (kurudia rudia) hasa mchezaji anapoumiliki mpira kwa muda
mrefu au mwanariadha fulani anapoelekea kushinda katika mbio.
10. Huwa na sentensi fupi fupi
Mfano
wa Sajili ya Michezoni
Nakwambia ndugu
msikilizaji hapa mambo yamechacha kwelikweli. Hawa wachezaji wa Manyuu
hawacheki na watu leo. Wameamua kuishambulia timu ya Cheusi bila huruma.
Kumbuka kwamba hii ni mara yao ya... Lo! Anauchukua mpira pale, mchezaji
nambari tisa... Matiksta. Matiksta, Matiksta na mpira. Anaucharazacharaza pale.
Anamwangalia mwenzake. Anaupiga mpira kwa kichwa pale! Lo! Mwenzake anaukosa.
Akiushika mpira pale ni mchezaji wa timu ya Cheusi, Romana. Romana, Romana
anaelekeza mpira kwenye lango la Manyuu. Anaupiga mpira kwa nguvu! Lo! Hatari
sana. Hatari sana katika lango la Manyuu. Hatari! hatari! Goooooooooo ooooh!
Wameukosa! Goal keeper ameudaka mpira huo. Pole sana wachezaji wa ... Mlinda
lango anaupiga mpira huo kwa hasira. Juu kabisa. Anauchukua pale nambari saba,
Saruta. Huyu ni mchezaji machahari sana. Mwaka uliopita, alipewa tuzo la
mchezaji bora wa mwaka. Ananyang'anywa na mchezaji mwingine hapa. Wanakabiliana
kidogo. Huyu mchezaji anaupiga mpira kwa mguu wa kushoto. Lo! Mpira umekuwa
mwingi na ukatoka nje.
Mashabiki wa timu
hizi mbili wanasubiri kwa hamu na ghamu kutambua ni nani atakayeibuka mshindi.
Katika mechi zilizotangulia, timu hizi zimekuwa zikitoka sare. Lakini leo lazima
mshindi atapatikana. Hawa ni fahali wawili. Kumbuka kwamba unapata matangazo
haya moja kwa moja kupitia idhaa yako uipendayo, redio nambari moja kote
nchini... Mpira unarudishwa uwanjani. Akienda kuurusha pale ni...
ü Sajili ya Mitaani
Lugha ya mitaani ni
lugha inayozungumzwa na vijana mtaani.
Sifa za Lugha ya
Mtaani
1. Ni
lugha legevu isiyozingatia kanuni za kisarufi
2. Huchanganya
ndimi
3. Hutumia
misimu kwa wingi
4. Hukosa
mada maalum
Mfano
wa Sajili ya Mtaani
|
Chali: |
Hey, niaje msupaa? |
|
Katosha: |
Poa. So, mathee
yako alikushow naweza kuja? |
|
Chali: |
Ha! Masa hana noma.
Si unajua nita... |
|
Katosha: |
Chali! Unataka
aniletee problem? |
|
Chali: |
Mimi ni boy wa
maplans. Ngoja nifikirie venye tutamshow |
|
Katosha: |
Na by the way,
kwani umejipaka mafuta ya manzi. Ama ulikuwa na msichana mgani? |
|
Chali: |
Oh! Niliscoop
mafuta ya Anita. Si unajua nataka kunukia hmmmm... |
|
Katosha: |
Ok. So, umefikiria
tumshow nini masa yako? Ama nikona idea poa. |
|
Chali: |
Nishow hiyo plot,
na by the way, nataka unisaidie kuhusu ile deal yangu na Kaunda. Ile ya siz
yangu. |
|
Katosha: |
Kwanza tutaplan na
huyo siz yako, niwe ndiye nimekuja kuvisit. Mamako atakubali |
|
Chali: |
Wow! Idea poa.
Utakuwa umekuja kufanya homework. Halafu masa akiishia kwa bed. Homework
tutaitupa mbali. |
|
Katosha: |
So, utamshow Anita
nakuja tufanye homework... |
D) Athari za lugha ya kwanza (mama)
Kiswahili sanifu vile vile huathirika kwa
kiwango kikubwa na lugha za kwanza(mama) za wanaokizungumza. Lugha hizi
huathiri pakubwa silabi pamoja na lafudhi ambapo wanazungumza lugha hizi, wengi
wao wameathirika kiasi kwamba wanazihamisha silabi zao asilia hadi kwa
Kiswahili huku wakiwa na dhana kuwa wanakijenga kumbe wanakibomoa Kiswahili
Sanifu.
. Hili huwa tatizo kubwa sana kiasi kwamba
sarufi za lugha za mama haziingiliani na sarufi ya Kiswahili sanifu.
Kwa mfano katika nafsi za Kiswahili Sanifu tunapata viwakilishinafsi vifuatavyo:
|
NAFSI |
UMOJA |
WINGI |
|
1 |
NI |
TU |
|
2 |
U |
M |
|
3 |
A |
WA |
Zipo baadhi ya lugha mama hasa za kinailoti
ambazo huvitumia au kuhamisha viambishi
nafsi vya lugha yao hadi Kiswahilipasi kufahamu madhara wanayoyaleta kwenye
sarufi ya Kiswahili.
Kwa mfano katika lugha ya Waluo, utagundua
kwamba wao hutumiwa kiwakilishinafsi A
kurejelea nafsi ya kwanza hali ya umoja ambapo katika Kiswahili huwa nafsi ya
tatu umoja.
Utawaskia wakisema :
a.
Abiro-Ninakuja
b.
Adwaro-Ninataka
Katika mtindo huo, wapo wale ambao huhamisha
nafsi hii namna ilivyo hadi kwenye Kiswahili. Utawaskia wakisema:
a. Mimi
anaenda shuleni. Badala ya :Mimi ninaenda shuleni.
b. Mimi anaandika
polepole.Badala ya:Mimi ninaandika
polepole.
c. Mimi anasoma
haraka. Badala ya:Mimi ninasoma
haraka.
Kwa kufuata mifano ya hapo juu itaonekana
wazi kuwa wanaotoka maeneo hayo ambao
huitumia lugha yao ya kwanza kama kioo wanapozungumza Kiswahili basi wana kazi ya ziada.
Hivyo basi wahusika hawa hustahili kuiacha
kando lugha yao ya mama wanapoikabili sarufi ya Kiswahili la sivyo hali
itawaendea mrama.
Waaidha zipo lafundhi za lugha hizi za kwanza
ambazo huathiri sana sarufi ya Kiswahili katika lugha ya Kikamba wengi wao
hutamka konsonanti J kama Y. Utagundua kwamba asilimia kubwa ya Wakamba
wanapozungumza mahali palipo na J watatamka Y.
Kwa mfano:
|
KISWAHILI |
KIKAMBA |
|
Jua |
Yua |
|
Juu |
Yuu |
|
Juni |
Yuni |
Waaidha palipo na sauti G wao hupachika NG
Kwa mfano:
|
KISWAHILI |
KIKAMBA |
|
Goli |
Ngoli |
|
Gareji |
Ngaleji |
|
Goti |
Ngoti |
Palipo
na R wanaweka L.
|
KISWAHILI |
KIKAMBA |
|
Rudi |
Ludi |
|
Rarua |
Lalua |
|
Rinda |
Linda |
|
Mrembo |
Mlembo |
Mfano mhusika hataeleweka iwapo ataambiwa
aisome sentensi kama hizi;
a.
“Linda ana rinda refu lililoraruka vibaya.”
b.
“Mimi ni fundi wa kupaka rangi”
Utamsikia mhusika akitamka:
a.
“Linda ana linda lebu lililolaluka bimbaya.”
b.
“Mimi ni bundi
wa kubaka langi.”
Katika hili kama hii sarufi Kiswahili sanifu hufanywa
chapwa mno.
Katika mfumo huo, jamii ya Waluhyia
haijasazwa nje. Katika jamii hii utagundua kuwa lafudhi yao wakati mwingine
huwatia mashakani katika uchambuzi na usomi wa Kiswahili.
Wengi wao badala ya sauti B hutia P, Sauti Z
hutia S, D hutia T
Kwa mfano:-
|
Matamshi bora ya Kiswahili |
Matamshi bandia ya Kiluhyia. |
|
|
1 |
Baba |
Papa |
|
2 |
Bora |
Pora |
|
3 |
Bata |
Pata |
|
4 |
Bure |
Pure |
|
5 |
Bei |
Pei |
|
6 |
Birika |
Pirika |
|
7 |
Bila |
Pila |
Sauti Z na S
|
Matamshi bora ya Kiswahili |
Matamshi bandia ya Kiluhyia. |
|
|
1 |
Mzuri |
Msuri |
|
2 |
Mzee |
Msee |
|
3 |
Mzinga |
Msinga |
|
4 |
Muziki |
Musiki |
|
5 |
Mkizi |
Mkisi |
|
6 |
Zambarau |
Sambarau |
|
7 |
Mzigo |
Msiko |
Sauti D na T
|
Matamshi bora ya Kiswahili |
Matamshi bandia ya Kiluhyia. |
|
|
1 |
Dada |
Tata |
|
2 |
Daktari |
Taktari |
|
3 |
Dadisi |
Tatisi |
|
4 |
Dereva |
Tereva |
|
5 |
Darasa |
Tarasa |
|
6 |
Domo |
Tomo |
|
7 |
Daka |
Taka |
Kwa kuangaziwa athari za hapo juu ni
dhihirisho tosha kuwa kufundisha sarufi katika mazingira hayo huwa kugumu sana.
Tatizo kubwa ni kupata kuwa kila mmoja ana shida moja ingawa hakuna anayegungua shida kama hiyo miongoni mwao.
Hivyo basi, ni muhimu kwa msomi au mwelekezi
ambaye kwa njia moja au nyingine ana tatizo kama hili basi ni muhimu kuzingatia
sauti za Kiswahili sanifu pamoja na
konsonanti zote hukuakitilia maanani matamshi bora ambayo hayataathiriwa na
lugha zao za kwanza.
Kwa hivyo athari kama hizi vile vile ni
kuangaziwa kwa somo linalohusu konsonanti na sauti katika Kiswahili ili kujenga
msingi imara katika matamshi ambayo huathiri sana Kiswahili sanifu
Hitimisho.
Kwa yakini viswahili sanifu kina mapigo aina
ainati ambayo yanakiathiri kucha kutwa.Baadhi ya mapigo haya hutokana moja kwa
moja na watumizi wa Kiswahili wenyewe ambao kwamba hawakitumii kwa kuzingatia
kanuni zilizowekwa bali shaghalabaghala.Hivyo basi niwajibu wa kila mmoja kuona
kuwa anapoitumia lugha hii ya Kiswahili, azingatie kanuni zote za kisarufi.
Waaidha yapo makosa yatokanayona mazingira
ambayo kwa upande wake huwa na athari kubwa sana. Ni jambo la busara kwa yeyote
kubaini kuwa usanifu wa Kiswahili ni swala nyeti la kuvaliwa njugabila
simile.La sivyo hali hii ya mazigira huenda ikaleta utata mkubwa sana.
Ni wajibu piawa kila mmoja kugungua kuwa baadhi ya lugha zetu za kwanza
imaziwe za kibantu ama kinailoti, zina tofauti kubwa sana na Kiswahili sanifu.
Hivyo basi ni jambo la msingi kwa kila mmoja kutofauti silabi za lugha zao za
mama na silabi au sauti za Kiswahili hasa sanifu. Kwa wengi hufanya makosa
pasipo hata wenyewe kufahamu kuwa wametenda makosa.
iwapo kila mmoja atakitumia Kiswahili kwa
usanifu ufaao, basi kwa vyovyoteviwavyo lugha hii itakua na kuimarika na
usanifu wake. Hivyo basi ni jukumu la kila mmoja kuitetea lugha hiikwa kuona
kuwa usanifu wake unabaki na kutumika itakikanavyo.
MAREJELEO
a. King’ei, K. (2010). Misingi ya
Isimujamii.Taasisi ya Taaluma za Kiswahili. Chuo kikuu cha Dar es salaam.
b. Mlacha, S.A.K. na Hurskainen, A.
(1995). Lugha, Utamaduni Na Fasihi Simulizi ya Kiswahili. Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam na Idara ya Taaluma za Asia na Afrika na Chuo Kikuu cha
Helsinki. TUKI
c. Msanjila, Y.P na wenzake. (2011). Isimujamii:
Sekondari na Vyuo. TUKI. Dar es salaam.
d. TUKI, (2004).Kamusi ya Kiswahili Sanifu.
(Toleo la Pili). East Africa: Oxford University Press na Taasisi ya Uchunguzi
wa Kiswahili (TUKI).
e. Crystal, D. (2002). The Cambridge of
Encyclopedia of Language: Second edition. London. Cambridge University
Press.
f. Halliday, M.A.K. (1990). Spoken and
Written Language. London. Oxford University Press.
0 Comments